Tuesday, April 30, 2013

KUTOKA BUNGENI - KAMBI YA UPINZANI YAMCHANA KINANA


Waziri wa Mmbo ya Ndani ya Nchi-Tanzania, Dk Emmanuel Nchimbi akishambulia Upinzani wakati akichangia mjadala wa kupitisha makadirio na matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2013/14 mjini Dodoma LEO. Dodoma, Tanzania. Kambi ya Upinzani kupitia kwa Msemaji  Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema), LEO ‘amemchana’ Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulharaman Kinana kwamba amekuwa akishiriki kikamilifu kufanya biashara ya pembe za ndovu zenye uzito wa tani nne.

Msigwa katika hutuba yake aliyosoma bungeni Leo amesema kwamba pembe hizo ziliripotiwa kukamatwa nchini Tanzania na Kenya mwaka 2009 na vyombo vya usalama vya Vietnam na kwamba pembe hizo zilisafishwa na kampuni ya wakala ya Sharaf Shipping Co. Ltd.

“Taarifa za Wakala wa Usajili wa Biashara na Makampuni (BRELA) zinaonyesha kwamba Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana anamiliki robo tatu ya hisa za Sharaf Shipping Co. Ltd., wakati robo iliyobaki ya hisa hizo inamilikiwa na mtu aitwaye Rahma Hussein. Kwa mujibu wa taarifa ilizonazo Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Rahma Hussein ni mkewe Abdulrahman Kinana.


“Sio tu kwamba kampuni ya Katibu Mkuu wa CCM na mkewe imehusishwa na usafirishaji haramu wa pembe za ndovu kutoka Tanzania, kampuni hiyo inaelekea kutoa
ajira haramu kwa wageni. Wakati shehena ya meno hayo tembo inakamatwa nchini Vietnam, nyaraka zilizoambatana na shehena hiyo zilionyesha kwamba kibali cha
kusafirisha shehena hiyo kilisainiwa na raia wa India anayeitwa Samir Hemani mnamo tarehe 13 Novemba 2008. Hemani alikuwa Meneja wa Fedha na Utawala wa
Sharaf Shipping Co. Ltd.
"Hata hivyo, nyaraka za Idara ya Uhamiaji ambazo Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imezipata zinaonyesha kwamba wakati Hemani anasaini
kibali cha kusafirisha shehena ya meno ya tembo kwa niaba ya wateja wa Kinana na mkewe, kibali chake cha kuishi Tanzania kilikuwa kimeisha tangu tarehe 7
Mei, 2008,” amesema Msingwa ambaye ni Waziri Kivuli wa Wizara ya Maliasili na Utalii,  wakati LEO akiwasilisha Bungeni makadirio ya matumizi kwa mwaka wa
fedha 2013/2014.

Waziri Nchimbi Aishukia Chadema Bungeni

Wakati Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akichangia mjadala wa kupitisha makadirio na matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka
wa fedha 2013/14 mjini Dodoma, ameishambulia kambi ya upinzani bungeni ikiwamo Chadema kwamba ni waongo na ameshangwa na kaili iliyotolewa na Msingwa.

Waziri Nchimbi ameishukia Chadema kueleza kwamba hoja zilizojengwa dhidi ya Katibu Mkuu wa CCM, Kinana na msemaji wa upinzani (Msigwa) kwamba Kinana
anasafisha biashara ya pembe za ndovu nje ya nchi ni uongo mtupu.

“Nimejaribu kufuatilia kwa makini alichokisema alikimaanisha, alikielewa, alikitafakari au aliandikiwa tu akaenda kusoma, baada ya kutafakari kwa kina
nikagundua hakuwa na nia mbaya, aliandikiwa tu na ameenda kusoma,” amesema Dk Nchimb

MAELEZO KUHUSU HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA



 
Wilaya ya Muleba ni mojawapo ya Wilaya saba zinazounda Mkoa wa Kagera. Wilaya hii ipo kati ya longitude 31 o 30' na 32 o 5' Mashariki ya Griniwich na Latitude 1 o 30' na 2 o 20' Kusini ya Ikweta.
Kabla ya mwaka 1975 Wilaya ya Muleba ilikuwa ni Tarafa mojawapo ya Wilaya ya Bukoba. Mwaka 1975 tarafa ya Muleba ilipewa hadhi ya kuwa Wilaya na makao yake makuu yalikuwa Kaigara. Mwaka 1977 majengo ya uhakika ya ofisi yalijengwa Kibonwangoma – eneo ambao lilikuwa ni maarufu kimila kwa shughuli za watemi (Bakama) na utawala wa Wilaya ulihamia huko. Shughuli za Halmashauri hata hivyo hazikuanza mara moja hadi mwaka 1984.
 
 
 
Wilaya inapakana na Wilaya ya Bukoba upande wa Kaskazini, Magharibi inapakana na Wilaya ya Karagwe, Kusini inapaka na Wilaya ya Biharamulo, Kusini Mashariki inapakana na Wilaya ya Chato na Mashariki inapakana na Mkoa wa Mwanza.
Wilaya ina eneo la kilomita za mraba 10,739 na kati ya hizo kilomita za mraba 3,444 ni nchi kavu na kilomita za mraba 7,295 ni eneo la maji hususani Ziwa Victoria . Eneo la nchi kavu linahusisha pia zaidi ya visiwa ishirini vilivyomo katika Ziwa Victoria .
JIOGRAFIA YA WILAYA
Wilaya ya Muleba imetawaliwa na vilima, mabonde na tambarale (plateaus). Wilaya ipo kati ya mwinuko wa mita 1,150 na 1,667 kutoka usawa wa bahari na sehemu ya juu kabisa ni Karambi. Mto Ngono unakatisha wilaya kuanzia Kusini kuelekea Kaskazini ambapo unaungana na Mto Kagera unaomwaga maji yake katika Ziwa Victoria.
Wilaya imegawanyika katika kanda kuu nne za kilimo ambazo ni: Ukanda wa mwambao wa Ziwa na Visiwa katika Ziwa Victoria, Ukanda wa juu, Ukanda wa chini Kusini na Ukanda wa Burigi. Ukanda wa mwambao wa Ziwa na ukanda wa juu unapata kipindi kirefu cha unyevunyevu (miezi 8 – 9) wakati ukanda wa chini na wa Burigi unapata kipindi cha unyevunyevu cha miezi 3 – 4 tu kwa mwaka.
Mvua zinanyesha zaidi upande wa Kaskazini – Mashariki yaani milimita 1800 wakati Kusini – Magharibi ni pakame. Kwa kufuata viwango vya miinuko na mvua, Wilaya inakuwa na kanda za kilimo tofauti zenye mazao mbali mbali yanayopandwa katika misimu tofauti.
Hali ya rutuba ya udongo si ya kuridhisha hasa kutokana na mvua nyingi zinazosababisha kuondolewa kwa virutubisho udongoni. Hata hivyo maeneo ya mabonde ya upande wa Kusini – Magharibi na miinuko tambarale (plateaus) yana rutuba ya kutosha wakati maeneo ya mwambao wa ziwa hayana rutuba.
IDADI YA WATU
Kulingana na takwimu za sensa ya watu na makazi za mwaka 2002 na ongezeko la watu la asilimia 2.5 kwa mwaka wilaya kufikia mwaka huu wa 2008 inakadiriwa kuwa na jumla ya watu wapatao 453,931 na kati ya hao watu 225,891 ni wanaume na watu 228,039 ni wanawake.
Msongamano wa watu kwa kilomita ya mraba ni 110. Watu wenye uwezo wa kufanya kazi ni asilimia 24 ya watu wote wakati watu wenye umri wa kwenda shule ni asilimia 30, zipo kaya 81,084 na wastani wa watu katika kaya ni 4.7.
Jedwali Na.1, 2 na 3 hapa chini vinachambua kwa kina takwimu za sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002 kama ifuatavyo:-
Jedwali Na. 1 : Idadi ya watu kwa umri na jinsi
Umri
Me
Ke
Jumla
0 -1
29718
32219
61937
1 – 5
29860
30760
60620
6 – 14
31518
28519
60037
15 – 24
34951
33697
68648
25 – 44
29331
25584
54915
45 – 60
19971
22957
42928
60+
16903
20340
37243
Jedwali Na. 3: Mlinganisho wa jinsi katika Grafu
Jedwali Na. 3: Idadi ya watu Kitarafa.
Tarafa
Idadi ya Kata
Idadi
ya vijiji
Idadi ya Mitaa
Me
Ke
Jumla
Muleba
6
22
2
27354
27760
55114
Izigo
6
25
 
9123
8893
18016
Kamachumu
4
15
 
29988
30759
68648
Nshamba
9
39
 
72769
73398
146167
Kimwani
6
31
 
53018
53266
106284
Total
31
132
2
192252
194076
386328
 
UTAWALA NA UONGOZI KISIASA
KIUTAWALA
Kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali Na. hapo juu wilaya ya Muleba imegawanyika katika Tarafa tano (5) nazo ni Izigo, Kamachumu, Muleba, Nshamba na Kimwani. Tarafa hizo tano nazo zimegawanyika katika kata 31, vijiji 132, mitaa 2 na vitongoji 677.
KISIASA
Wilaya pia imegawanyika katika majimbo mawili ya uchaguzi. Jimbo la Muleba Kusini linaongozwa na Mh. Anna Tibaijuka (Mb) na Jimbo la Muleba Kaskazini linaongozwa na Mh. Mwijage (MB), na wote wawili wanatoka Chama Tawala cha CCM.
Upande wa Kata, Kata zote 30 zinao madiwani wa kuchaguliwa ambapo kata moja iko wazi baada ya diwani wake kufariki dunia na Kata 2 madiwani wake ni wa kutoka kambi ya upinzani. Madiwani hawa wote ni wanaume. Wapo pia madiwani 11 wanawake wa viti maalum ambapo 8 ni wa kutoka chama cha CCM na 3 wanatoka kwenye vyama vya TLP 1 na CUF 2.
 

UCHUMI
Pato la mwananchi wa Muleba linakadiriwa kuwa kati ya Tshs. 100,000 – 150,000 kwa mwaka. Hali hii ni chini ya mstari wa umaskini hivyo kuashiria kuwa wilaya hii ni kati ya wilaya maskini sana katika nchi ya Tanzania .
Zaidi ya asilimia 90 ya wakazi wa Muleba wanategemea zaidi shughuli za kilimo kwa maisha yao ya kila siku. Zao kuu la biashara ni kahawa na mazao ya chakula ni ndizi na maharage. Kuporomoka kwa bei ya kahawa kumewakatisha tamaa wakulima hivyo kupelekea kutothanimi zao hili.
Zao la ndizi pamoja na kuwa ni zao la chakula pia huwapatia wakulima kipato kwani huuzwa katika masoko ya nje ya wilaya na mikoa jirani kama Mwanza na Shinyanga. Pia zao hili huwapatia wakulima kipato wanapotengeneza pombe ya kienyeji (Rubisi). Maharage mara nyingi hutumiwa na familia wakati zao la chai halipewi kipaumbele baada ya bei yake kuwa ya chini sana hivyo kupelekea wakulima kutelekeza mashamba.
 
           
           
 

MAELEZO YA JUMLA KUHUSU MKOA KAGERA


 
Mkoa wa Kagera unapatikana kaskazini magharibi mwa nchi ya  Tanzania. Makao makuu ya mkoa yapo katika mji wa Bukoba umbali wa kilometa 1500 kutoka Dar es Salaam, mkoa huu unapakana na nchi ya Uganda kwa kaskazini, Rwanda na Burundi kwa upande wa magharibi mkoa wa Kigoma, Mwanza kwa upande wa kusini na ziwa Victoria kwa upande wa mashariki. Vile vile mkoa wa Kagera uko kusini mwa ikweta kati ya 1 “00” na 2”45” latitudi. Kwa Iongitudo uko katika nyuzi 30”25” na 32”40” Mashariki mwa ‘greenwich'.
Mkoa wa Kagera ulijulikana kama “Ziwa Magharibi” jina hili lilidumu katika kipindi cha ukoloni na baada ya uhuru mpaka mwaka 1979 baada ya vita kati ya Tanzania na Uganda.
Mkoa ulipata jina hili kutokana na mto Kagera ambao hutiririsha maji yake kutoka Rwanda kupitia kaskazini na kumwaga maji yake katika ziwa Victoria.
Mkoa wa Kagera una jumla ya eneo la kilomita za mraba 39,168 kati ya hizo kilometa za mraba 28,513 ni eneo la nchi kavu za kilomita 10,655 ni eneo la maji. Ukiacha mbali wilaya za Biharamulo na Chato ambazo ni tambarare sehemu kubwa ya mkoa ni yenye milima na vilima vilivyogawanywa na mabonde yenye matingatinga. Upande wa magharibi wa mkoa mito mingi inamwaga maji yale katika mto Kagera ambao nao humwaga maji yake katika ziwa Victoria.

Hali ya hewa
Hali ya hewa ya mkoa wa Kagera kwa ujumla ni ya joto la wastani wa 26.02 sentigredi. Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800-1,100 kwa mwaka kati ya mwezi Septemba na Januari na kati ya mwezi Machi na Mei. Mvua hizi ndizo zinazowezesha kuwepo kwauoto wa asili wa kuvutia katika maeneo mengi ya mkoa. Kwa miaka ya kawaida mkoa hupata mvua za uhakika za vuli na masika ambazo ni muhium kwa shughuli za kilimo na ufugaji.

UTAWALA
 
Wakati tunapata UHURU, mkoa wa Kagera ulikuwa na jumla ya wilaya nne (4), wilaya hizo ni Ngara ambayo ilianzishwa mwaka 1947, Biharamulo, Bukoba, na Karagwe mwaka 1958 ambayo ilizinduliwa rasmi na gavana wa kiingereza Sir Richard Turnbul. Aidha, mwaka 1975 wilaya mpya ya Muleba ilianzishwa kutoka kwenye wilaya ya Bukoba na mwaka 2007 wilaya ya Chato na Missenyi zilianzishwa na kuunda jumla ya wilaya 7 za mkoa wa Kagera.
Kwa sasa mkoa wa Kagera una jumla ya wilaya saba (7) na halmashauri 8. Wilaya hizo ni Bukoba, Muleba, Biharamulo, Ngara, Chato, Karagwe, Missenyi na Ngara. Halmashauri ni Bukoba Manispaa, halmashauri ya wilaya ya Bukoba, Muleba, Biharamulo, Ngara, Chato, Karagwe na Missenyi.
Kisiasa mkoa una jumla ya majimbo 10 ya uchaguzi (Muleba 2, Karagwe 2, Ngara 1, Biharamulo 1, Missenyi 1, Bukoba Manispaa 1, Bukoba Vijijini 1 na Chato jimbo 1).

IDADI YA WATU
 
Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 1967 mkoa ulikuwa na watu 658,712, mwaka 1978 watu 1,009,379, mwaka 1988 mkoa ulikuwa na watu 1,326,183 na mwaka 2002 watu 2,033,888. Ongezeko la idadi ya watu lilikuwa kwa wastani wa asilimia 2.7. Aidha, mwaka 2011 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002 mkoa unakadiriwa kuwa na idadi ya watu 2,746,058.

 
Halmashauri Ya Wilaya
Idadi ya Watu

1978
1988
2002
MAOTEO 2011
Missenyi
-
-
-
174,889
 
Bukoba (V)
296,462
343,950
395,130
467,129

Bukoba (M)
36,914
47,009
81,221
153,016

Muleba
217,493
274,447
386,328
492,404

Chato
-
-
-
383,162
 
Biharamulo
165,580
209,524
410,794
252,218

Karagwe
185,013
292,589
425,476
542,517

Ngara
107,917
158,658
334,939
422,044

JUMLA
1,000,379
1,326,183
2,033,888
2,746,058
 
Chanzo: Ofisi Kuu ya Takwimu Taifa (NBS) , 2011
 
HISTORIA YA MKOA WA KAGERA
Mkoa huu haukuitwa Kagera bali ulikuwa moja ya maeneo yaliounda jimbo lililoitwa Lake Province. Jimbo hili lilijumuisha Wilaya ya Bukoba, Musoma, Shinyanga na Tabora. Baadaye ulibadilishwa jina na kuitwa ‘West Lake Region' (Ziwa Magharibi) na kujumuisha Wilaya 4 za Ngara, Biharamuro, Karagwe na Bukoba.
Kabla na baada ya kuja kwa wakoloni mkoa wa Kagera ulikuwa na utawala wa Kimila (Chiefdoms) uliogawanyika katika himaya 8. Himaya hizo ni pamoja na Kyamutwara, Kihanja (Kanazi), Kiziba, Ihangiro, Bugabo, Karagwe, Biharamulo (Rusubi) na Maruku (Bukara).
Baadhi ya Watemi waliotawala himaya hizo ni pamoja na Emmanuel Rukamba (Kyamtwara), Rumanyika (Karagwe), Kasusura (Biharamulo), Lugomola (Bukara), Rutinwa (Kiziba), Kayoza (Bugabo), Kahigi (Kihanja) na Nyarubamba (Ihangiro). Kila mtemi alikuwa na walinzi wake walioitwa Warugaruga.
Wakazi wa asili ya Kagera ni wabantu na wengi wao wana asili ya Bunyoro. Wanaongea lugha sawa na ile ya Wanyoro, Wanyankole, Watoro na Wakiga. Busubi na Bugufi wana lugha na desturi sawa na Watusi, Wahutu na Waha. Lakini makabila hayo ni ya Wabantu wa Ziwa (Interlacustrine Bantu) na yanafanana mila na desturi. Makundi hayo yaligawanyika kati ya wachungaji (Bahima) ambao walitawala na wakulima (Bairu) ambao walitawaliwa na mara nyingi kudharauliwa. Bahima (Balangira) walikuwa na koo chache zipatazo 20 na walitawaliwa na Wahinda, Wabito na Wankango.
Bairu walikuwa na Koo kama 130 zenye mashina 24 ambayo kiasili walikuwa Bairu lakini kwa kuoa katika Bahima au kufanya kazi kwa Watemi walipandishwa hadhi na kuwa Bahima (Batware). Kila ukoo uliitwa jina la Baba mwanzilishi wake na kina ukoo ulikuwa na kitu walichokatazwa kula (Omuziro) na mnyama walioshirikishwa nae (Ekyerumono).
Mkoa ulibadilishwa jina na kuitwa Kagera mwaka 1979 baada ya vita ya Tanzania na Uganda. Chini ya uongozi wa Mkuu wa Mkoa aliyekuwepo wakati huo Capt. Peter Kafanabo jina la Kagera lilipendekezwa kwa sababu ya mto Kagera unaogusa sehemu kubwa ya Wilaya zote zinazounda Mkoa wa Kagera.
Uchumi wa wenyeji wa Kagera ulijikita katika mashamba ya migomba. Chakula chao kikuu ni ndizi katika aina zake mbalimbali. Katika mashamba yao hulima mazao mengine kufuatana na msimu. Mazao hayo ni pamoja na maharage, mihogo, mahindi na mboga. Baada ya kuja kwa wazungu waliongeza ulimaji wa kahawa kama zao la biashara lililowasaidia kujiongea kipato.

 





 
 

 

 
 
 
 
 

 
 
 
 
 
MAJIMBO YA UCHAGUZI
Mkoa unayo majimbo ya Uchaguzi 10 na wapo Wabunge 9 wa kuchaguliwa na Wabunge 3 wa viti maalum. Jumla ya Wabunge 11 wanatoka chama cha Mapinduzi (CCM) na Mbunge 1 anatoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo. Majina ya waheshimiwa wabunge na majimbo wanayowakilisha pamoja na wale wa viti maalumu ni kama ifuatavyo:-

 
Na
Jina La Mbunge
Jimbo
Chama
Wilaya
1.
Mhe. Hamis Sued Kagasheki
Bukoba Mjini
CCM
Bukoba
2.
Mhe. Jason Samson Rweikiza
Bukoba Vijijini
CCM
Bukoba
3.
Mhe. John Pombe Magufuli
Chato
CCM
Chato
4.
Mh. Dk Antony Mbasa  
B'mulo Magharibi
CHADEMA Biharamulo
5.
Mhe. Begumisa Gosbert Blandes
Karagwe
CCM
Karagwe
6.
Mhe. Eustace Katagira
Kyerwa
CCM
Karagwe
7.
Mhe. Anna Tibaijuka
Muleba Kusini
CCM
Muleba
8.
Mhe. Charles Mwijage
Muleba Kaskazini
CCM
Muleba
9.
Mhe.Asumpta Nshunju Mushama
Nkenge
CCM
Missenyi
10.
Mhe. Deogratius Ntukamazina
Ngara
CCM
Ngara
11.
Mhe. Bernadetha Mushashu
Viti Maalumu
CCM

12.
Mhe. Elizabeth Batenga
Viti Maalum
CCM

13.
Mhe. Conjester Rwamulaza
Viti Maalum
CHADEMA

 
Vyama vya siasa vinavyoendesha shuguli zake vizuri hapa mkoani ni pamoja na CCM, TLP, NCCR - Mageuzi, CUF, UMD, UDP, na CHADEMA. Hatuna matukio ya kukiukwa kwa sheria na utaratibu kwa vyama vya siasa.

HALI YA UCHUMI NA MAENDELEO YA MKOA
Uchumi wa mkoa unategemea zaidi kilimo ambapo zaidi ya asilimia 70 ya watu wanajishughulisha na kilimo cha mazao ya chakula na biashara. Shughuli za uvuvi, mifugo,viwanda na madini zinachangia pia katika uchumi wa mkoa.
Kwa kuzingatia malengo ya Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (MKUKUTA) , Dira ya Taifa ya mwaka 2025 na malengo ya Milenia, Mkoa wa Kagera unaendelea kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo na umepiga hatua katika sekta za uchumi, miundo mbinu na huduma za jamii. Hata hivyo pamoja na hatua hizi zilizopigwa, juhudi za wananchi mkoani za kujiletea maendeleo zinakumbana na matatizo na vikwazo mbalimbali ambavyo vimeendelea kupatiwa ufumbuzi kwenye mipango ya maendeleo ya Mkoa.

KANDA ZA IKOLOJIA (ECOLOGICAL ZONES) :
Mkoa wa Kagera umetenganishwa katika Kanda tano za kilimo kuzingatia mwinuko wa maeneo hayo kutoka usawa wa bahari na kiwango cha unyeshaji wa mvua.
 
Ukanda wa kwanza : Ukanda huu unajumuisha maeneo ya mashariki ya wilaya ya Bukoba na Muleba yanayoambaa kandokando ya ziwa victoria na uko katika mwinuko wa mita 1,300 mpaka 1,500 kutoka usawa wa bahari. Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800 - 1,750 kwa mwaka. Shughuli kuu za kiuchumi katika eneo hili ni kilimo cha ndizi, maharagwe, mahindi na kahawa. Eneo la ukanda huu ni asilimia 17 ya eneo la Mkoa.
 
 
 
Ukanda wa pili : Huu ni ukanda wa juu ulioko kwenye mwinuko wa mita 1,400 mpaka 1,800 kutoka usawa wa bahari. Ukanda huu unajumuisha maeneo ya juu ya wilaya ya Karagwe na Ngara na mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800-1,000 kwa mwaka. Mazao yanayolimwa kwenye ukanda huu ni ndizi, maharagwe, mahindi na kahawa. Eneo la ukanda huu ni asilimia 19 ya eneo la mkoa.
 
 
Ukanda wa Tatu : Ukanda huu uko katika mwinuko wa mita 1,000 kutoka usawa wa bahari na unajumuisha wilaya ya Ngara ,Biharamulo na Chato.Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 750-800 kwa mwaka. Shughuli kuu za kiuchumi ni uzalishaji wa mazao ya mahindi, mihogo, mpunga, mtama, karanga na pamba. Eneo la ukanda huu ni asilimia 27 ya eneo la mkoa.
Ukanda wa Nne : Ukanda huu upo kwenye mwinuko wa mita 1,000 kutoa usawa wa bahari na unajumuisha maeneo ya mashariki ya wilaya ya Karagwe,wilaya ya Misenyi na maeneo ya magharibi ya wilaya ya Bukoba. Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800-1,000 kwa mwaka. Shughuli kuu za kiuchumi ni kilimo cha mazao ya mahindi,maharagwe na ufugaji. Eneo la ukanda huu ni asilimia 10 ya eneo la mkoa.
 Ukanda wa Tano :Ukanda huu unajumuisha maeneo ya kaskazini ya wilaya ya Karagwe na Misenyi na uko kwenye mwinuko wa mita 1,000 kutoka usawa wa bahari .Ukanda huu unapata mvua za wastani wa milimita 750-800 kwa mwaka.Sehemu kubwa ya ukanda huu ni misitu ya hifadhi na mapori ya akiba. Eneo la ukanda huu ni asilimia 27 ya eneo la mkoa.

 


 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

HII SIYO BREAKING NEEEWWWWSSSSS.... hata usiposoma powa tu...MTOTO UMLEAVYO Yaani imekuwa kawaida wamama wengine huwa wanafurahia watoto wao wadogo kutamka matusi machafu, eti ni ujanja, pambafu zenu....

HII SIYO BREAKING NEEEWWWWSSSSS.... hata usiposoma powa tu...MTOTO UMLEAVYO

Yaani imekuwa kawaida wamama wengine huwa wanafurahia watoto wao wadogo kutamka matusi machafu, eti ni ujanja, pambafu zenu....

NYUMBA ZA KIFAHARI ZA VIGOGO SASA HATARINI KUBOMOLEWA...!!

MAGHOROFA yaliyojengwa kandokando ya Mto Mlalakua na Ufukweni mwa Bahari ya Hindi yatabomolewa, hivyo kuzua mshtuko mkubwa kwa wamiliki.

Uchunguzi  uliofanywa na gazeti hili kwa zaidi ya wiki nne umebaini kwamba kazi ya kubomoa nyumba hizo inaweza kuanza wakati wowote ingawa kuna changamoto kubwa kwani baadhi ya nyumba hizo ni za vigogo wenye madaraka makubwa serikalini au ndani ya vyama vya siasa.
Habari zaidi zinadai kwamba baadhi ya vigogo hao wamekimbilia mahakamani kufungua  kesi ya kupinga nyumba zao zisiguswe wakati wengine wamekua wakitoa vitisho kwa waliopewa mamlaka ya kuzibomoa.

Vyanzo vyetu vya habari vinadai kwamba baadhi ya nyumba hizo zina hati zilizopatikana serikalini wakati zingine wamiliki wao walivamia maeneo hayo na kuporomosha maghorofa makubwa.
Kutokana na ujenzi huo holela, wakazi wa Kawe kwa Malecela waliamua kumwandikia barua Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,  Profesa Anna Tibaijuka wakitoa malalamiko juu ya ujenzi huo.


 Barua hiyo ambayo gazeti hili lina nakala yake iliyoandikwa Februari 20, mwaka huu ilieleza kwamba ujenzi wa nyumba hizo umekuwa ni kero kubwa kwani zimejengwa katika mkondo wa maji hivyo mvua inaponyesha inasababisha mafuriko kwa wananchi wengine.

Wananchi hao wamemueleza waziri kwamba nyumba hizo zimeziba mkondo wa maji katika baadhi ya mito inayoingia baharini, hivyo kusababisha maji kuhama na kuelekea kwenye nyumba zao na daraja la eneo la Malecela kusombwa na maji hivyo kusababisha magari kutopita.
Walidai kuwa nyumba nyingi zimejengwa katikati ya mto na wengine wamejaza vifusi kando ya mto unaopita karibu na nyumba zao, hivyo kusababisha mkondo wa maji kwenda kwa wananchi.

“Hivi sasa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wanashindwa  kutembelea ufukwe wa bahari kutokana na baadhi ya nyumba kuziba njia na mbaya zaidi waliojenga kando ya mkondo wameharibu mikoko,” imesema sehemu ya barua hiyo.
Waliendelea  kusema kwamba vigogo hao  ambao ni wavamizi baadhi yao wamekuwa wakitembea na bastola hadharani na   kuwatishia maisha wale wanaodiriki kuzungumzia ujenzi wanaoufanya katika maeneo hayo.

Wananchi hao wametishia kuwa endapo hawatasikilizwa wataenda Ikulu kumuona Rais Jakaya Kikwete.
Kaimu Mkurugenzi wa Baraza la Hifadhi ya Mazingira nchini (NEMC),  Ignas Mchallo alisema:
“Wote waliojenga katika maeneo hayo  watahamishwa kwa kufuata sheria kwani kuna wengine waliojenga kabla ya sheria ya mazingira ambayo inataka kuwepo kwa nafasi ya mita 60 toka mtoni au ufukweli,” alisema Mchallo.


Naye  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka alisema  kwamba nyumba 73 zilizojengwa kwenye fukwe za Bahari ya Hindi, zitavunjwa na akazitaja kuwa ziko kwenye fukwe za Kawe, Mbezi na Msasani na kwamba ingawa zilijengwa kihalali baada ya kupewa hati, lakini sheria mpya hairuhusu nyumba hizo kuwepo.


"KUNA MAJAMBAZI WAMETUMWA NA VIGOGO WAJE KUNIUA".......MAMA ZITTO...!!

SHIDA Salum ambaye ni mama mzazi wa mwanasiasa machachari ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe amesema kuna watu wanataka kumuua.


Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu Jumamosi iliyopita, Shida alisema Aprili 19, mwaka huu, saa moja na nusu katika Ghorofa la NSSF maeneo ya Tabata Bima, hawezi kuisahau kwa kuwa ndiyo siku ambayo majambazi walimvamia wakiwa na bastola.
Akisimulia mkasa huo Shida alikuwa na haya ya kusema:
“Majambazi hayo yaliyonivamia siyajui lakini mmoja wao huwa namuona. Kabla hawajaja walinipigia simu wakaniambia wana shida na mimi lakini
hatukupanga namna ya kuonana.
Uwazi: Sasa walipofika nyumbani kwako, uliwakaribishaje?
Shida: Walipofika walivamia na kufanikiwa kuingia sebuleni.
Uwazi: Baada ya kuingia ikawaje?
Shida: Cha kwanza walichotaka ni laptop (Kompyuta mpakato), flash na simu zangu.
Uwazi: Uliwapa?
Shida: Baada ya kutoa amri hiyo niliwajibu kuwa kompyuta iko ofisini na simu niliwaambia ziko kwenye chaji.
Uwazi: Baada ya hapo ikawaje?
Shida: Mmoja wa majambazi hayo alinionyesha bastola kuwa kama sijatii hayo wanayoniambia basi watanifanya kitu kibaya,   ndipo nikamuita kijana wangu aitwaye Mtana aende chumbani kuchukua simu zangu niwape.
Uwazi: Ikawaje?
Shida: Niligundua kuwa Mtana alikuwa anasikia amri zilizokuwa zikitolewa na majambazi hayo, hivyo alipiga kelele kuomba msaada kwa wananchi.
Uwazi: Majambazi wakafanya nini?
Shida: Waliposikia kelele walikimbilia nje, wakaingia ndani ya gari lao ambalo namba zake zisijui, wakatoweka.
Uwazi: Pole sana.
Shida: Pamoja na purukushani hizo namshukuru Mungu sana kwa kuwa hawakunidhuru na hawakufanikiwa kuchukua chochote.
Uwazi lilitinga nyumbani kwa mama huyo na kukuta ulinzi ukiwa umeimarishwa ambapo sasa kuna askari wenye bunduki.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, majambazi hayo yalifanikiwa kuingia ndani baada ya mlinzi aliyekuwepo zamu kwenda kubadili nguo za kiraia ili avae za kiaskari.
“Tukio lilikuwa la haraka sana, wakati askari huyo anatoka kwenye kibanda cha kubadilishia nguo ndipo na wale majambazi walipokuwa wakitoka ndani na kuingia kwenye gari lao,” kilisema chanzo.
Waandishi wetu walimtafuta kiongozi wa walinzi wanaolinda nyumbani kwa mama huyo, aliyejitambulisha kwa jina moja la Ngosha na alipoulizwa kuhusu sakata la kuvamiwa alikiri kulifahamu.
“Baada ya tukio lile tumeimarisha ulinzi ili kuhakikisha usalama wa watu na mali zao. Sasa tumeweka askari wenye bunduki na tunaamini tukio kama hilo halitajirudia,” alisema Ngosha.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, ACP Marietha Minagi alikiri kutokea kwa tukio hilo.
“Nina taarifa ya tukio hilo na tunaendelea na upelelezi kuwasaka majambazi hao, wananchi waondoe hofu.” alisema Kamanda Minagi.

"ATAKAYEKUBALI KUIVUNJA CHADEMA ATALAANIWA HAPA DUNIANI MPAKA MBINGUNI ".....ZITTO KABWE...!!


WAKATI Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, akisema kuwa chama chake sasa hakitawapokea na kuwapa nafasi za uongozi wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaofukuzwa, mkakati wa kukivuruga chama chake umebainika, MTANZANIA Jumapili linaripoti.
Mbowe, wakati akitoa kauli hiyo jana mkoani Tabora, taarifa zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa mkakati unaodaiwa kuandaliwa na chama dola kukidhoofisha Chadema unaendelea kuratibiwa kwa karibu na ‘virusi’ (mashushu) waliopenyezwa ndani ya chama hicho na huenda yakaibuliwa mambo mengi zaidi yanayodaiwa kufanywa na chama hicho.

Aidha matukio yanayotokea bungeni, nguvu za dola kutumika kupita kiasi, uwepo wa ‘virusi’ ndani ya chama hicho ni miongoni mwa mambo yanayotajwa na baadhi ya maofisa wa ngazi za juu wa vyombo vya ulinzi na usalama kwamba chama hicho kinaandaliwa anguko.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa mkakati wa kukidhoofisha Chadema ulianza tangu siku nyingi na unaratibiwa kwa ukaribu na ‘virusi’ wanaodaiwa kupenyezwa ndani ya chama hicho, ambacho katika siku za hivi karibuni kimepata uungwaji mkono mkubwa.

Inaelezwa kuwa kumekuwa na juhudi kubwa zinazofanywa na mahasimu wa Chadema kutaka kukidhoofisha chama hicho kupitia harakati zake za kisiasa, ambazo imekuwa ikizifanya kwenye mwanga na gizani.

ANGALIA VIDEO HAPO CHINI....

Kwamba matukio ya sasa yanayotokea bungeni, wanachama wake kuundiwa kesi na hata kukamatwa kwa Mbunge wake wa Arusha Mjini, Godbless Lema, ni matokeo ya mkakati huo.

Inadaiwa kuwa mahasimu wa Chadema wamekuwa wakifanya juu chini kuhakikisha wanakibana chama hicho kuanzia bungeni, ambako imeonekana wazi kuwa umaarufu wa chama hicho kwa kiasi kikubwa umechangiwa na wabunge wake kuibana vilivyo serikali pindi wanapowasilisha hoja mbalimbali ndani ya vikao vya Bunge.

Tayari hali kama hiyo imeshuhudiwa Bungeni hivi karibuni, baada ya wabunge wake watano kusimamishwa kwa kukaidi kiti cha spika, wakati kiti hicho kikishindwa kuwachukulia hatua wabunge wa CCM wanaokwenda kinyume na kanuni zake.

Inaelezwa kuwa hatua hiyo ni mkakati wa kukifanya Chadema kishindwe kutekeleza majukumu yake sawa sawa.

Kuibuka kwa matukio ya wana Chadema wawili, mmoja akidaiwa kumrekodi mwingine wakidaiwa kupanga mikakati ya kutisha, nako kunaelezwa wazi kwamba chama hicho hakipo salama kama kinavyofikiri.

Hata hivyo, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Azaveli Lwaitama, kwa upande wake anasema mizengwe inayofanywa dhidi ya Chadema si ya kukidhoofisha kama wanavyofikiri, bali ni kukipandisha juu chama hicho.

Akitolea mfano tukio la kukamatwa kwa Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema) Godbless Lema kwa tuhuma za kuchochea vurugu katika Chuo cha Uhasibu, Dk. Lwaitama alihoji mamlaka ya Mkuu wa Mkoa kumkamata mbunge aliyechaguliwa kwa kura za wananchi, akidai kuwa ni ya kipuuzi.

“Wenzetu wa Kenya wameshaondoka katika mfumo huu wa kipuuzi, eti mkuu wa mkoa ambaye hakuchaguliwa na wananchi anajipa mamlaka ya kumkamata mbunge aliyewekwa madarakani na wananchi..huu mimi nasema ni upuuzi,” alisema Dk Lwaitama.

Wakati hayo yakitokea, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, amesema chama chake hakitawapokea na kuwapa nafasi za uongozi wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaofukuzwa.

Amesema utaratibu wa awali wa kuwapokea na kuwapa nafasi za uongozi wanaCCM wanaofukuzwa au kujiondoa wenyewe kwenye chama hicho na kukimbilia Chadema, sasa umesitishwa.

Mbowe aliyasema hayo jana, katika mkutano wa ndani wa chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa Chuo cha Ualimu, Tabora na kuhudhuriwa na makada wake wa Kanda ya Magharibi, inayojumuisha mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora.

Katika hotuba yake hiyo, alisema dhamira ya Chadema kwa sasa ni kukiimarisha na kukipatia viongozi walioandaliwa tofauti na vyama vingine vya kisiasa nchini.

Alitoa mfano wa viongozi wa CCM aliodai kuwa idadi kubwa ya viongozi wake wanapatikana kutokana na uwezo wao wa fedha badala ya ule wa kiuongozi.

Alisema Chadema inajipanga kuhakikisha viongozi wake kuanzia ngazi za chini wanawajibika na kuwatumikia wananchi na kuonya kuwa yeyote atakayebainika kutowajibika katika kutekeleza majukumu yake, chama hakitasita kumchukulia hatua kwa mujibu wa Katiba.

Akizungumzia lengo la kuanzishwa kwa Kanda za majimbo za chama hicho, alisema ni kuzidi kukijengea uwezo na kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi, jambo ambalo limekuwa gumu kwa serikali ya CCM.

Aidha, Mbowe aliwaonya wabunge wa chama hicho kwa kueleza kuwa kuanzia sasa watapimwa kwa uwezo wao wa uongozi kutokana na utaratibu mpya wa kanda na namna wanavyotekeleza majukumu yao kwa kusaidiana kati ya mbunge na mbunge, ambao watakuwa katika kanda moja, licha ya kutofautiana majimbo.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe, ambaye aliambatana na Mbowe katika mkutano huo, alisema viongozi wa Chadema Kanda ya Magharibi wanapaswa kuwa tayari kujitolea kwa ajili ya chama chao.

Zitto alisema Chadema kinapita katika kipindi kigumu, hivyo viongozi wake wanapaswa kukiimarisha katika ngazi ya kanda ili kuwaenzi wote waliokipigania kwa muda wa miaka 22 ya uhai wake.

“Ndugu zangu wana kanda ya magharibi, viongozi wa Chadema na wanachama, katu msije kukubali mtu yeyote awagawe kwa misingi na malengo yake binafsi, kwani chama chetu sasa kina maadui wengi wasiokitakia mema,” alisema Zitto.

Aliwataka viongozi wenzake kuwa makini na watu ambao kila wakilala wanawaza kuiangamiza Chadema au kuipoteza kabisa katika siasa kwa kuwagonganisha viongozi wake.

CREDIT :GUMZO LA JIJI

Monday, April 29, 2013

"LAZILY TUZIKAGUE KUCHA ZA LEMA..... TUPO TAYARI KUFA....."HAYA NI BAADHI YA MABANGO YA WAANDAMANAJI HUKO ARUSHA


Asubuhi ya leo, kama ilivyotarajiwa na wengi baada kufuatia taarifa mbalimbali katika vyombo vya habari, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alifikishwa mahakamani baada ya kukaa rumande tangu alipokamatwa usiku wa kumkia siku ya Jumamosi, Aprili 27, 2013.

Mbele ya hakimu Joyce Msofe na mawakili Kimomogoro na Humphrey Mtui wanaomtetea, Lema amesomewa shitaka la kosa la uchochezi linalomkabili kwamba aliwachochea wanafunzi wa chuo cha uhasibu Arusha kumzomea Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa kuwaambia wanafunzi kuwa Mkuu huyo wa Mkoa, “hajui chuo cha uhasibu kilipo, amekuja akiwa amechelewa na anaingia hapa kama anaingia kwenye send off.”
 
Mtuhumiwa Lema amekana kosa hilo.Mwendesha mashitaka alisema dhamana ipo wazi kwa mtuhumiwa endapo atatimiza masharti ya dhamana.

Mtuhumiwa alifanikiwa kutimiza masharti ya dhamana ambayo ni kuwepo kwa mtu mmoja mwenye kitambulisho kinachokubalika kisheria na kuweka rehani kiasi cha shilingi milioni moja.

Baada ya kutoka mahakamani hapo, Lema alielekea kwenye maeneo ya Ofisi za chama, CHADEMA. kwa maandamano  makubwa

Picture

Picture

Picture
Picture

BUSU SI UGOMVI......MAMBO YA KUIGA YATATUMALIZA





MAANDAMANO MAKUBWA YANAENDELEA JIJINI ARUSHA BAADA YA GODBLESS LEMA KUACHIWA HURU


Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema ameachiwa kwa dhamana hivi punde baada ya kushtakiwa kwa makosa ya uchochezi katika mahakama ya Mkoa wa Arusha huku maandamano yakifanyika hivi sasa katika mitaa ya Jiji la Arusha, Tanzania.

Katika Mahakama hiyo kulikuwa na umati mkubwa wa wafuasi na wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Mashabiki, wafuasi na wanachama wa chama hicho walifurika katika mahakama hiyo kwa ajili ya kumuunga mkono mbunge huo.habarimasai.com itaendelea kukuletea Taarifa zaidi baadaye.
 
Hivi sasa mashabiki, wafurukutwa na wanachama wa Chadema wanafanya maandamano makubwa kuelekea katika ofisi za chama hicho ambazo zipo katika eneo la Ngarenaro.

Hivi sasa wanapita katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mulongo kwa maandamano huku wakipiga kelele za kuzomea.

Kesi ya uchochezi dhidi ya Lema imefunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mkoa wa Arusha na endeshwa na Hakimu Devota Msoffe.

Mwandishi wetu anasema kwamba kesi hiyo imeahirishwa mpaka Mei 29 mwaka huu. 

Katika hati ya mashtaka ambayo ipo katika mahakama hiyo inasema kwamba kosa la Lema ni ' kutoa maneno yanayodaiwa kuwa ni uchochezi. 

Endelea kuwa nasi  kwa taarifa mbalimbali moto moto.
credit the choice

ASKARI MWANAUME ABAKWA NA WANAWAKE WANNE BAADA YA KUTEKWA


Askari mmoja mwanaume anadaiwa kutekwa kisha kudhalilishwa kijinsia na wanawake wanne kwa karibu wiki moja kabla ya kupigwa mawe na kutupwa katikati ya milima.

Mateso ya muathirika huyo mwenye miaka 25 yalianza pale alipopata lifti ya gari kuelekea mji wa Mutare nchini Zimbabwe.
Wanawake wawili na mwanaume mmoja walikuwa kwenye gari, Mercedes Benz, na, baada ya kuendesha kwa takribani saa moja kuelekea mji huo, dereva wa gari hilo akabadili mwelekeo wa safari hiyo.
Ndipo muathirika huyo akalalamika, alitishiwa kwa kisu.
Msemaji wa polisi wa Manicaland, Inspekta Msaidizi Nuzondiwa Clean, alieleza: "Baada ya kubadilishwa mwelekeo huo, mlalamikaji alihoji wapi walikokuwa wakielekea na walimweleza walikuwa wakienda kupata chakula.
 
"Askari huyo alitaka kushushwa, lakini dereva huyo akatoa kisu na kumtishia nacho. Mmoja wa abiria wanawake akamfunga kwa kitambaa cheusi machoni mtuhumiwa huyo."
 Kwa mujibu wa Nuzondiwa,watesi  hao  walimpeleka mlalamikaji kwenye nyumba isiyojulikana ambako walimvua nguo zote na kumpora simu yake na Dola za marekani 35.
 Watuhumiwa walimwamuru mtu huyo kulala na mmoja wa wanawake hao katika matukio kadhaa na alishikiliwa kati ya Aprili 19-23.
 
 Kisha akafungwa tena kitambaa machoni na kushushwa kwenye Milima ya Dangamvura ambako, kwa mujibu wa polisi, alipigwa mawe katika mguu wake wa kushoto, na kumsababishia majeraha makubwa.
 Watuhumiwa hao kisha wakawasha gari lao na kutokomea kusikojulikana.Askari huyo alitoa taarifa Kituo cha Polisi cha Sakubva

"UREMBO SIYO KIPAJI NA SI KILA MWANAMKE MZURI ANAWEZA KUIGIZA"...JACKLINE WOLPER


Muigizaji Jacqueline “Jackie” Wolper amewashangaa wanaodhani kuwa urembo wa mwanamke ni mbadala wa kipaji hasa katika sanaa ya maigizo. 




Alisema urembo ni moja ya sifa ya mwanamke lakini kamwe hauwezi kumfanya asiye na kipaji kuwa nacho.
 

“Ukiwa mrembo ni bora zaidi,kwa kuwa itamfanya avutie kwenye movie,lakini pamoja na hayo ni lazima awe na uwezo wa kuigiza kulingana na kipande husika”alisema Wolper.
 

Wolper aliendelea kulalama kuwa kila mtu akijona ana sura ya kuvutia na umbo zuri basi anajua anaweza kuigiza ndio maana matokeo yake wanafanya vitu sivyo na mwisho wake wanaacha fani kabisa.
 

Alifafanuwa kuwa kuigiza ni zaidi ya urembo hivyo yeyote ambaye anafikiri anaweza kufanya kazi hii kwa uzuri wa sura na umbo ajaribu kama hakuchemka.

Source: Mwananchi

MSANII SIZE NANE ANAILILIA BIKRA YAKE HADHARANI

Mwanamuziki  aliyeitikisa vilivyo Kenya kabla ya kuokoka na kuachana na muziki wa kidunia, mwanadada Size 8 sasa ameanza kufunguka katika interview kwenye vituo mbali mbali vya redio na Tv kuhusiana na maisha mapya ya kidini.

Kati ya  mambo yote ambayo Size 8 amekuwa akiyaongelea, ni moja tu ambalo amekuwa akilitilia mkazo kwa kumaanisha kuwa linamsikitisha zaidi .....Jambo hilo ni lile la kupoteza BIKRA YAKE.....
Size 8 ameziambia media kuwa  "Najutia sana kupoteza bikra yangu. Ninaamini kuwa kijana anatakiwa kujilinda na kujizuia kufanya ngono katika ujana wake wote mpaka atakapo pata kibali toka kwa Mungu."

MUME WANGU HANA PUMZI KITANDANI....KWAKE DAKIKA TATU NI NYINGI SANA....NAOMBENI USHAURI

Mimi ni mdada wa miaka 27 na nina watoto wawili kwa sasa nimeolewa na mkaka mwenye miaka 32.

Kwa kweli mume wangu ni kijana handsome. Katika maisha yangu ya usichana mpaka kuolewa nimekuwa na mahusiano na wanaume takribani 4 kabla ya mume wangu.

Wanaume hao wote kwakweli walikuwa nao wazuri  na kati yao wawili walikuwa waume za watu na walikuwa na maumbile yakunitosha.... 


Pamoja na maumbile  yao,sikuwahi kufika kileleni japokuwa walikuwa wanapumzi ndefu yaani walikuwa wanaweza kuplay for about  1 hour . Tena kama tutalala pamoja usiku huo walikuwa wanaweza hata 4-5.

Nilipompata mume wangu nilimpenda toka rohoni na baada ya mhusiano ya miaka miwili tulioana,tatizo ambalo lipo kwenye ndoa yangu na nililiona toka mwanzo ni kwamba mume wangu hana pumzi kitandani japokuwa ndio mwanaume pekee anayenifikisha kileleni .

Yaani mume wangu yeye ni 3 minutes tu amemaliza  na baada ya muda anakoroma, hatuwezi kufanya hata mara  mbili kwa usiku hata nikimchezea anashindwa kusimama labda afanye kimoja asubuhi kingine usiku.

Na ili nikojoe kuna staili lazima niziapply mimi mwenyewe niwe najigusa kwake maana yeye tukifanya anashindwa kujizuia mara moja anakojoa.

Nisaidieni wapendwa nifanyaje maana  bado  nampenda  mume  wangu."
---------------


Jibu la Dyna: 

Shukurani sana kwa ushirikiano, hongera kwa kufanikiwa kufika kileleni kwani sio wanawake wote hufika hapo. Sidhani kuwa ni kweli kuwa mumeo anakojoa ndani ya dakika 3 na wakati huohuo wewe unafika kileleni.

Unapokuwa kwenye uhusiano wa kudumu au ndoa hupaswi kabisa-kabisa kurudisha mawazo yako nyuma na kuanza kufananisha utendaji wa wanaume uliokuwa nao na mpenzi wako wa sasa/mumeo. Jifunze kukubali jinsi mumeo alivyo na ridhika na uwezo wake aliojaaliwa na Mungu.

Ndio maana kabla ya uchumba kutangazwa kule kwetu huwa kuna swali unaulizwa na mama au bibi au shangazi


- "je una uhakika kuwa unataka kuolewa na huyu bwana? 

-je uko radhi kuishi nae hata kama siku moja utagundua kasoro zake? (kasoro hapa wanamaanisha kushindwa kufanya tendo). 

Hivyo basi unapofunga ndao na mtu na kugundua kuwa uwezo wake kitandani umebadilika ghafla kutokana na umri au mataizo mengine ya kiafya, unatakiwa kukubali tatizo na kumpa ushirikiano ili kuepusha matatizo.

Kilele na mwanamke:
Mwanamke anafika kileleni kuanzia Dk 10 mpaka dk 45 tangu tendo lianze na pengine inaweza kuchukua muda mrefu zaidi, hivyo basi kama unafanikiwa kufika kileleni ni wazi kuwa mumeo anauwezo wa kwenda mwendo wa angalau Dk15-20 sio dakika  3  kama  ulivyosema!

Napenda utambue kuwa uwezo wa tendo kwa wanawaume unatofautiana kama ilivyo kwa baadhi ya wanawake, suala muhimu ni upendo mlionao (mnapendana) na yeye anauuwezo wa kulifanya tendo mpaka wote mnafikia mshindo nakuridhika.

Mawasiliano wakati wa Tendo:
Suala lingine hapa ni kutojua namna ya kucheza na wewe au mwili wako, kama unapenda kuchezewa zaidi kabla ya tendo la ndoa ni wajibu wako kuliweka hilo wazi na kumuelekeza mumeo wapi pa kushika, usitegemee yeye afanye hivyo kwani hajui nini unachokitaka au kukipenda. Ili ufurahie tendo na lifanywe your way unatakiwa kuwasiliana na mumeo wakati tendo linaendelea....
 


Kama nilivyosema hapo awali sio wanaume wote wanauwezo wa kufanya  mapenzi unaofanana, hivyo basi kama yeye anamudu asubuhi na jioni au asubuhi mchana na jioni (weekends) then kubali utaratibu huo kuliko kulazimisha afanye ulivyozoea wewe mara tatu katika saa moja.....ni ngumu kwa baadhi ya wanaume hasa wenye umri wa miaka 35 na zaidi.

Ni matumaini yangu utafanyia kazi ushauri kutoka kwa wachangiaji wengine na kuongezea maelezo ya hapo juu  ili kuishi maisha mazuri na yenye amani kwa faida yako, mumeo na watoto wenu

MBUNGE LEMA AZUILIWA KUPIGA MSWAKI WALA KUNYWA CHAI......


TUKIO la kukamatwa na kuwekwa mahabusu kwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), kwa madai ya uchochezi, limeibua sura mpya baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutajwa kuwa nyuma ya mkakati huo,
 

Lema ambaye bado anaendelea kusota rumande siku ya tatu baada ya kunyimwa dhamana, ameanza kufanyiwa vituko na Jeshi la Polisi baada ya jana asubuhi mkewe kuzuiliwa asimpe mswaki wala chai.
 

Mbunge huyo alikamatwa kutokana na amri ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, aliyedai kuwa aliwachochea wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha kumzomea kiongozi huyo na kupopoa gari lake kwa mawe.
 

Hata hivyo, siku moja kabla ya kukamatwa Lema aliwaonesha waandishi wa habari ujumbe mfupi wa simu ya kiganjani aliyotumiwa na Mulongo akimtishia kuwa atamfungulia kesi yoyote anayoitaka.
 

“Umeruka kihunzi cha kwanza, nitakuonesha kuwa mimi ni serikali, ulikojificha nitakupata na nitakupa kesi ninayotaka mimi,’’ ulisomeka ujumbe huo uliotumwa kupitia simu namba 0752 960276 ambayo Lema alidai ni ya Mulungo.
 

Pia nguvu kubwa iliyotumika kumkamata mbunge huyo usiku saa 5:30 kwa kutumia askari na maofisa wa usalama kuzingira nyumba yake, imehojiwa na baadhi ya wananchi, wakitilia shaka kuwa kuna siri ndani yake.
 

Madai ya Mulongo kuwa Lema alichochea wanafunzi hao yanakinzana na ushahidi wa video unaoonesha kuwa mbunge huyo alitumia kila aina ya ushawishi kuwasihi wasiandamane baada ya mwenzao, Elly Kago (22), kuuawa na watu wasiojulikana jirani na chuo hicho.
 

Akizungumza na gazeti hili jana, mke wa Lema, Neema, alisema kuwa alifika kituo cha polisi asubuhi akipeleka chai, lakini akaelezwa kuwa haruhusiwi kumpelekea chai.
 

Alisema kuwa alipiga simu kwa mkuu wa upelelezi wa mkoa ndipo akaambiwa ampelekee na alipofika tena kituoni askari aliyekuwa zamu alianza kupekua mfuko wa Neema kwa fimbo, kisha akaamuru Lema apewe, ila anywe kwa dakika tatu.
 

Wakati anafungua chupa ya chai na kumimina kwenye kikombe, askari alimweleza kuwa imebaki dakika moja, hatua iliyomuudhi Lema akidai ni udhalilishaji, hivyo akashindwa kunywa.
 

Alipotaka kupewa mswaki, askari alikataa kuwa vifaa hivyo vinaweza kutumika kama silaha, hivyo haruhusiwi kupewa.
 

Tanzania Daima Jumapili lilizungumza na wanasheria kadhaa pamoja na wanasiasa wabobezi kuhusu sakata hilo, ambapo baadhi walidai huo ni mkakati wa CCM kutaka kuidhoofisha CHADEMA katika uchaguzi mdogo wa madiwani ujao kwenye kata nne.
 

“Kesho mnaweza kusikia Lema akifunguliwa kesi ya ajabu ya kutunga halafu kwa kipindi hiki kampeni zikianza mahakama itakuwa ikiisikiliza mfululizo ili asipate nafasi ya kushiriki kikamilifu.
 

“Huu mkakati si wa Mulongo peke yake bali ni mbinu za CCM zilizobakia katika kuhakikisha wanaikamata Arusha. Lakini naona kama wanazidi kujimaliza,” alisema mwanasiasa mmoja aliyeomba kuhifadhiwa jina lake.
 

Mwanasiasa huyo kutoka mkoani Arusha aligusia pia mkanganyiko wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) hivi karibuni kutangaza kata nne kurudia uchaguzi na kuiacha moja ya Sombetini ambayo diwani wa CCM alihamia CHADEMA.
 

“Ujue CCM wanafanya mambo bila kupima athari, Arusha ni mji wa kitalii lakini kwa sasa unaogopeka kwa fujo za polisi na wanasiasa, hata kesho utaona wakati Lema akipelekwa mahakamani.
 

“Hapa ni ngome ya CHADEMA hata kama Lema hayupo, sasa NEC wameibana Sombetini kwa hofu kuwa kata zote zikienda CHADEMA watakuwa na madiwani zaidi ya CCM, hivyo ishu ya meya kufufuka upya, ndiyo wakaamua kumtumia Mulongo kufanya mchezo huu wa hatari,” alisema.
 

Alipopigiwa simu jana jioni na kuulizwa juu ya madai hayo, Mulongo alizungumza kwa ukali akisema: “Wewe mhariri unaweza kunipigia simu kuniuliza swali kama hilo?”..
 

Aliendelea kufoka akisema: “Acheni kufanya kila kitu siasa, wewe ni polisi kujua Lema kwanini akamatwe hivyo, niache mimi niko na wageni wangu,” alisema na kukata simu.
 

Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Francis Stolla, alizungumzia suala la kukamatwa kwa Lema akisema kuwa nguvu kubwa na utaratibu uliotumika kumkamata haukuwa wa busara.
 

Stolla alisema: “Kwa mujibu wa kifungu cha 58 na 59 vya sheria ya ushahidi, Jeshi la Polisi au hata kama ni kwa amri ya mkuu wa mkoa ya kukamata walipaswa kuchagua njia nyingine ya busara.
 

“Jeshi linaweza kuwa na mamlaka mapana ya kukamata au hata kama ni kwa amri ya mahakama, busara huhitajika kutumika. Lema ni mbunge, anafahamika na upatikanaji wake hauna utata, anapotuhumiwa kuhitajika polisi busara inatumika kumwita au kumwandikia aende, si kumvizia kama walivyofanya,” alisema.
 

Mwanasheria mwingine ambaye aliomba kuhifadhiwa jina, alifafanua kuwa: “Rais peke yake ndiye Amiri Jeshi. Uamiri jeshi wa rais haugawanyiki mpaka kwa wakuu wa mikoa.
 

“Uamiri jeshi wa rais upo kikatiba, hauwezi kuwa wa wakuu wa mikoa au wa wilaya. Ndiyo maana anayeamrisha polisi katika mkoa ni Kamanda wa Polisi wa Mkoa, na wilayani anakuwapo ofisa anayeamrisha (OCD),” alisema.
 

Aliongeza kuwa sheria zinaruhusu mkuu wa mkoa na wilaya kutoa amri ya kukamata mtu kama hakuna askari lakini mtuhumiwa anapokamatwa sharti aambiwe anakamatwa kwa kosa lipi na anayemkamata ajitambulishe.
 

Alisema kuwa siku ya tukio chuoni, polisi walikuwapo wakati Lema akizungumza na wanafunzi na hawakuona kosa lolote kwake ndiyo maana hawakumkamata, sasa iweje mkuu wa mkoa aje na amri.
 

Akizungumzia nguvu iliyotumika katika kumkamata Lema, Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA (BAVICHA) Mkoa wa Tanga, Aaron Mashuve, aliliomba Jeshi la Polisi kuelekeza nguvu kama hizo katika kusaidia watu wenye ulemavu wa ngozi (albino).
 

Alisema nguvu hiyo kama ingetumika wauaji hao wangekuwa wamekamatwa badala ya polisi kupoteza muda kuhangaika na wanasiasa ambao wanaweza hata kuitwa kituoni wakaenda kwa hiari yao.
 

Katika hatua nyingine, CHADEMA mkoani Arusha kimetangaza kumfungulia mashtaka mkuu wa mkoa huo kwa tuhuma za kumtishia mbunge wao kwa ujumbe wa maandishi, pia kumtaka athibitishe madai ya kuwa kifo cha mwanafunzi kina uhusiano na masuala ya kisiasa.
 

Katibu wa mkoa wa chama hicho, Amani Golugwa, alisema taratibu za kuyashughulikia masuala hayo yote mawili zinaendelea chini ya jopo la wanasheria wa chama hicho.

Source:Tanzamia Daima