Friday, May 31, 2013

MZUMBE SECONDARY YAFUNGWA...WANAFUNZI WAPEWA SIKU MBILI WAPOTEE KATIKA MAZINGIRA YA SHULE


Wananfunzi wakidato cha kwanza hadi cha sita katika shule ya sekondari Mzumbe Morogoro wamelazimika kuandamana kwenda ofisi ya mkuu wa mkoa wa huo wakishinikiza kuboreshewa huduma muhimu.

Maboresha wanayodai kuboreshewa shuleni hapo ni pamoja na miundombinu, kuondoa ubadhirifu, uongozi mbovu na kukomeshwa vitendo vya lugha chafu zinazo tolewa na baadhi ya walimu.

Maandamano hayo yalizimwa mapema asubuhi baada ya jeshi la polisi kulazimika kufika katika eneo la
sangasanga barabara kuu ya Iringa Morogoro ambapo maandamano hayo yalikuwa yamefika kuelekea katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Morogoro.

Wananfunzi hawa wa shule ya sekondari Mzumbe Morogoro ya wenye vipaji maalum wanadai kuwa maandamano hayo yanatokea baada ya kuvumilia kwa muda mrefu na hivyo wameamua kupaza sauti zao wakibainisha matatizo lukuki yanayo wasibu ambayo yanaweza kushusha kiwango cha taaluma yao.

Mkuu wa shule ya sekondari Mzumbe Dismas Njawa ameelezea namna alivyoweza kutatua baadhi ya matatizo lakini hayakukidhi haja za wanafunzi hao.

Katibu tawala Mkoa wa Morogoro Elia Ntandu alilazimika kwenda kuzungumza na wanafunzi hao akiahidi kuyafanyia kazi yale yatakayo wezekana.



Wanafunzi hawakuelewa, na ndipo Serikali ilipoamua kuifunga shule ya Sekondari ya vipaji maalumu, Mzumbe kwa muda usiofahamika na kuwapa wanafunzi siku mbili, kuanzia leo, kuondoka shuleni hapo
---
Monica Lyampawe,
TBC Morogoro.

KIJANA ANUSURIKA KUFA BAADA YA VIBAKA KUMCHOMA MOTO HUKO MKOANI LINDI


Mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Ismai Mayoba(31) anayefanya kazi Bar ya Mangrove,Mkazi wa Manispaa ya Lindi amenusurika kifo baada ya kuvamiwa na kundi la Vijana waliotaka kumpora na hatimae kumchoma moto. 

Kwa sasa kijana huyo amelazwa katika Hospital ya Sokoine Mjini humo.

Kufuatia tukio hilo,Jeshi la Polisi wilayani Lindi limefanikiwa kumkamata mtu  mmoja kati ya watuhumiwa saba waliohusika na tukio hilo lilitokea katika eneo la Mtaa wa Congo.


Akithibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kukamatwa kwa mtuhumiwa,Afisa Mnadhimu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi,Renatha Mzinga alimtaja ndugu Ally Manially(22)mkazi wa mtaa wa Kongo kuwa anashikiliwa na Jeshi hilo na atafikishwa mahakamani leo kujibu shitaka la kujeruhi na kujipatia pesa kwa njia ya Udanganyifu ikiwa pamoja na kumchoma mwenzie Moto huku akijua ni kosa kisheria.

Aidha Mzinga alieleza kuwa Jeshi la polisi linaendelea kutafuta watuhumiwa wengine 6 waliohusika na tukio hilo

ZANZIBAR YAPIGA MARUFUKU NDOA ZA JINSIA MOJA.....UKINASWA IMEKULA KWAKO ( MIAKA 30 JELA )



Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imetunga sheria ya kupiga marufuku ndoa za watu wa jinsia moja.Waziri wa Katiba na Sheria wa Zanzibar, Bwana Abubakar Khamis Bakar, aliyasema hayo kwenye Kikao cha Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakati akijibu swali la Mwakilishi wa Jimbo la Wawi, Saleh Nassor Juma kutoka Chama cha Wananchi (CUF).

Katika swali lake, Bw. Saleh Nassor Juma alitaka kujua ni lini Serikali ya Zanzibar itatunga sheria ya kukataza ndoa hizo na kuweka adhabu kali kwa watu ambao watabainika kufanya vitendo hivyo vichafu. 


Waziri Abubakar amesema, ndoa za watu wa jinsia moja ni kinyume na utamaduni wa Zanzibar na kwamba sheria hiyo imeweka adhabu ya kifungo cha miaka saba kwa wale wote watakaopatikana na hatia hiyo.

Pia alisema kama ninavyomnukuu: "Sheria hii inahusu makosa mengi yakiwemo ya ubakaji, zinaa, usagaji na umalaya ambayo yote yana adhabu ya kifungo cha maisha au miaka isiyopungua 30 gerezani," mwisho wa kunukuu.

Monday, May 27, 2013

RIHANNA IMEKULA KWAKE..!!!!! ...KARRUECHE TRANS SASA AHAMIMIA NYUMBANI KWA CHRIS BROWN


 
Siku zote mwenye kiu iliyopitiliza akipewa maji ya kunywa hutamani atumie jagi zaidi ya kikombe anachowekewa maji, ndivyo ilivyomtokea mrembo Karrueche Tran aliyetoswa mwaka jana na Chris Brown aliyemchagua Rihanna dhidi yake wakati mrembo huyo akiwa na moyo uliojaa mapenzi na maumivu ya kulikosa penzi la ‘turn up the music singer’..
Sasa alipopewa nafasi tena ameamua kuitumia vyema na katika kupunguza zaidi umbali ameamua kuhamia kabisa nyumbani kwa mwimbaji huyo. 


Kwa mujibu wa TMZ Chris na Karrueche wamekua wakiishi pamoja nyumbani kwa muimbaji huyo Los Angeles tangu walipoonekana pamoja kwenye sherehe ya kuzaliwa Chris Brown alipotimiza miaka 24. 
Ripoti zinasema mrembo huyo amehamishia nguo zake na vitu vyake takribani vyote kutoka kwake na kuvipeleka nyumbani kwa Chris Brown lengo ni kuwa karibu zaidi na mwimbaji huyo. 

Rafiki wa karibu wa KT ameuambia mtandao wa Hollywoodlife kuwa karrueche anajaribu kuweka commitment katika mahusiano yake na Chris ambayo mwimbaji huyo hawezi kuitunza lakini ameamua kujiweka kwenye mstari huo kwa ajili ya mahusiano yao. 

Chanzo hicho kiliongeza kuwa Karrueche anampenda Chris kwa sababu wanaendana na anapenda upande mwema wa Chris Brown. 

Inawezekana Karrueche hamhofii tena Rihanna kwa kuwa mwaka jana alilazimika kuisomba mizigo yake kutoka kwenye nyumba ya mwimbaji huyo baada ya kumwagwa na himaya yake kuchukuliwa na RiRi bila sababu za msingi isipokuwa Chris kuamua tu kumrudisha RiRi. 


Kwa sasa Chris na Rihanna hawako pamoja tena na Karrueche anaonekana kukaba nafasi yake vizuri. Swali, je hii pembe tatu ya mapenzi yaliyojaa drama itaishia hapo au baadae itambidi KT aondoe tena mizigo yake kumpisha Rihanna?

VIKONGWE WATATU WAUAWA KIKATILI KWA KUCHOMWA MOTO HUKO BUNDA


MAUAJI ya kikatili yametokea usiku wa kuamkia leo wilayani Bunda, mkoani Mara baada ya watu wenye hasira wa kijiji cha Kasaula kuwauwa kwa kuwachinja kama Kuku kisha kuwachoma moto vikongwe watatu kwa kuwatuhumu wanajihusisha na vitendo vya kishirikina. 
 Pia watu hao mbali na kuwaua kikatili vikongwe hao kwa tuhuma kwamba walimuua kijana mmoja aitwaye Sale Ligolo, walichoma moto na kuteketeza nyumba walizokuwa wakiishi wazee hao pamoja na kupora kuku waliokuwa wakiwafuga na kuwatafuna kumaliza hasira zao.
 Kwa mujibu wa wa taarifa ya mwandishi Masau Bwire aliyepo Bunda kwa sasa, tukio hilo limetokea usiku wa kumakia leo baada ya watu hao wenye hasira kuwasaka ajuza hao baada ya kuwepo tuhuma kwamba walishirikiana kumuua kijana huyo hivi karibuni.
Kijana huyo alikufa kwa kugongwa na gari, lakini dereva aliyemgonga alidai hakuona kama alimgonga mtu ila mbwa na pia inaelezwa  tangu azikwe kijana huyo alikuwa akirejea kwa mkewe na kumuita nyakati za usiku pamoja na kusumbua familia yao akitaka apewe chakula na ndipo wanafamilia hao walipoamua kwenda kwa mganga kuchunguza tukio hilo. 
 Wakiwa kwa mganga,wanafamilia hao walitajiwa majina ya wanakijiji watatu wa kijiji hicho ambao hata hivyo walitoroka kwenda vijiji vya jirani pamoja na familia zao kabla ya usiku wa leo kuvamiwa walipokuwepo na kuangushiwa adhabu hizo za kinyama. 
Wa kwanza kushambuliwa na kuuwa ni bibi aitwaye Bi Mgala ambaye alikimbilia kijiji cha jiorani kwa rafiki yake aitwaye Bi Laya, ambapo walimkata miguu yote miwili na kumtenganisha kichwa na kiwiliwili kabla ya kumchoma moto ambapo hata hivyo kitu cha ajabu ni kwamba ziliungua nguo zake tu huku mwili ukiwa upo vile vile. 
Baadaye walimgeukia Bi Laya aliyekuwa akitaka kuwatoroka na kumfanyia unyama kama rafikie kwa kosa la kumhifadhi Bi Mgala kwa kuamini huenda wanafanya shughuli za kishirikina pamoja na baadaye kurudi Kasaula na kumnasa Bi Chausiku na kumfanyia kama walivyowafanyia ajuza hao wengine kisha kuchoma nyumba tatu. 
 Bibi wa tatu wanayemtuhumu pia kwa ushirikina, ametimka kijijini hapo, lakini nyumba yake imeteketezwa pamoja na kuku waliokuwa wakiwafuga kuporwa na watu hao na kutumia moto waliouwasha katika nyumba hizo kuwachoma na kuwala kwa hasira. 
Kamanda wa Polisi wa Bunda, Mika David Nyange amethibitisha juu ya tukio hilo la kusikitisha na kwamba wanedelea na upelelezi kwa nia ya kuwasaka waliohusika na kitendo hicho cha kujichukulia sheria mikononi.

" ANAYEDAI KUOMBWA RUSHWA YA NGONO AJITOKEZE HADHARANI."...HASHIM LUNDENGA

Hashim Lundenga.
Baada ya shutuma za rushwa ya ngono kuzidi kwa waandaaji wa shindano la Miss Tanzania, uongozi unaosimamia shindano hilo umesema kama kuna mrembo yeyote ambae amewahi kuombwa rushwa hiyo ya ngono ajitokeze.

Mkurugenzi Hashim Lundenga amesema “kuna kushutumiwa kwamba tunachukua rushwa ya ngono kutoka kwa Wasichana kitu ambacho sio kweli, hakuna msichana aliesema ameingia kambini au ameshinda kwa sababu ametoa rushwa ya ngono, katiba yetu inakataza kabisa yeyote kujihusisha na hilo”
Baadhi ya Warembo waliojitokeza 2012.
.
Toka Miss Tanzania ianze 1994 mpaka sasa kuna kesi zisizozidi nne za wazazi waliokuja kuwaondoa watoto wao kwenye kushiriki mashindano hayo baada ya kupata taarifa mbaya kuhusu hizo kashfa za ngono.

Moja ya kesi hizo ni pamoja na ya Mchungaji aliemuondoa mwanae baada ya kupewa ubalozi wa kinywaji chenye kilevi, mrembo mwingine alikua Nadya aliekua masomoni Chuo kikuu familia yake ilikataa kabisa mtoto wao kushiriki.
.
.
Lundenga amesema kuna wazazi wengine ambao walieleweshwa na wakaelewa akiwemo Mzee Muhere ambae aliposikia mtoto wake ameshinda Miss Kinondoni aliwapigia kelele sana lakini akaeleweshwa akaelewa na sasa mtoto wake anamiliki kampuni kubwa na anaendesha maisha vizuri kuliko baba yake alivyodhani.

Kwa kumalizia, Lundenga amekiri kwamba wanao utaratibu, sheria na kanuni kwenye katiba yao ambayo imepitishwa na Serikali ikiwa na maagizo mablimbali ikiwemo marufuku ya kiongozi yeyote kuomba rushwa ya ngono.
 
Pamoja na kuzushiwa hizo kashfa, amesema idadi ya Warembo wanaotaka kushiriki haijapungua bali imeongezeka kwa sababu Wasichana ndio wanazidi kujitokeza.

JACK WOLPER ALIA NA MATAPELI YANAYOTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KWA JINA LAKE KUOMBA HELA WATU


Katika kile kinachoonekana ni mwendelezo wa matapeli wa mjini kutumia majina ya waigizaji maarufu nchini kutapeli watu kwa njia ya mtandao, dhahama hii sasa imemkuta mwanadada Jacqueline wolper baada ya watu wanaoaminika kuwa ni matapeli kutumia jina lake kujipatia fedha na vitu vingine kiudanganyifu.

Akizungumza kwa simu na tovuti ya bongomovies, mwanadada Jacqueline wolper  alisema matapeli hawa sasa wameamua kutumia mtandao wa instagram na mtandao mwingine wa kijamii uitwao badoo kwa jina la “wolper gambe25” katika kutapeli watu kwa kuwaomba hela au michango mbalimbali kupitia account hizo feki

“Leo nilikuwa naenda saluni, baada ya kufika tuu, yule dada wa saluni akaanza kunilalamikia kuwa mbona sijaenda kuchukua viatu nilivyomuagiza pamoja na hela? 

 
Nikawa sijui cha kumwambia maana sikumuagiza viatu na wala sijampigia simu kumwambia anitumie hela, ndipo aliponionesha huo ujumbe kwenye simu yake na ndio nikagundua hizo account feki za hao watu wanaoutumia jina langu kutapeli watu” Alisema Jack.

“Mimi sipo facebook na wala sitarajii kujiunga, nawaomba sana mashabiki wangu wajue hilo. Natumia mtandao wa instagram kwa jina la wolpergambe au jacklinewolperjacklinewolper.”
Alisisitza Wolper

Pia alisema kuwa amegundua leo kuna mtu mwingine anayetumia jina lake kuomba watu wamchangie kuhusu kampeni inayoitwa “Zinduka” na amewataka sana mashabiki wake wasije wakafanya hivyo kwani mtu huyo ni mwizi na analengo la kumchafulia jina lake.

PENZI LA WASTARA LAGOMBANIWA.....


TAKRIBAN  wiki moja baada ya kumaliza eda tangu alipofariki mumewe Juma Kilowoko ‘Sajuki’ Januari 2, mwaka huu, staa mkubwa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma anagombewa na midume ikitaka kumuoa.
Akizungumza na mwandishi wetu  akiwa nchini Oman, Wastara alifunguka kuwa tangu amalize eda yake hiyo amekuwa akipata usumbufu mkubwa kutoka kwa wanaume mitandaoni na wanaomtamkia mwenyewe.
“Jamani mpaka nahisi kuchanganyikiwa kabisa, wanaume zaidi ya mia tano hata sijui walipotokea wanataka kunioa, hadi nahisi majanga,” alisema Wastara.

Wastara alisema kuwa wanaume hao wamekuwa wakihangaika bure kwa sababu kwa sasa hafikirii kabisa kuolewa kwani anapotembea bado anasikia harufu ya mumewe Sajuki.
 
“Bado harufu ya Sajuki ipo mwilini mwangu, wanaume wanaonitolea macho mtoto wa mwenzao wanakosea sana, sifikirii kabisa suala hilo kwa sasa,” alisema Wastara mwenye mtoto mdogo aliyezaa na Sajuki.

DUH! LULU ANAZIDI PENDEZA KILA SIKU, HEBU CHEKI PICHA HIZI HAPA UJIONEE MWENYEWE


Muigizaji wa kike aliyekulia kwenye tasnia ya bongo movie, kwa kuwa alianza tangu akiwa mdogo na hadi sasa kipaji chake kinazidi kung’aa. Haishii kung’arisha kipaji chake tu bali anazidi kuwa na muonekano wenye mvuto pia.


Lulu anaonekana hana stress tena kama ilivyokuwa siku kadhaa zilizopita alipokuwa chini ya ulinzi mkali akituhumiwa kusababisha kifo cha muigizaji mwenzake Steven Kanumba.


Huu ndio muonekano wa Lulu sasa hivi:

RAIS NKURUNZIZA WA BURUNDI AJA KUHUBIRI INJILI TANZANIA



Rais Pierre Nkurunziza.
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza, anatarajiwa kuja nchini Agosti, kuhubiri Injili katika mkutano mkubwa wa Injili unaoandaliwa na Baraza la Makanisa ya Kipentekoste nchini (PCT), imefahamika.

Kwa mujibu wa Askofu Samson Mlawi aliyezungumza na mwandishi wa habari hizi mwishoni mwa wiki, tayari  Kamati ya  Maandalizi imefanya vikao kadhaa ambavyo pamoja na mambo mengine, kamati ndogo zimeundwa ili kurahisisha ujio wa Rais huyo.


Alisema, kwa kutambua umuhimu na uzito wa ujio huo katika shughuli hiyo ya kiroho, kamati imeweka mtandao wa mawasiliano kuhakikisha waumini wa madhehebu hayo kutoka mikoa mbalimbali wanahudhuria mkutano huo ambao bado unatafutiwa uwanja.

Askofu huyo alisema Rais Nkurunziza pamoja na mambo mengine, anatarajiwa kuleta ujumbe wa amani na uvumilivu wa kidini hususan katika kipindi hiki cha mpito baina ya madhehebu ya Kikristo na Waislamu nchini.
 

“Mimi na wanakamati wenzangu, tunaamini Mungu atafanya kazi yake kupitia Rais kuhubiri Habari Njema kwa Watanzania kama ambavyo angehubiri mtu mwingine yeyote, lakini kutokana na nafasi yake ni matumaini yetu kwamba ujumbe huo utachukuliwa kwa uzito wa kipekee,” alisema.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Askofu, mwezi huo huo wa Agosti, Mwinjilisti wa Kimataifa wa Huduma ya Christ For All Nations (CFaN), Reinhard Bonkke anatarajiwa kuwasili nchini kwa ujumbe maalumu kwa waumini wa madhehebu ya Kikristo na  Taifa kwa ujumla.
 

Alisema, ujio wa wageni hao mashuhuri nchini, utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza shaka na wasiwasi kwa baadhi ya Wakristo ambao wako njia panda kuhusu masuala muhimu ya kiimani, ikiwa ni pamoja na suala la kuchinja.
 
Source:MPEKUZI HURU

UPDATE: TRENI YAUA UKONGA- MOSHI BAR




Muda mfupi auliopita treni imegongana na gari aina ya RAV4 na dereva (mwanaume)amekufa muda huu na abiria(mwanamke) yu mahututi.  

KAMA HUKUPATA NAFASI YA KUONA PICHA ZA KILICHOJIRI MAHAKAMANI SIKU RAMA MLA WATU ALIPOACHIWA HURU, BASI HUU NDO MDA WAKO KUZITAZAMA HAPA

Na Richard Bukos
HUKUMU ya kuwaachia huru washitakiwa waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya mauaji, Ramadhan Seleman Mussa ‘Rama Mla Watu’ na mama yake, Khadija Ally Seleman imeibua vicheko na vilio katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Ijumaa iliyopita.
Ramadhan Seleman Mussa ‘Rama Mla Watu’ akiwa na furaha baada ya kuachiwa huru.
Huku Ijumaa Wikienda likifuatilia hukumu hiyo hatua kwa hatua, hali hiyo ya taharuki ilitokea mara baada ya jaji wa mahakama hiyo, Rose Temba kuwaachia huru washitakiwa hao na kuibua sekeseke hilo huku mayowe ya vicheko na vilio vikitawala kutoka pande mbili zilizokuwa zikifuatilia kesi hiyo.
Ikumbukwe kwamba kijana Rama na mama yake walikuwa wakishitakiwa kwa kosa la mauaji ya mtoto Salome Yohana yaliyotokea mwaka 2008.
Wakati upande wa familia ya Rama ukigubikwa na furaha baada ya kuachiwa huru, upande wa wazazi wa Salome uliangua vilio kuonesha kutoridhishwa na hukumu hiyo.
Mama mzazi wa Rama, Khadija Ally Seleman.
Kabla ya hukumu, Jaji Temba alipitia mwenendo mzima wa kesi hiyo na kubaini kwamba mshitakiwa namba moja (Rama) alionekana kuwa na hatia na kuzitaja sababu zilizomtia hatiani kuwa ni kukamatwa na kichwa cha mtoto huyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kiwiliwili chake kukutwa kwenye tundu la choo nyumbani kwa washitakiwa hao, Tabata jijini Dar.
Hali kadhalika, mwili huo wa Salome ulikuwa umeviringishwa na fulana ya Rama.
Jaji Temba alisema sababu nyingine iliyowatia hatiani Rama na mama yake ni maelezo ya Rama kuwa mama yake ndiye aliyemuua Salome kwa kumkata kichwa kwa kutumia shoka na kumpa kichwa hicho ili akipeleke kwa shangazi yake anayefanya kazi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Jaji Temba alisema licha ya ushahidi huo, alipitia maombi ya wakili wa washitakiwa hao, Yusuph Shekha aliyeomba mteja wake, Rama akapimwe akili.
Mama mzazi wa marehemu Salome, Pendo Dustan.
Baada ya Rama kupelekwa katika Hospitali ya Mirembe mkoani Dodoma, jaji huyo alisema ripoti kutoka kwa daktari, Mndeme Erastus ilionesha kuwa wakati Rama akitenda kosa hilo alikuwa na matatizo ya akili.
Ripoti hiyo ilimfanya jaji huyo kuwafutia mashitaka washitakiwa hao kwa kuwa, mshitakiwa wa pili aliingizwa hatiani kutokana na maelezo ya mshitakiwa wa kwanza.
Baada ya kutoa maelezo hayo, jaji huyo aliwaachia huru Rama na mama yake lakini aliamuru Rama awekwe chini ya uangalizi kwenye hospitali ya wahalifu ya Isanga mkoani Dodoma hadi akili yake itakapotengemaa.
Baba wa marehemu Salome, Yohana Majana.
Kufuatia taarifa ya hukumu hiyo, ndugu wa washitakiwa walikuwa wakishangilia huku Rama akisubiriwa mtaani wakati upande wa wazazi wa Salome ulikuwa ukihuzunika na ‘kumaindi’.
Kwa upande wa familia ya Salome, waliokuwepo mahakamani hapo ni mama mzazi, Pendo Dustan na baba wa marehemu, Yohana Majana na Furaha Musa ambao walionekana kupigwa na fadhaa na kuangua vilio mahakamani hapo huku wakitafuta njia ya kukata rufaa.
“Jamani mwanangu, roho inaniuma sana! Kibaya muuaji wake leo ameachiwa, lazima tukate rufaa,” alisema mama wa marehemu huku akilia kwa kwikwi.
Anti wa Salome.
“Ina maana kesi ya Salome ndiyo imeishia hivyo, masikini Salome uuuwii,” alisikika mwanamke mwingine huku akiangua kilio.
Hali hiyo iliwafanya askari kuingilia kati na kuwatoa nje watu wote.
Watu wengi wamekuwa wakimsubiri Rama nyumbani kwao Tabata kwa lengo la kutaka kumshuhudia ‘live’.

HII NI NEEMA KWA WALIOFELI KIDATO CHA NNE....UFAULU WAONGEZEKA, MATOKEO NI MUDA WOWOTE

Idadi ya watahiniwa waliofaulu mtihani wa kidato cha nne mwaka jana imeongezeka kwa kati ya asilimia 20 na 23 baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), kufanya marekebisho alama za viwango vya ufaulu, Mwananchi limebaini.

Habari ambazo gazeti hili imezipata zinasema matokeo hayo ambayo yamewezesha kiwango cha ufaulu kupanda na kufikia asilimia kati ya 54 na 57, huenda yakatangazwa wiki hii pamoja na yale ya kidato cha sita ambayo pia yamechelewa kutangazwa.

Chanzo cha habari kutoka Necta kimesema matokeo hayo mapya yanaonyesha kuwa, ufaulu wa kuanzia daraja la kwanza hadi la nne umeongezeka kutoka asilimia 34.5 kwa matokeo yaliyotangazwa awali na huenda yakafikia asilimia 57. Hii inamaanisha kwamba watahiniwa wapatao 82,000 ambao awali walikuwa wamepata sifuri katika matokeo ya awali sasa wamepanda na kupata madaraja ya ufaulu katika matokeo mapya.

Kwa matokeo hayo, watahiniwa wa mwaka 2012 watakuwa wamefanya vizuri kuliko wa mwaka 2011, ambao watahiniwa 225,126 sawa na asilimia 53.37 ya 349,390 waliofanya mtihani huo walifaulu.

Msemaji wa Necta, John Nchimbi alisema upangaji wa matokeo hayo ulikuwa bado unaendelea. “Ninachojua kwa sasa ni kuwa mchakato unaendelea na matokeo yatatangazwa mapema tu ili watoto waweze kujiunga na shule mapema,” alisema Nchimbi.

Pia alisema usahihishaji wa mitihani ya kidato cha sita umekamilika.

Matokeo ya awali

Matokeo ya awali yaliyotangazwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa yalionyesha kuwa kati ya watahiniwa 367,756 waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana, waliokuwa wamefaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu walikuwa 126,847 sawa na asilimia 6.4. Waliopata daraja la nne walikuwa ni 103,327 sawa na asilimia 28.1.

Katika matokeo hayo, watahiniwa 240,909 sawa na asilimia 65.5 walipata sifuri, hesabu ambayo imebadilika katika matokeo mapya ambayo yanaonyesha kuwa sasa waliopata daraja hilo ni 158,100 ambayo ni asilimia 43.

Hata hivyo, habari kutoka Necta zinasema kuwa licha ya kuwezesha kuongezeka kwa waliofaulu, matumizi ya kanuni mpya ya kukokotoa matokeo hayo yalisababisha zaidi ya wanafunzi 2,500 kushuka ufaulu ikilinganishwa na awali.

Maofisa mbalimbali wa Necta pamoja na wale wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na taasisi zake, walikutana mwishoni mwa wiki iliyopita kukubaliana masuala mbalimbali juu ya matokeo hayo pamoja na suala la matokeo ya wanafunzi hao 2,500 kabla ya kutangazwa wiki hii.

“Baada ya wajumbe kujadili suala lile, busara ilibidi itumike kwa hiyo hakuna mwanafunzi ambaye alama yake itashuka, kwa kawaida isingewezekana mtoto ambaye matokeo yalitoka akiwa amefaulu leo umwambie ameshuka,” kilieleza chanzo chetu.

Matokeo ya awali ndiyo chimbuko la kupitiwa upya baada ya wadau kuyalalamikia na kumlazimisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuunda tume ya kuyachunguza Februari 23, mwaka huu.

Kabla ya tume hiyo kuhitimisha shughuli zake, ilitoa taarifa ya awali ambayo ilipendekeza kufutwa kwa matokeo hayo kwa maelezo kwamba Necta ilitumia kanuni mpya ya kukokotoa matokeo bila kushauriana na wadau.

Serikali ilitoa taarifa bungeni kwamba imeamua kufuta matokeo ya 2012 na kuamuru yapangwe upya kwa kufuata madaraja yaliyotumika mwaka 2011.


Mwananchi

Friday, May 24, 2013

WAASI WA M23 WATISHIA KUTUVAMIA MUDA WOWOTE....SERIKALI YA MKOA WA KAGERA YATOA TAHADHARI KWA WANANCHI


Serikali ya Mkoa wa Kagera imewatahadharisha wananchi wake kuepukana na wageni wasiowafahamu kwenye maeneo yao kutokana na tishio la kikosi chaM 23 cha nchini Congo DRC kinachotishia kuivamia Tanzania...

Kumekuwa na mapigano  makali  kati  ya waasi wa M23  na  vikosi vya serikali  nchini  Congo ambako jeshi letu lipo huko...

Waasi  hao  wametishia  kuivamia  Tanzania  muda  wowote  ili  kulipiza  kisasi.Miongoni mwa mipaka ambayo iko wazi  ni Kagera, na hii ndo sababu iliyopelekea  serikali ya Mkoa huo kutoa tahadhari kwa wananchi wake na watanzania kwa ujumla....

"UHUSIANO WA KIMAPENZI BILA NGONO NI KUONGOPEANA".....TOPE OSOBA

Muigizaji Tope Osoba wa Nigeria, amekataa kuwa na mahusiano bila ya kukutana kimwili, na kufunguka kwamba anashangazwa na wasanii wengi wa Ghana na Nigeria wamekuwa wakiolewa na wanaume zao kuishi nje ya nchi kwa zaidi ya mwaka na hakuna kati yao aliyepata nafasi ya kumtembelea mwenzake.

Ngono ni kitu cha kuburudishana kati ya wawili wapendanao. Ngono ni nzuri. Imeumbwa ili wapenzi wa-enjoy na kubadilishana siri za mioyo yao.” Alifunguka actress huyo.
Alipoulizwa kuhusu mapenzi kabla ya ndoa, Tope alisema: “Mapenzi kabla ya ndoa ni poa tu, al muradi usalama kwanza. kwanza tusidanganyane, hauwezi kudumisha uhusiano bila ngono.”
Alifafanua kuwa maisha ya namna hiyo hayapo na kama yapo yana kitu nyuma ya pazi kwa kuwa hakuna mwaminifu bila ya sababu ya msingi
http://laivu.com/maraha/files/2013/05/tope-osoba_350.jpg

KATIKA VURUGU ZA GESI MTWARA, ASKARI WATUHUMIWA KUMBAKA HADI KUMUUA KWA KUMPIGA RISASI YA TUMBO MAMA MJAMZITO WA MIEZI 7....!!

Hali ya usalama katika Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani hapa imezidi kuwa mbaya baada ya askari polisi kudaiwa kufanya unyama kwa kuwabaka wanawake na kumpiga risasi mjamzito

Mbali na unyama huo polisi pia wanadaiwa kuchoma moto nyumba tatu za wananchi katika mtaa wa Magomeni na vibanda vya maduka kadhaa na kupora vitu vilivyomo ndani.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara, Linus Sinzumwa anasema hali ni shwari na kwamba wananchi watoke nje kuendelea na shughuli zao kama kawaida.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Mohamedi Kodi amethibitisha kupokea mwili wa mjamzito ukiwa na tundu tumboni, zinazoaminika kuwa za risasi na hivyo kufanya idadi ya maiti zilizopokelewa hospitalini hapo kufikia mbili na majeruhi 18: “Ni kweli kwa leo tumepokea maiti moja ya mwanamke ambaye ni mjamzito wa
miezi saba, amepigwa risasi tumboni...” “...pia tumepokea mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Chuno, amevunjwa miguu yote kwa risasi.”

Habari zinadai kuwa mjamzito huyo ameuawa akiwa nyumbani kwake baada ya polisi kuvamia makazi yake.

Huduma za kijamii zimesimama, hakuna maduka yaliyo wazi, hakuna usafiri wa daladala wala pikipiki, mji upo kimya, sauti za milio ya mabomu na bunduki zimetawala, wanajeshi waliovalia sare wameuzingira mji wakiwa katika magari na pikipiki.
Picture
Wakizungumza na Waandishi wa Habari kwa nyakati tofauti wakazi hao wamelalamikia kitendo cha askari wa jeshi la polisi kuingia katika makazi yao, kuwapiga, kuwabaka na kuwapora mali zao:

“Magomeni A hatuna amani askari wanaingia majumbani mwetu wanatupiga na kutunyang’anya simu, yani huku Magomeni hatuna amani kabisa, tumepoteza watoto na hatujui hata waume zetu wako wapi” alisema Paulina Idd na kuongeza: “Majumba yetu yamechomwa moto wanaofanya fujo ni polisi wenyewe halafu wanakuja wanatubaka na kuiba mali zetu halafu tunateseka sisi yaani tumechoka kabisa na serikali yenyewe,” alisema Paulina.
Picture
Wanawake na watoto wakiwa hospitali ya rufaa ya Ligula, Mtwara kwa ajili ya kuomba hifadhi baada ya kuyakimbia makazi yao kwa hofu
Kamanda Sinzumwa alipoulizwa kuhusiana na tuhuma hizo alisema hawezi kuzungumzia suala hilo kwa madai kuwa atapingana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Mchimbi aliyewasili Mtwara leo: “Kuhusiana na suala hilo siwezi kulizungumzia kwa sasa kwani nitapingana na Waziri wangu kwani leo ametoa tamko bungeni na leo atawasili,” alieleza Sinzumwa

Wakazi wakimbia maeneo yao
Wakazi wa maeneo mbalimbali wamekimbia makazi yao hususani wanawake na watoto na kuhamia hospitali ya rufaa kwa kuhofia usalama wao huku wengi wao wakipotezana na ndugu zao.

Hali hiyo imetokea kufuatia kuwepo kwa milipuko ya mobomu katika maeneo mbalimbali mjini hapa huku huduma za kijamii zikiwa bado zimesitishwa. Hali hiyo imetokea baada ya kusambazwa kwa vipeperushi vilivyokuwa vikihamasisha wananchi wa mkoani hapa kusitisha huduma zote hapo jana  ili kusikiliza hotuba ya wizara ya nishati na madini.

Kufuatia hali hiyo imesababisha kifo kwa raia mmoja aliyefahamika kwa jina Karim Shaibu (22) mkazi wa Chikongola ambaye alipigwa risasi wakati wa fujo kati ya jeshi la polisi na wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari mganga mkuu wa mkoa hospitali ya rufaa ya Ligula Dk Sadun Kabuma alithibitisha kupokea kwa kifo hicho ikiwa ni pamoja na majeruhi 17 wakiwemo askari watatu: “Ni kweli jana kuanzia majira ya saa 10 hadi saa 11 nilipokea majeruhi 17 ambapo kati ya hao wamishtuko ni wanawake watano na askari watatu na kijana mwingine ambaye alikuwa na jeraha na katika harakati zan kumwokoa maisha yake alifariki akiwa chumba cha upasuaji,” alisema Dk Kabuma

Wananchi wazungumzia bajeti

Wakizungumzia uwasilishwaji wa hotuba ya Wizara ya Nishati na Madini wakazi wa hapa wamesema kuwa hawakubaliani na ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kwani mpango huo utawaletea dhuluma: “Mpango wa kusafirishwa kwa gesi asilia hatuna mpango nao kwa wakazi wote wa Mtwara kwa kifupi akina mama wa mtwara hatutaki itoke,” alisema Fatuma Abdallah.

Read more: http://talkbongo.blogspot.com/2013/05/katika-vurugu-za-gesi-mtwara-askari.html#ixzz2UCuhRSEQ

"NILIJIUNGA CHADEMA ILI NISAIDIE HARAKATI ZA UKOMBOZI WA TANZANIA NA SINA MPANGO WA KUGOMBE UBUNGE" ... PROFESA JAY

Mchawi wa rhymes, Profesa Jay amesema hakujiunga na CHADEMA ili mwaka 2015 awanie ubunge kama wengi wanavyodhani.




Rapper huyo wa ‘Machozi, Jacho na Damu’ ambaye jina lake halisi ni Joseph Haule, ameliambia gazeti la Mwananchi la leo kuwa amejiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ili kukisaidia chama katika changamoto za kuikomboa nchi.

“Kujiunga na siasa si dhambi na haina maana kwamba nina mpango wa kugombea jimbo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Sihitaji kugombea hata udiwani ila ni kwa dhumuni la kutaka kuongeza nguvu katika chama ili kuyafikia malengo,” ameliambia gazeti hilo.
 

Ameliambia kuwa yeye ni mfuasi wa Chadema tangu mwaka 2005 na amekuwa karibu na chama kwa nyakati nyingi lakini kwa sasa ameamua kuingia rasmi katika chama kama chachu katika kuongeza harakati kwa vijana.
 

“Nimeingia ili nisaidie hiki chama kuikomboa Tanzania kwani kwa muda mrefu niliokaa katika chama hiki nimegundua kuwa wamedhamiria kumkomboa msanii, kijana wa kawaida na wakubwa kwa wadogo hivyo nadhani nipo sahihi katika uamuzi wangu.”

BLA_EUCCQAEHZCc
“Natambua mimi ni mwanamuziki, sawa nina mashabiki wengi lakini haina maana kwamba sina haki ya kuchagua chama ninachoona mimi kinanifaa, lakini siwezi kusita kufanya kazi sehemu yoyote au wakati wowote chama kikinitaka nifanye kwa wakati husika,” alisema Profesa J

AIBU: MUME WA MTU ANASWA NA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI GESTI...!!


INAUMA sana! Wakati wazazi wakihenyeka na wakati mwingine kujinyima ili mabinti zao waweze kupata elimu bora itakayowasaidia maishani mwao wapo wapuuzi wanaokatisha jitihada hizo.

Mwanaume mmoja aitwaye Taliki Juma mkazi wa Temeke – Wailesi jijini Dar es Salaam ameingia  katika  dimbwi la AIBU baada ya kunaswa akiwa na mwanafunzi wa kidato cha pili wakifanya mchezo mchafu.

 

Mbaya zaidi, bila haya wala soni, Taliki alimwingiza binti huyo (jina na shule anayosoma vinahifadhiwa kwa sababu za kimaadili) katika chumba anachoishi na mwanamke anayedaiwa ni mke wake ambaye alikuwa safarini.

Chanzo chetu cha habari kilipiga simu chumba cha habari na kueleza juu ya tabia ya Taliki ya kwenda na denti huyo chumbani kwake tena akiwa kwenye sare za shule.

Kikao cha dharura kiliitishwa haraka baada ya sosi wetu kutoa maelekezo juu ya habari hiyo ambapo kwa muda huo na foleni za jiji la Dar usafiri uliopendekezwa ukawa ni pikipiki.


Haraka timu ya waandishi  wetu ilielekea eneo la tukio lakini kwa bahati mbaya walikwama.
 
Taarifa iliyopatikana kutoka kwa mtoa habari wetu ni kwamba, muda mfupi kabla timu haijaingia eneo la tukio, Taliki alifanikiwa kukwepa mtego baada ya kumuondoa denti huyo.


Wikiendi iliyopita Mei 18, mwaka huu chanzo chetu kilekile kilipiga tena simu kwa mwandishi yuleyule na kueleza kuwa jamaa kwa mara nyingine amemwingiza yule denti chumbani kwake.

Timu A iliondoka na kwenda moja kwa moja hadi eneo la tukio na kuliweka chini ya uangalizi huku timu B ikielekea katika Kituo cha Polisi cha Wailesi na kuomba ushirikiano wao.

Timu ya maaskari wa kituo hicho wakiwa tayari kwa lolote, waliungana na waandishi wetu kwenda eneo la tukio.

Waandishi wetu, maaskari na wazee wachache wa mtaani hapo walivamia katika chumba hicho na kufanikiwa kumnasa laivu Taliki akiwa na denti huyo kama walivyozaliwa akimfanyisha mambo ya kikubwa muda ambao alitakiwa kuwa darasani.


Binti huyo ambaye alionekana kushtuka sana baada ya kukutwa chumbani hapo, alieleza kuwa amekuwa katika uhusiano na Taliki kwa muda mrefu baada ya kumrubuni kwa fedha na zawadi mbalimbali.

“Ni kweli huyu hapa ni mpenzi wangu, huwa ananipa pesa. Nyumbani kwetu ni Mwananyamala na nimetoka nyumbani nikienda tuisheni lakini Taliki aliniambia nije kwake.
 

“Naombeni mnisamehe jamani. Mama akijua atanipiga sana. Nisameheni tafadhali na ninaahidi mbele yenu kuwa nitaachana kabisa na huyu mbaba (Taliki),” alisema denti huyo.
 

Denti huyo alitoa namba ya simu ya mama yake mzazi ambapo alipigiwa na kufika eneo la tukio na kujionea jinsi mtoto wake anavyoharibiwa wakati yeye akiwa kwenye juhudi za kumtengenezea maisha. 

Mama wa binti huyo, hakuamini alichokiona na alijikuta akimwaga machozi muda wote, watu wazima wakapata kazi ya kumtuliza.


UPUUZI WA TALIKI
“Ni kweli nakubali huyu ni mpenzi wangu na nipo naye muda mrefu ila naombeni sana mnisamehe, kwa kweli ni shetani tu alinipitia (Mh! Huyu shetani anasingiziwa mengi sana).
 
“Ndugu zangu wakijua hili jambo watanitenga, naombeni muwe na roho ya huruma (utadhani na yeye ana huruma), maisha yangu yataharibika (sijui alikuwa anamtengenezea yule binti  wa watu maisha?).”
 
Utetezi wake haukusaidia na badala yake alifikishwa katika Kituo cha Polisi Wailesi na kufunguliwa mashitaka katika Jalada namba WS/RB/585/2013 – KUFANYA MAPENZI NA MWANAFUNZI.
 
credit.gumzo la jiji
 

BAADHI YA MATUKIO YALIYOTOKEA MTWARA MANISPAA

  Baadhi ya wananchi wa eneo la magomeni mkoani mtwara wamekimbilia katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara Lugula wakihofia usalama wao kutokana na vurugu za kuchomwa kwa nyumba zao pamoja na vibanda vya biashara zilizotokea leo asubuhi katika eneo hilo..

Maduka maeneo ya Magomeni yamechomwa moto ikiwamo pia mali za Askari magereza . Mwanafunzi wa CHUNO amefikishwa hospitali Ligula na majeraha ya risasi mguuni.  
Mwanamke mwingine anayekadiriwa kuwa na miaka 25 mjamzito ameuawa kwa kupigwa risasi maiti ipo Ligula.




Kwa sasa( jioni  hii)  inaelezwa kuwa katika baadhi ya mitaa hali imetulia na ni idadi ndogo ya wananchi ndiyo inayoonekana wakitembea mitaani isipokua eneo la magomeni ambako mbomu yanaendelea kusikika huku huduma za kijamii katika mji huo zikiwa zimesimama zikiwemo usafiri, huduma za kibenki na shule

HATIMAYE DR. SLAA AKUBALIWA KUOANA NA MPENZI WAKE...





HATIMAYE Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, imetupilia mbali rufaa iliyokuwa imekatwa na aliyekuwa mume wa Josephine Mushumbusi( KWA  SASA  NI  MCHUMBA WA DR. SLAA) , Maimbo baada ya kuiona rufaa hiyo haina msingi wowote kisheria.

Hukumu hiyo ya rufaa ya  madai ya ndoa Na.32/2012 ilitolewa leo na Hakimu Aniseth Wambura ambapo alisema mahakama yake imefikia uamuzi huo wa kuitupa rufaa hiyo kwasababu haina mantiki ya kisheria.

Hakimu Wambura alisema mahakama yake imekubalina na hukumu iliyotolewa Aprili 2012 na Mahakama ya Mwanzo Sinza katika kesi ya madai talaka iliyokuwa imefunguliwa na Mushumbusi anayetetewa na wakili wa kujitegemea Philemon Mutakyamilwa  dhidi ya Maimbo ambapo mahakama hiyo ya chini ilitangaza kuwa hakukuwa na ndoa baina ya watu hao kwasababu Maimbo alikuwa ni mzinzi, simwaminifu katika ndoa yake na alikuwa akimtesa mkewe.

“Baada ya mahakama yangu kusikiliza hoja za mwomba rufaa na mjibu rufaa ,mahakama hii imefikia uamuzi wa kukubali hoja za Mushumbisi kuwa kwa tabia ile ya mbaya ya uzinzi na ukosefu wa uaminifu katika ndoa yake hapakuwepo na ndoa baina yao hivyo mahakama yake inatangaza kuwa hukumu ya mahakama ya Mwanzo Sinza ambayo iliivunja ndoa hiyo ilikuwa hukumu sahihi “alisema hakimu Wambura.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo wakili Mutakyamilwa alisema amefurahishwa na hukumu hiyo kwani mahakama imetenda haki  kwasababu kesi hiyo ya madai ya talaka ilikuwa na msukumo wa siasa chafu zilizokuwa na lengo chafu la kumchafulia jina mteja wake(Mshumbusi) ambaye kwa sasa ni mzazi mwenzie Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk.Wilbroad Slaa.
KWA  HIYO, KWA  SASA  DR. SLAA   NA  MPENZI  WAKE  W ANAWEZA  KUOANA..!!!

"ANA MIAKA 26 LAKINI NIMESHINDWA KUACHA PUNYETO, NIFANYEJE?"... NAOMBENI USHAURI

Mimi ni kijana wa miaka 26 ninaandika hivi kwa sababu nimeamua kuomba mawazo kwa wa wanajamii, kwa ukweli na uwazi mimi ni mtu ambaye nimekuwa na tabia ya kupiga punyeto kwa muda mrefu hili tatizo lilianza kipindi fulani nipokuwa mkoa fulani hapa Tanzania, Nlikuwa na rafiki yangu mmoja na mpaka sasa bado ni rafiki yangu ni mtu mzima na ameoa pia ana watoto yeye ni mfanya biashara ya kununua na kuuuza madini. Alipokuwa akitoka porini kama amechelewa anapita geto kwangu tunalaa sasa tukaanzisha mchezo wa kushikana sehemu zetu za siri mpaka tunamaliza kitu tunachotaka japo hatuingiliani. Tuliendelea na mchezo huo kwa muda mrefu kwa sababu imekuwa mazoea.
  Sasa tatizo langu liko hivi mimi kwa sasa niko nje kidogo na nchi yangu na yeye yuko na kazi zake za porini na akienda huchukua muda mrefu kurudi na mimi kulingana na mazoea inaniathiri kwa sababu kila ninapokumbuka ule mchezo namaliza nikiwa mwenyewe yaani yeye amekuwa kwenye kumbukumbu ya akilii yangu kwa sababu kuna siku tulifanya ule mchezo mpaka nikaona nimefika kileleni tofauti na wanawake niofanya nao mapenzi hakuna aliyetomasa mpaka nifikie hivyo. Na hii imenipelekea kila mwanaume ninayemwona kama ana umbo sawa na rafiki yangu natamani kufanya nae ule mchezo kitu ambacho kinakuwa ni ngumu. Na kila siku najaribu kujizuia kufanya huu mchezo ninashindwa sijui nitumie njia gani ili kuepukana na hili tatizo hili kubwa linalonisumbua.

LAANA: KAKA ANASWA AKILIFAIDI PENZI ZITO KUTOKA KWA DADA YAKE WAKIWA COCO BEACH.....!!

Wednesday, May 22, 2013 | 1:31 PM

UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Firauni. Usemi huu unakamilishwa na tukio la kunaswa kwa vijana wawili wenye undugu wa damu wakifanya mapenzi ‘wakiduu’ kando ya Ufukwe wa Bahari ya Hindi

Imefahamika kwamba vijana  hao, kaka na dada (majina tunayo)  wamenaswa ‘wakiduu’ katika mapango yaliyopo kando ya Ufukwe wa Coco, Oysterbay jijini Dar es Salaam.
TUKIO ZIMA
Tukio zima lilitokea mchana kweupe wa saa 9 na kudhihirisha habari za mara kwa mara zinazoeleza kwamba Ufukwe wa Coco umekuwa ukitumika kwa ufuska usiku na mchana.
Risasi Mchanganyiko lilinasa tukio hilo kwa kutumia mitambo maaalum iliyoelekezwa kando ya bahari.
Wawili hao walinaswa tangu walipokuwa wakiingia katika ufukwe huo na kuwafuatilia nyendo zao, hatua kwa hatua.


DEMU ALIKUWA AKIZINGUA
Haikufahamika mara moja kama wawili hao walikuwa na makubaliano ya kwenda kuduu katika ufukwe huo au la, lakini kwa mbali ilionekana kama vile dada mtu alikuwa akizingua kwenda kutenda dhambi hiyo.
Picha za video zilizonaswa, zinamuonesha dada huyo akionekana kutoa upinzani pale alipokuwa akishikwashikwa na kaka yake.
Alionekana kama vile hakuwa tayari kwa mchezo huo.
Hata hivyo, kaka mtu anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 23-26 alikuwa akilazimisha kitu fulani ambacho kilionekana dhahiri kupitia kamera zetu.
Ni kama vile hawakuwa na makubaliano na kile walichokuwa wakienda kukifanya.
Mara kadhaa dada huyo alionekana kumkwepa kaka yake na alikuwa akijiondoa karibu yake pale alipomlazimisha kutaka kumfanyia kitu kisichokuwa cha kawaida.


KAMERA ZAELEKEZA KWAO
Kamera za Risasi Mchanganyiko ziliwafuatilia wawili hao kwa kuwa walionekana kuwa na kitu ‘spesho’.

WAINGIA MAPANGONI
Mpaka wanazama katika mapango yaliyopo kando ya ufukwe huo wa Coco, kamera zilikuwa zikiendelea kuwachukua hadi walipozama ndani kabisa ya mapango hayo.

WANASWA LIVE
Walipozama ndani ya mapango hayo, ghafla walitokea askari ambao nao walikuwa wakifuatilia nyendo za wawili hao.
Askari hao wa Kituo cha Oysterbay, wakiongozwa na kamanda wa oparesheni maalumu katika Wilaya ya Kinondoni, Kamanda Swai walifuatilia kwa umakini tukio hilo.

WANASWA
Wakiwa chini ya mapango, kaka na dada waliondoa ‘viwalo’ vilivyokuwa maungoni mwao na kuanza kuduu kama vile walikuwa katika ufukwe unaoruhusiwa kufanya vitendo hivyo.

WAKUTWA WATUPU
Kabla askari hawajawavamia, waliwashuhudia wawili hao wakiwa katika kilele cha sterehe yao huku dada mtu akionesha kutoa ushirikiano kwa shingo upande.
Ghafla, askari waliwavamia na kuwatibulia starehe yao kisha kuwatia mbaroni.

 
 KAKA ATAKA KUFANYA FUJO
Baada ya kuona kuwa wamevamiwa na askari, kaka mtu alichomoka na kutafuta silaha ili kuweza kujihami na wavamizi wake bila ya kujua kama ni askari.
Katika hilo nusura zipigwe kati ya askari na kaka huyo ambaye alikuwa akitaka kupigana na watu asiowajua kwa kuwa walikuwa wametinga mavazi ya kiraia.
Hata hivyo, alitulizwa na kutakiwa kuvaa pensi yake ili aweze kutoa maelezo kwa kina.

DADA APIGWA NA BUTWAA
Wakati yote yakiendelea, dada mtu alikuwa amepigwa na butwaa na kutojua cha kufanya hadi aliporushiwa kitenge chake kilichokuwa pembeni ili ajisitiri mwili wake.

SIRI YAFICHUKA
Katika mahojiano ya awali yaliyoongozwa na Kamanda Swai, ilibainika kwamba wawili hao ni ndugu wa damu yaani kaka na dada.

DADA ALITOKA MKOA
Maelezo hayo yanasema kuwa dada mtu alitoka mkoani na alikuja kutembea jijini Dar es Salaam, ndipo kaka yake alipomtaka watoke kwenda kumuonesha vivutio vya jiji hilo.
“Nina miaka 19, nimetokea Iringa kuja Dar kutembelea familia lakini kaka akanileta huku na kunifanyia vile, siyo kama tulikuwa tumekubaliana,” alisema dada huyo kwa aibu.
Kaka mtu alikiri kile kilichosemwa na dada yake na kushindwa kujitetea kwa kuwa kila kitu kilikuwa hadharani.

WASEKWA RUMANDE
Wawili hao walichukuliwa na kupelekwa katika Kituo cha Oysterbay kwa ajili ya kufunguliwa kesi ya uzembe na uzururaji na kusekwa rumande kabla ya kufikishwa mahakamani.

SOURCE.GUMZO LA JIJI