Monday, July 22, 2013

SHILOLE ATANGAZA BIFU LA NGUMI BAADA YA SINTAH KUMPONDA KUWA ANAUWEZO MDOGO KIMUZIKI



MWIGIZAJI wa kike wa filamu na muziki Bongo zuwena Mohamed ‘Shilole’ amemtangazia hali ya hatari msanii mwenzake wa filamu na mtangazaji wa televisheni Christina John ‘ Sintah’ kuwa popote atakapomkuta lazima amchape kwa kipigo ambacho hatasahau katika maisha yake...

Shilole  ametoa kauli hiyo kufuatia kuandikwa na mwanadada huyo katika mtandao wake akimbeza kwa kejeli. .
“Ni kweli sisi wanawake hatupendani na kuwa na wivu wa kijinga, mtu anakurupuka anakotoka bila hata kufanya utafiti na kunibeza eti sina uwezo wa kuimba na JLO (Jenifer Lopez) ....

"Kuna mtu aliyetegemea mimi kwenda kufanya show Marekeni! Sasa ninachomwambia ninamtafuta nikikutana naye nimtapa kipigo cha Mbwa mwizi,”aliongea kwa hasira Shilole.

Katika mtandao wake Sintah aliandika kwa kusema Shilole ni sawa na mtu anayeota ndoto za mchana, na kumkejeli kwa kusema kuwa aendelee kuota anaweza baadae kurudi katika hali yake...

  Sehemu ya maneno yanayomkera Shilole ni haya: 
“Shilole bwana hii week katujia na kali kuliko eti ameongea na Benny Medina (Jlo’s Manager) ili aweze kufanya collabo na my sister, heee yes inawezekana maana hakuna lisilowezekana chini ya jua lakini swali ni?? wataimbaje?? yule dada yake na mie ni RnB na music wa Shilole bado sijaujua ni chakacha ama nini sasa naomba msaada kwenye tuta wadau wa music, hili linauwezekano??,”
 

“ Chakacha na RnB?? Kwa sababu Shilole nyimbo zake sawa na Snura wa majanga, kidogo Linah angeniambia ana collabo na my sisy ningeelewa sasa Shilole?? Ndoto za mchana ila si vibaya kuota maana ukishtuka unarudi ktk reality,”

Shilole anasema kuwa hajawahi kumuona mwanamke mwenye roho dhaifu kama Sintah, anajifanya anambabaikia Jlo wakati hata hajulikani....

“Mimi sikuwa nimeenda Marekani kwa ajili ya kuomba kumshirikisha J-lo kuimba naye,  lakini baada ya meneja wake kuja kuniona na kumpelekea video za muziki wangu  JLO alikubali kufanya kazi na mimi...

"Ilitakiwa nionane naye siku ya Jumapili lakini ndio siku niliyoondoka na ninarudi huko kwa ajili ya kazi hiyo, sijui nikifanya naye kazi atajificha wapi?,” anasema Shilole.

Shilole anasema Mungu ni mkubwa hata kama kuna mtu anayemchukia kwa mafanikio yake bado Mungu ana nafasi kubwa kuwazima watu wenye roho mbaya wivu kama Sintah ambaye anaonekana yupo tayari kwa ajili ya kuwaombea matatizo watu wanaojituma kwa ajili ya kuendesha maisha yao. 

-Via FC

JOSEPH LUDOVICK AFUNGUKA....ADAI KWAMBA MATESO YOTE ANAYOYAPATA NI KWA AJILI YA CHADEMA




SIKU chache baada ya Mahakama kumuachia kwa dhamana mshitakiwa mwenza wa Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare, Joseph Ludovick, amefunguka na kuelezea tuhuma ambazo zimekuwa zikielekezwa kwake, ikiwamo uhusiano wake na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mwigulu Nchemba.

Ludovick, ambaye anadaiwa kurubuniwa na Nchemba na hivyo kumrekodi Lwakatare wakipanga mipango ya kumdhuru Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mwananchi, Denis Msaky, alijitokeza juzi katika mtandao wa kijamii wa Mabadiliko na kuomba kuulizwa jambo lolote, kwa kile kilichoonekana kutaka kujibu tuhuma ambazo zimekuwa zikielekezwa dhidi yake.

Maswali na majibu yake ilikuwa ni kama ifuatavyo;


KUHUSU UHUSIANO WAKE NA MWIGULU

Akielezea uhusiano wake na Mwigulu baada ya kuulizwa swali na mtu aliyejitambulisha kwa jina la Abdul Dello, Ludovick alisema ni wa kawaida na kwamba haufikii kama ule wa Lwakatare na Maggid Mjengwa.

“Tumejuana kwenye mitandao ya kijamii na tukadevelop ukaribu, ilitokana na mimi kukosoa mijadala yake na kumpinga.

“Ninayo mahusiano na watu wengi tu nje ya Chadema. Mfano ni huyo Mwigullu, Sixtus Mapunda, Mbunge Kangi Lugora, nk.na sidhani kama ni dhambi hii. Wapo wengi tu wenye uhusiano kama huu. Wote hawa katika nyakati tofauti tumesaidiana mengi.

Katika swali lake lingine, Abdul Dello alihoji: “Ludo, Mwigulu Nchemba alithibitika kukutumia m-pesa ya elfu 50 ilikuwa ya kazi gani?

Ludovick alijibu akieleza kuwa: “Nilikuwa na tatizo binafsi la kifamilia, nilihitaji msaada.”
KUHUSISHWA NA USALAMA WA TAIFA
Mtu mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Hamis Hamad alimuuliza akisema:

“Ludo, unasemwa sana mtaani kuwa wewe ni TISS Agent (wakala wa usalama wa taifa) uliyepachikwa pale Chadema kwa ajili ya kuiua kifo cha kawaida na ndiyo maana unafanya kazi nyingi za kujitolea badala ya kwenda kufundisha kama taaluma yako ya ualimu inavyokuruhusu, kweli?

Majibu ya Ludovick yalikuwa hivi: “Nchi hii tunapenda majungu tuuu, na magazeti yetu yamebobea kusambaza majungu na kupakazia watu. Huwezi kuelewa dhana hii hadi ikukute. Juu ya kazi ni tofauti za kimtazamo, so wengine wanapenda kuajiriwa na wengine hawapendi, so haicount hii. Ni uamuzi tu. Niliijua Chadema 2006 na kujiunga rasmi 2009. Hakuna aliyenipachika huko. Ni by conviction, nakuhakikishia hata matatizo yote ninayoyapata ni kwa sababu ya Chadema.”

AELEZA ANAVYOMFAHAMU LWAKATARE


Boniface Magessa alimuuliza hivi: “Ludovick, elezea kidogo unavyomfahamu Lwakatare. Siku ya tukio la kurekodiwa ulikuwa wapi? Kama mlikuwa wote siku hiyo, ulikaa mbele yake au nyuma yake?

Ludovick: “Magessa, Lwakatare tumekutana Bukoba 2010 wakati wa kampeni. Tumefahamiana kwa sababu ya Chadema tu. Na ameendelea kuwa rafiki yangu na kiongozi wangu.

Siku ya tukio la kurekodiwa nilikuwa nyumbani kwake Lwakatare. Siyo muhimu juu ya location”.

MASWALI MENGINE
Leila Sheikh alimuuliza hivi; “Ludo, eti uliwahi kuruka ukuta usiku fulani?

Ludovick: “Da Leilah umefunga wewe? Sasa haya ya kuruka ukuta usiku fulani ni nini tena? Teh teh, hebu fafanua? Marcois, siku hizi kibwagizo changu ni kuwa natazama yote haya nayo ni ubatili mtupu, ni sawa na kufukuza upepo”.

Swali lake lingine lilisomeka hivi: “Kama wewe ni mwanachama hai wa Chadema kwa nini umeitwa 'msaliti' na shabiki wa Chadema kuwa ile kanda ya Lwakatare ulitumwa na Mwigulu kuipiga? Je, ile kanda ni ya kweli?

Inadaiwa kuwa ile kanda inaonesha nia/mpango wa kumuumiza Msacky.

Katika majibu yake Ludovick naye alijibu “Leila, mimi ni Mwanachadema hai. Kuitwa msaliti ni hali halisi ya sasa. Lakini inawezekana kuwa mimi wanayeniita msaliti, siku moja wakaona kuwa ndiye mwokozi. 

 
Fikiria kama ningekuwa natumika kama mnavyosema, kwa nini kesi ya ugaidi imefutwa? Si ningesema tu kuwa kulikuwa na watu wengine kadhaa? Kama ninatumika, kwa nini nikamatwe Iringa na kusafirishwa usiku tena chini ya ulinzi mkali? Leila teh teh kwamba nilitumwa kurekodi ile kanda!!! Yaani na Lwakatare naye akatumwa ili aongee haya tunayotuhumiwa kuyapanga? 


Na je, suala hili ikionekana kuwa ni kweli Lwakatare alilifanya, nani atakuwa msaliti kwa Chadema? Je, chama chetu kinazo sera za kudhuru waandishi? Sasa msaliti ni yule anayechafua chama kwa kupanga mambo yasiyoendana na sera za chama? Au ni yule anaye kilinda chama? Haya si nyote mnajua concept ya whistle blowers? Hamtegemei wawemo ndani ya Chadema?

Na je, kama Mahakama itaamua kuwa tuhuma zetu ni kweli bila chembe ya shaka, ninyi mtaendelea kusema nini, kuwa mimi msaliti au wote sasa tutakuwa wasaliti? Naomba tuachie mahakama suala hili. Kuitwa msaliti wakati unaumia kwa ajili ya hao wanaokuita wasaliti, kibinadamu inaumiza sana. Na hilo ndilo linanitokea.

Kuhusu kwa nini watu wote wananilaumu, si kweli. Wapo wasioona hivyo, ila in a great party propaganda chafu za CCM na za Chadema zimenifanya muhanga wa mambo haya. Uhusiano wangu na Lwakatare kwa sasa ni wa mashaka sana.

Swali jingine la Sheila ni hili: “Je, wewe bado mwanachama wa Chadema? Kama ndiyo, mbona walikutema kwa muda ukakaa rumande bila dhamana? Kwa nini wewe ambaye ni volunteer wa Chadema ulikanwa pale baada ya kushikiliwa na polisi? Huo ndiyo u****wa kafara.

Alijibu hivi: “Mimi ni mwanachama wa Chadema na nakuhakikishia mateso yote ninayoyapata ni kwa sababu ya Chadema.

Masharti ya dhamana hayakuwa wadhamini wawekwe na Chadema, bali watu wawili. Sasa sidhani kama Chadema walikuwa na kesi mahakamani hadi watafute wadhamini. Kuhusu kuwa volunteer wa Chadema ni majungu niliyoyazungumza. Sijawahi kuwa volunteer wa Chadema. Mimi ni mwanachama wa kawaida.

Nyoni Magoha alimuuliza hivi: “Wewe bado una imani na Chadema? Utaendelea kuwa mwanachama hai au umeshajitoa/utajitoa?

Majibu ya Ludovick: “Ninayo imani kubwa sana na isiyotetereka kwa Chadema. Nitaendelea kuwa mwanachama hai”.

Hata hivyo, Ludovick ambaye anatajwa kuhusika na tukio la kutekwa na kujeruhiwa kwa Mhariri Mtendaji Mkuu wa New Habari (2006) Ltd, Absalom Kibanda, alikwepa kuzungumzia jambo hilo na hata alipoulizwa baadhi ya maswali yenye mwelekeo huo.

Kuhusishwa Ludovick na tukio la Kibanda kunatokana na utata wa kauli na mwenendo wake siku ambayo Mhariri Mtendaji huyo alijeruhiwa.


Mtanzania:

BATA MTAMU: VIDEO YA MWANAMKE AKIZINI NA CHUPA YA SODA ...

BATA MTAMU: VIDEO YA MWANAMKE AKIZINI NA CHUPA YA SODA ...

COMPUTER ZA USHAHIDI ZILIZOTUMIKA KWENYE UWIZI WA ATM ZAIBIWA NDANI YA KITUO CHA POLISI - MAKAO MAKUU MWANZA



Siri za wizi uliotokea Makao Makuu ya Polisi mkoani Mwanza zimeanza kuvuja ambapo imebainika kuwa kompyuta aina ya laptop zilizoibwa ndani ya chumba cha vielelezo zilikuwa za ushahidi wa kesi ya wezi wa mashine za kuchukulia fedha(ATM).


Katika wizi huo wa benki ambao ulifanyika kwenye mashine za ATM mbalimbali na watuhumiwa watatu kunaswa Februari 10, mwaka huu saa 6 usiku wakiiba kwenye ATM za NMB,Tawi la PPF Plaza, Polisi walinasa vitu vingi vya watuhumiwa hao ikiwa ni pamoja na kompyuta mbili ambazo zinadaiwa kuibwa kituoni hapo juzi.



Habari zilizopatikana kutoka ndani ya Polisi zimeeleza kwamba katika wizi huo uliotokea katika maghala ya Polisi, moja kati ya vifaa vilivyoibwa ni mafaili mbalimbali ya vielelezo kadhaa vya kesi zinazochunguzwa na polisi ikiwa ni pamoja na laptop hizo ambazo zilikuwa ni ushahidi kwa kesi hiyo ya wizi wa ATM.



Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Ernest Mangu alipoulizwa kuhusiana na vielelezo vilivyoibwa Polisi, alikanusha kwamba laptop hizo zilikuwa kielelezo cha kesi za wizi wa fedha katika ATM lakini pia hakuwa tayari kueleza zilikuwa za kesi gani.



Wakati Kamanda huyo akikanusha baadhi ya askari ambao wanahusika na uchunguzi huo wamedai kuwa wizi huo uliendeshwa na maofisa wa polisi wasio waaminifu na kubainisha hakuna wizi unaoweza kufanywa na watu kutoka nje ya polisi.
mpekuzi:

WAVAA VIMINI WAPIGWA MARAFUKU KUINGIA HOSPITALI YA MKOA WA DODOMA



MGANGA Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Dk Ezekiel Mpuya amesema tangazo lililotolewa hospitalini hapo la kuwataka watu kuvaa mavazi ya heshima wanapoingia hospitalini hapo lilikuwa likihusu watumishi wa hospitali hiyo na si wananchi wa kawaida.


Akizungumzia suala hilo juzi, Dk Mpuya alisema kuwa Katibu wa Hospitali hiyo alitoa tangazo hilo kimakosa hali ambayo ilisababisha walinzi kuzuia watu waliovaa ‘ovyo’ kuingia hospitalini hapo.
“Uongozi wa Hospitali unaomba radhi kwa usumbufu waliopata wagonjwa na wananchi waliofika hospitalini hapo kwani tangazo lilitolewa kimakosa na Katibu kwani lilikuwa likiwahusu watumishi pekee na si wananchi,” alisema Dk Mpuya.


Kwa mujibu wa tangazo hilo, Hospitali ya Mkoa wa Dodoma iliweka masharti ya uvaaji ambapo mavazi yaliyopigwa marufuku ni sketi fupi, fulana zisizo na mikono nguo za kubana pamoja na Jeans.


Juzi kulitokea kutoelewana kati ya walinzi na watu waliokuwa wakitaka kuingia hospitalini hapo na kuzuiwa kutokana na aina ya mavazi waliyokuwa wamevaa.

LINAH AKANUSHA MADAI YA KUBAKWA USIKU BAADA YA KULEWA



Mrembo na mwanamuziki wa kike nchini, Linah Sanga amezikanusha ripoti zilizosambazwa leo kuwa amebakwa na rapper Kimbunga na kudai kuwa ameshangazwa mno na taarifa hizo.

Taarifa hizo zimeanza kusambazwa leo mchana baada ya akaunti ya Facebook inayoonekana kuwa ya rapper Kalapina yenye jina ‘KalApina Kikosi Cha Mizinga’ kuandika:
 
“Mtoto kimbunga amechamba ana leta usela mavi mambo ya kizamani hivi yupo chini ya ulinzi osterbay police kwa kosa la kumbaka msanii lina.”

Mwandishi wetu amezungumza na Linah ambaye amesema amepigiwa simu na watu wengi wa karibu kumuuliza suala hilo wakiwemo, Barnaba, Ditto, Amini na mtangazaji wa Clouds FM, Soudy Brown.

 
Amesema Soudy alimwambia kuwa ameziona taarifa hizo kwenye Facebook kwenye akaunti ya Kalapina.
“Sasa nikasema Kalapina ameandika hivi, kwasababu sijaingia mwenyewe kuangalia chochote. 

"Sikutaka kujipa stress kwasababu kuna kazi nafanya nisije nikaharibu kazi kwahiyo nikaona vitu vingine kama hivi ni vya kupotezea tu lakini sio vizuri kabisa yaani.

 "Kiukweli sijapenda, yaani bora mtu anizushie kitu kingine chochote lakini si suala kama hilo hapo, si suala zuri,” amesema Linah.
 
Amesema jana usiku alitoka na mpenzi wake kwenda kwenye sinema na wakarejea nyumbani salama.


“Sasa sielewi huko kubakwa nimebakwa saa ngapi na nilikuwa na boyfriend wangu labda yeye ndio kanibaka! Maana mtu wanayeniambia amenibaka Kimbunga, huyo Kimbunga hata simjui, namskia tu.
 
Nashindwa kuelewa, kwanini mtu azushe kitu kama hicho yaani ndo nataka kujua source ni nini. Niko fine yaani, kwasababu naelewa ‘it’s not true, lakini nafikiria huyo mtu mpaka kaamua kunifanyia kitu kama hicho, nimemkosea nini au kuna kitu gani, yaani hicho ndio kinaniumiza kichwa.”

Saturday, July 20, 2013

NAMBA ZA SIMU ZA MAWAZIRI ILI KUWATUMIA MAONI KUHUSU KODI YA SIMU


Kufuatia kauli za Serikali magazetini kuhusu mimi na kodi ya umiliki wa kadi za simu; nijibu tu kwa ujumla kwamba SITAACHA. Badala yake naomba kuwapatia namba zao: Makamba 0767783996 na Mgimwa 0754/0684765644, tunachohitaji ni kauli ya Serikali kuwa kodi imesitishwa na itaondolewa na sio siasa chafu. Kwa mliotaka msimamo wangu juu ya kauli ilinukuliwa jana tarehe 18 Julai 2013 na Gazeti la Majira kwamba Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Januari Makamba kwamba; “Mnyika anaangalia upepo unakoelekea, akiona watu wanalalamika ndipo anaongea namsihi aache kufanya siasa katika jambo hili”, naomba kutumia mtandao huu kutoa majibu ya ujumla kwa maswali na masuala yote kama ifuatavyo:

Nieleze kwamba sitaacha kufanya siasa kwenye jambo hili mpaka kodi hiyo itakapofutwa kuwawezesha wananchi wa kipato cha chini kubaki na fedha walau kidogo kwa maendeleo.

Sitaacha kufanya siasa kwa sababu ndio kazi yangu ambayo wananchi walinichagua kuifanya ya kuwawakilisha na kuisimamia Serikali ambayo yeye Makamba ni sehemu yake. Sitaacha kufanya siasa kwa sababu Mwalimu Nyerere alisema ili nchi yetu iendelee inahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora.

Ambacho sitafanya ni siasa chafu kama hizo ambazo Makamba amefanya za kusema uongo, kwa kuwa naamini anafahamu kabisa kwamba sijaanza kuongea kuhusu suala hili baada ya malalamiko ya wananchi bali jambo hili nilianza kulishughulikia bungeni mara baada ya Waziri wa Fedha kuwasilisha jedwali la marekebisho la kuanzisha kodi lukuki za simu ikiwemo hii. Katika mchango wangu bungeni, nieleza kwamba muswada huo wa sheria ya fedha kwa kupandisha kodi kwenye mafuta na simu ni ‘muswada wa majanga ya kuwaongezea mzigo wa gharama za maisha kwa wananchi.

Aidha, sikuishia kusema tu kwa niaba ya wananchi bali nilichukua hatua kwa mujibu wa kanuni za Bunge nami kuwasilisha jedwali la marekebisho ya kupinga kodi ya umiliki wa kadi za simu pamoja na kodi nyingine zote zenye kuongeza mzigo wa gharama za maisha kwa wananchi sio kwenye sekta ya mawasiliano bali pia kwenye sekta zingine ikiwemo sekta ndogo (sub sector) nyeti ya mafuta.

Mlioniuliza kwa SMS katika simu na kwenye mitandao ya kijamii sasa ni wakati wa Makamba kuhojiwa kwa njia hizo hizo (Simu yake ya Mkononi ni 0767783996) kwa kuwa yeye ni sehemu ya Serikali na Serikali ndiyo ambayo iliingiza suala hili kwa mara ya kwanza ndani ya ukumbi wa Bunge kupitia hotuba ya Bajeti Serikali na ikalirudia kuliingiza kupitia jedwali la marekebisho ya Sheria ya Serikali; ni wakina nani hasa kwa majina ndani ya Serikali na Bunge walioingiza kodi hii? Na ni wakina nani hasa waliopigia kura ya ndio kuipitisha?

Aidha, amenukuliwa na gazeti la Mwananchi la leo tarehe 19 Julai 2013 akieleza kwamba hakubaliani na suala hili na kupita kwake ilikuwa na kuzidiwa nguvu. Hivyo, ataje kwa majina hayo waliozidi nguvu serikali kinyume na matakwa yake. Amenukuliwa akisema pia kwamba anajua kuwa suala hili haliwezi kutekelezwa na kwamba ni lazima litabadilishwa kwa kuangalia eneo lingine la kutoza kodi. Ni vizuri akahojiwa, ikiwa huo ni msimamo wa Serikali; mwenye mamlaka ya kusitisha kodi hiyo ni nani na kwanini hajitokezi kutoa agizo la kusitisha wakati maandalizi yakiendelea ya kupeleka muswada bungeni wa kuifuta kabisa kodi hiyo katika mkutano ujao?

Wakati Naibu Waziri akisema hayo, Waziri wa Fedha Dk William Mgimwa katika Serikali hiyo hiyo yeye ametoa kauli tofauti siku hii hii ya leo ambapo kwa mujibu wa gazeti la Mtanzania amewataka watumiaji wa mitandao ya simu nchini na watanzania kwa ujumla kuwa na subira kuhusu tozo ya sh 1000 kwa mwezi kwa kila laini ya simu za kiganjani.

Na kwa kuwa amesema kwamba Serikali inaendelea kupokea maoni kutoka kwa wadau, natoa mwito kwa wananchi kumtumia maoni kupitia namba zake za simu za mkononi 0754/0684-765644. Aidha, ni vizuri aeleze subira hiyo ivutwe mpaka lini? Na ni wakina nani hasa kwa majina waliomfanya akaingiza kodi hiyo katika kitabu cha Hotuba yake aliyosoma bungeni kuhusu bajeti ya Serikali na wakina na hasa kwa majina waliomfanya arejeshe kodi hiyo ya kadi za simu kwenye jedwali la marekebisho ya muswada wa sheria ya fedha alilowasilisha bungeni.

Nasisiza kuwa kauli za ujumla za Serikali bila kuwataja kwa majina wahusika ni za kujivua mzigo wa lawama baada ya malalamiko ya wananchi kuhusu kodi hii na nyinginezo kwa kuhamisha mzigo huo kwa wabunge. Ni muhimu badala ya kutoa kauli za ujumla za kulaumu wabunge, Rais ama kiongozi mwingine mwenye mamlaka ajitokeze kusitisha kutozwa kwa kodi hiyo na kuanzisha mchakato wa muswada wa kufuta kodi hiyo kuwasilishwa katika mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanza tarehe 27 Agosti 2013.

Majina ya wahusika yasipotajwa au mamlaka zinazohusika zisipotoa kauli katika mkutano wa hadhara nitakaoshiriki jumapili tarehe 21 Julai 2013 katika Uwanja wa Sahara kata ya Mabibo kuanzia saa 8 Mchana mpaka saa 11 Jioni nitatoa mrejesho kuhusu yaliyojiri katika mkutano uliopita wa Bunge na kueleza hatua zaidi zinazopaswa kuchukuliwa kuwezesha majina ya wabunge hao kutajwa hadharani na hatua za kuondoa kodi hiyo kuchukuliwa. 



Uongozi bora na uraia mwema wenye uwajibikaji ni chimbuko na chachu ya ukuaji endelevu wa uchumi wa nchi na ustawi wa maisha ya wananchi. Twende kazi.
John Mnyika (Mb)
19 Julai 2013

HIKI NDO KICHAPO WANACHOPEWA WAASI WA M23 NA JESHI LA KONGO ( FARDC )


 Goma -DRC.
WAKATI mapigano yakizidi kuwa makali kati ya wanajeshi wa DR Congo (FARDC) na kundi la waasi wa M23, wanajeshi wa DRC wako hatarani kushitakiwa kwa tuhuma za kuwatesa waasi na kunajisi maiti zao.
 
Wanajeshi hao wanatuhumiwa kwa kosa la kukiuka haki za binadamu na sheria za Umoja wa Matifa (UN) inayokataza ukiukwaji wa haki za binadamu huku ukikataza watuhumiwa na mateka wa kivita kufanyiwa vitendo vyovyote vinavyo ashiria kukiuka haki zabinadamu badala yake mateka wote wanatakiwa kushtakiwa kwa muujibu wa sheria.

 Maiti ya muasi wa M23 ikinajisiwa na Askari wa Congo,baada ya kukamatwa, kuteswa hadi kufa katika mapigakano yanayoendelea maeneo ya Kivu na Goma nchini Congo.

Msemaji wa Katibu Mkuu wa UN Ban Ki-moon alisema kwamba, Umoja huo umeonyesha wasiwasi kuhusu taarifa ya kutokutendewa haki kwa wafungwa wa M23 na kunajisiwa kwa maiti ya wapiganaji wa M23 baada ya kukamatwa na vikosi vya silaha.

Alisema watuhumiwa wa M23 walifanyiwa vitendo vibaya na askari wa DRC mbele ya raia bila ya kuzingatia Sera ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu na kwamba watuhumiwa waliohusika katika matukio hayo watafanyiwa uchunguzi wa kina.

Wanajeshi wa DRC wakiinajisi maiiti ya muasi wa M23 baada ya kukamatwa na kupigwa hadi kufa mbele ya raia

Wanajeshi wa DRC wakiendeleza mateso makali kwa waasi wa kundi la M23 mpaka kifo kinapowafika wakiwa uraiani


Wanajeshi wa DRC wakiwa wamemfunga mpiganaji wa kundi la M23 nyuma ya gari na kumpitisha mitaani.


 Wanajeshi wa Congo wakimfunga askari wa kundi la M23 mbele ya raia baada ya kukamatwa

 
 Wanajeshi wa DRC wakimtembeza muasi wa kundi la M23 mitaani baada ya kukamatwa.

Credit: Habari mpya

MSHIRIKI WA TANZANIA ( NANDO ) AAMBUKIZWA MAGONJWA YA ZINAA BAADA YA KUFANYA MAPENZI NA MGHANA KATIKA JUMBA LA BIG BROTHER




 Akiongea  kwa  uchungu  na  huzuni  mbele  ya  Bimp,Nando ambaye  ni Mshiriki wa Tanzania  amemlaani  mshiriki wa  Ghana  kwa  kumwambukiza  GONJWA LA  ZINAA...

Nando  amelinyaka  gonjwa  la  zinaa  maarufu  kwa  jina  la  "Chlamydia"  na  hivi  sasa  yuko  katika  dozi.Gonjwa  hilo  amelinasa  baada  ya  kungonoka  na  SELLY   bila  KONDOMU.....  

Kwa  nini  Nando  hakutumia  Kondomu?

Akiongea  na  Bimp ambaye  ni  mshiriki  toka  Ethipia, Nando  amekaririwa  akidai  kuwa Selly  aligoma  kutumia  kondomu.


Kwa  kuwa  alikuwa  na  HAMU  na  tayari  stimu  zilikuwa  juu , Nando  anadai  kuwa  hakuwa  na  jinsi  zaidi  ya  kulikamua   TUNDA    bila  kulimenya....

Namkariri:
"You know I hate that bi*ch !
I'm f*cking frustrated cos that bi*ch *Selly* gave me STD! That's why my blood pressure was high yesterday!"


Pole Nando, kama  kauli  yako  ni  ya  kweli, nenda  kapime  na  ngoma.

Friday, July 19, 2013

PICHA ZA USHUHUDA WA WANACHAMA 5 WA CUF WAKIELEZA JINSI WALIVYOTESWA NA ASKARI HUKO MTWARA


 Baadhi ya Viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) kutoka (kulia) ni, Mwenyekiti wa Vijana Wilaya ya Mtwara Mjini, Ismaili Njalu. Katibu wa Wilaya ya Mtwara mjini, Said Kulanga na Mwenyekiti wa Wilaya ya Mtwara mjini, Salum Mohamed wakiwaonesha waandishi wa habari majelaha waliyoyapata baada ya kupigwa na Wanajeshi wa Wananchi (JWTZ) katika mkutano uliofanyika Makao Makuu ya Chama hicho Dar es Salaam.

--------------
CHAMA cha Wananchi (CUF) kinaandaa utaratibu wa kufungua kesi mahakamani dhidi ya ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanywa na Wanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kwa watendaji wa chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Naibu Mkurugenzi Mipango, Uchaguzi wa Bunge Shaweji Mketo,kwa niaba ya wanachama wenzake alisema, bado wanawasiliana na wanasheria, taasisi za haki za binadamu na mamlaka nyingine ili kupata mwongozo waweze kufungua kesi hiyo.

Mketo na wenzake watano, ni miongoni mwa watu walioonja joto ya mateso ya siku 28 kutoka kwa askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), ambao wameweka kambi Mtwara kudhibiti machafuko yanayotokana na madai ya kuzuia bomba la gesi asilia lisijengwe Dar es Salaam.

Mbali na Mketo wengine ni Mwenyekiti wa Vijana Mtwara mjini Salum Mohamed, Mwenyekiti wa Mtwara mjini Salum Mohamed, Mwenyekiti wa Wilaya Mtwara vijijini Ismail Jamal,Katibu wa Wilaya Mtwara mjini Said Kulaga na dereva wa CUF makao makuu Kashinde Juma.


Naibu Mkurugenzi Uchaguzi na Mipango wa CUF, Shaweji Mketo akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kuteswa kwa wanachama watano wa chama hicho na askari wa JWTZ mkoani Mtwara. 
 -----
Akisimulia mkasa huo uliompata yeye na wenzake alisema wakiwa njiani walikutana na gari mbili za jeshi kubwa na ndogo zikiwa njia panda ya newala na mtwara mjini,na kuwasimamisha huku walitokea askari wapatao 50 vichakani na kuanza kuwapiga huku wakiwasachi mifukoni.

“Askari wa JWTZ walikuwa 50 walitusachi na kuchukua fedha zangu shilingi 85,000 na nilipoanza kuzuia fedha hizo wasizichukue ndipo walipoanza kunipiga kweli wakanivua viatu vyangu nilivyowahi kununua nje ya nchi wakavichukua na mimi kuniachia vyao vya jeshi hivi hapa ,”alieleza Mketo.

Alisema walikuwa wakipigwa na fimbo, kumwagiwa maji yaliyokuwa yamewekwa barafu na pilipili jambo ambalo liliwafanya waendelee kupata maumivu makali sana.

Mketo alisema hata hivyo kuteswa kwao ni ishara kuwa Mtwara bado inanuka damu na hakuna usalama huku wananchi wengi wakihofiwa kufariki dunia.

Hata hivyo alisema wakati wakiendelea kuwatesa alisikika mwanajeshi mmoja akisema wao wapo pale kwa ajili ya kutekeleza amri ya Waziri Mkuu aliyoitoa Bungeni kwamba wananchi watakaokaidi amri ya serikali wanatakiwa kupigwa.

Kiongozi huyo ambaye aliongea kwa masikitiko makubwa huku akiwataka wenzake kuonesha majereha kwa wanahabari alisema kuwa licha ya kuwaambia wanajeshi waliokuwa wakiwatesa kuwa amefanyiwa upasuaji mkubwa wasimpige eneo hilo hawakujali kwani waliendelea kumchapa na bakora katika eneo la mshono hadi lilipogeuka rangi na kuwa nyeusi.

Alisema kiongozi mmoja ambaye ni Mwenyekiti wa Mtwara mjini Salum Mohamed aliambiwa azivute ndevu zake kwa kutumia mikono na alifanya hivyo hadi haapo zilipoanza kuvuja damu ndipo wakamwambia walichokuwa wanakihitaji.

Mketo alisema vitendo hivyo ni vya kinyama na kwamba haviwezi kuvumilika hivyo serikali inatakiwa kuviangalia utendaji kazi wa vyombo vya dola kwani ni kulinda raia na si kutesa.

Hata hivyo aliilaumu serikali kwa kuvifungia vyombo vya habari mkoani humo kwa kigezo cha kwamba vinawashawishi wananchi kuandamana jambo ambalo si kweli.
SOURCE:http://freebongo.blogspot.com/2013/07/picha-za-ushuhuda-wa-wanachama-5-wa-cuf.html

BASI LA NAJMUNISA LAPATA AJALI NA KUUA WANNE DODOMA



Basi la Najmunisa linalofanya safari zake kati ya mikoa ya Dar es Salaam na Mwanza limepata ajali katika eneo la Mbande mkoani Dodoma na kuua watu wanne huku likiacha majeruhi kadhaa.

Basi hilo lililokuwa linaelekea Mwanza lilipata ajali hiyo baada ya kupasuka tairi la mbele.

Mali za abiria inaelezwa zipo salama kutokana na uwepo wa Check Point ya polisi jirani na eneo la ajali.


MAJINA SABA YA WANAJESHI WA TANZANIA WALIO UAWA HUKO DARFUL SUDANI



Majina ya askari saba wa Tanzania waliokufa  kwenye shambulio la ghafla mjini Darfur yamepatikana.


Askari hao waliokufa ambao walikuwa kwenye vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa huko nchini Sudan ni Sajenti Shaibu Othuman, Koplo Oswald Chaula, Koplo Mohamed Juma, Koplo Mohamed Chikilizo, Pte. Rodney Ndunguru, Pte. Peter Werema na Pte. Fortunatus Msofe.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kwenye mtandao ni kwamba askari hao walikwenda kujaribu kumwokoa mwenzao (ambaye hakutajwa) ambaye alisemekana kutekwa na vikosi vya waasi nchini humo.
Wakati  wakijiandaa, ghafla walizingirwa na askari hao waasi na kisha kushambuliwa kwa risasi hadi kufa.
 
Haikufahamika hali ya askari huyo ambaye alidaiwa kutekwa kama bado yu hai ama ni miongoni mwa waliokufa.
Mungu azilaze roho za askari wetu mahali pema peponi, Amina
 
MPEKUZI

WALIOJIFANYA MASISTA WA KIKATOLIKI WAKAMATWA UWANJA WA NDEGE WAKISAFIRISHA MADAWA YA KULEVYA..!!

Wasafirishaji hao walisimamishwa wakati wakiwasili kwenye kituo maarufu cha mapumziko nchini Colombia, sababu polisi walifikiri kwamba mavazi yao hayakuwa yakionekana halisia.

Maofisa waligundua kwamba kila mwanamke kati yao alikuwa na zaidi ya kilo 4 za cocaine zikiwa zimefungwa katika miguu yake.
Wakiwaongezea fedheha katika mashitaka, wasafirishaji hao walipangwa mstari mbele ya waandishi wakiwa bado wamevalia mavazi yao ya kituko kuficha ukweli.
Wanawake hao watatu, wenye umri wa miaka 20, 32 na 37, walitua kwa ndege kwenye kisiwa hicho cha San Andres kutoka Bogota siku ya Jumamosi asubuhi.
Kapteni wa Polisi Oscar Davila alisema wanawake hao walionekana kama wamechanganyikiwa, na kuongeza kwamba mfumo wa tabia zao haukuonekana kuwa sahihi.
Pale masista hao bandia waliposimamishwa na kupekuliwa, walikutwa wakiwa na shehena kubwa ya cocaine ikiwa imefungwa katika miili yao.
Wote watatu waliangua kilio na kusisitiza kwamba walitumiwa tu kusafirisha dawa hizo sababu ya matatizo yao ya kifedha, alisema Davila.
Wanawake hao walikamatwa na kuswekwa rumande kwa mashitaka ya kusafirisha dawa za kulevya.
Dawa hizo zilikadiriwa kuwa na thamani ya Dola za Marekani 35,000 mtaani, kwa mujibu wa Kamishna wa Polisi wa mji huo, Jorge Gomez.
"Hawakuwa wafuasi halisi wa dini, hawakuwa masista," alisema. "Kinyume cha hilo, walikuwa wakitumia mwanya huo kwa ajili ya kazi hii.
"
San Andres, iliyoko Caribbean nje ya ufukwe wa Nicaragua, ni moja ya mahali maarufu kabisa nchini Colombia kwa ajili ya wakazi na watalii.
Hatahivyo, inatumika pia kama njia kuu ya kupitishia dawa za kulevya kwa ajili ya kusafirisha cocaine kati ya Colombia bara na Amerika ya Kati
Wanawake watatu wamekamatwa kwa madai ya kujaribu kusafirisha dawa za kulevya kupitia uwanja wa ndege wakiwa wamevalia kama masista.

WASICHANA WA SEKONDARI NI HATARI SANA KWA SASA TUWE MAKINI.


Habari wanajamii. 
Ngoja nami niwe mtoto kidogo kwa kusimulia na kutoka kasiri ka mambo ya kitoto.
 
Wiki iliyopita nilikuwa natoka zangu Mbeya kuelekea Dar es salaam kwa basi moja hivi.
 
Jirani yangu kwenye siti alikuwa amekaa "katoto" flani ka kike kama ka miaka 17-19. 

Yule mtoto alikuwa mstaarabu sana. Akaniamkia kisha akatulia. Gari lilipoondoka akaanza kunisemesha. Akaniuliza ninapokoka, niendako, origin yangu na maswali kibao ya kizushi. Akajitambulisha kuwa yeye ni mwanafunzi wa kidato cha nne alikuwa anaumwa akarudi nyumbani anaelekea shuleni(akataja jina la shule).
 

Njiani nikawa nikinunua maji namnunulia, nikinunua kitu chochote naye namnunulia. Safari ikaendelea.
 
Tulipofika Morogoro akaniomba nimwazime simu yangu afanye mawasiliano kwani yake haina credit. Bila hiyana nikampatia akaitumia akanirejeshea.
 
Kwa kweli nilimchukulia kama mdogo wangu tu hadi tunafika.
 
Kituko kikaanza usiku kama saa 6:30 usiku hivi, nikiwa nimelala ikaingia message kwenye simu yangu "mimi yule dada tuliyesafiri wote leo, umefika salama nyumbani? Usiku mwema".
 
Kumbe katoto ka watu kalichukua namba yangu bila mimi kujua. Basi mtoto akatuma tena asubuhi kama saa 12:00 "vipi umeoa? Unaonekana mstaarabu, nimemiss sana jinsi ulivyo mpole, asubuhi njema".
 
Sikujibu chochote. Mchana akatuma message tena, jioni tena nami bila kujibu. Usiku wa siku ya pili kama saa tano usiku akapiga tena simu na kunitamkia anapenda tukutane aniambie jinsi gani alivyonipenda kimapenzi. Kisha akakata simu nami sikupiga.
 
Jioni nikamtumia message nikimpa ushauri na kumnasihi kuwa ajitahidi katika masomo yake na aache kufikiria kuhusu mapenzi. 

Akakoma kupiga na kutuma tena message ila nikawa nimejifunza kitu kwa zile message alizokuwa anatuma. Utadhani kaandikiwa jinsi zilivyojaa maneno ya kimahaba ya kukata na shoka. Na jinsi message zilivyo huwezi amini kama kaandika mtoto wa sekondari.
 
Kama hali ndo ilivyo kwa mabinti zetu wanaosoma basi kazi tunayo wazazi na hatutavuna kitu kwa mabinti zetu wa aina hii.



Source:Jamii Forums

MASHABIKI WAMPONDA WEMA SEPETU BAADA YA KUYAANIKA MATITI YAKE MTANDAONI


 
“Did I miss a spot…? I dunno,” ni maneno ya Wema kwenye picha aliyoiweka leo katika mtandao wa Instagram. 


Hata hivyo mashabiki wengi wamemshambulia mrembo huyo kwa kile wanachohisi hakupaswa kuiweka katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani. 
 
Haya ni baadhi ya maoni:  

nanchesca5 Girl, I’m not trying to fix you,But this is the holy month.Keep it calm.It won’t hurt.

princesswawiey R u sure…ur a muslim? 1

khadijaumumustafa Wewe ni binti wa aina gani usieogopa mwezi mtukufu wa ramadhan ama kweli umeshindikana kabisa hata nachanguduwa uheshim huu mwezi ila wewe ni zaidi SubhanaLLAH.


sweettuma Punguza picha za hivyo vastaraa mwez ukiisha vaa utakavo jst jistir kwamda mfup hailet picha nzur .
 

mamu30 mhuu wema wangu ulivyokuwa na damu ya kunguni kesho tutaikuta hii picha kwenye mablog itakuwa gumzo ooh wema haheshimu mwezi mtukufu kumbe picha ya sikunyingi wao watadhani ndio unavyovaa hivi wakati wa mfungo lol
 

hazole Mnaolalamika mwezi mtukufu just unfollow her thn mwezi ukiisha rudini #GivePeopleSpaceToBreath


husnaomary Muislam mzma hata haushim mwez mtukuf wema….emu muogope Allah….picha gn hii na ramadhan hii….innallillah…nakupenda wema bt kumbuka kuwa huu mwez mtukuf…..heshma ishke mkondo wake…dis z Dunia baby…ickushikilie akili yako….nakupenda ndomana nakwambia.


hapnicole Mwenyezi Mungu anasema uwe msafi siku zote nd sio mwezi mmoja tu huo ni unafiki so bora yeye kuliko wewe unae mjaribu yeye kwa mwezi mmoja tu ni mtazamo


sele_yg Unanitega mwezi mtukufu..


noranuru what..ndo kuwatamanisha watu au ,mmh shoga namwezi huu wote..huchoki?
source:Mpekuzi huru

HABARI ILIYOANDIKWA NA GAZETI LA "TANZANIA DAIMA" KUHUSU UDINI WA LIPUMBA YAWACHEFUA CUF


Habari iliyoandikwa na Gazeti la Tanzania Daima ikimhusisha Prof. Lipumba na udini  imewachefua  CUF  na  kuwafanya  watoe  waraka mkali wakiita Serikali kulichukulia hatua gazeti la Tanzania Daima kwa uchochezi wa kidini..
Chama    hicho  kimedai kuwa  Lengo la Gazeti la Tanzania Daima na Mwandishi wake ni kupandisha hasira za Waislam
--------------------------------------------------------------------
HUU  NI  WARAKA  WA  CUF:
CUF TUNASHANGAZWA NA JINSI SERIKALI INAVYOSHINDWA KULICHUKULIA HATUA GAZETI LA TANZANIA DAIMA KWA KUENDELEZA UCHOCHEZI WA KIDINI.

CUF-Chama cha Wananchi, kinasikitishwa sana na kitendo cha uchochezi wa Kidini unaofanywa na Gazeti la Tanzania Daima chini ya Muandishi George Maziku, kufuatia habari iliondikwa leo Tarehe 18/07/2013 toleo na 3149 . Aina hii ya uchochezi na Chuki ya Kidini anayoiendeleza bw, Maziku chini ya usimamizi wa Mmiliki wa Gazeti la Tanzania Daima na Mhariri wake, kwa maslahi ya Kisiasa tu, yatatupeleka mahala pabaya sana kama Taifa.

CUF-Chama cha Chama Wananchi tunashangazwa na tuna hoji juu ya lengo na Dhamira ya Gazeti la Tanzania Daima na Muandishi wake nini juu ya muendelezo wa habari wanayoitoa kwa muda wa miezi miwili sasa ? Habari hii ina lenga nini ? Kwamba Viongozi wa Kisiasa wanaotokana na Dini ya Kiislam hapaswi kujumuika na Waislam wenzao kwenye Nyumba za Ibada ? Au waislam hawapaswi kujadili Maendeleo ya Taifa lao ?

CUF-Chama cha Wananchi tunaona Lengo la Gazeti la Tanzania Daima na Muandishi wake ni kupandisha hasira za Waislam kwa mtazamo wa Ubaguzi wa Kidini kupitia tasnia ya Habari na hivyo kuleta machafuko yasiokuwa ya lazima.

Hata hivyo ikiwa lengo ni kuondosha Dalili za Udini kwenye mambo ya Siasa, hivi Gazeti la Tanzania Daima na Muandishi wake hawakuona Waraka wa Uchaguzi wa Mwaka 2010 uliotolewa na Kanisa Katoliki na kupewa jina la IIani ya Uchaguzi wa Kanisa Katoliki ? Waraka ambao uliwataka Wakristo kuichagua Chadema na wagombea wake, Sio hivyo tu Waraka huo ulikwenda mbali zaidi na kuwatahadharisha Wakristo wasichague CUF na CCM na kuvifananisha Vyama vya CUF na CCM ni sawa na Chui waliovaa Ngozi ya Kondoo kwa Kanisa.

Waraka huo ulipingwa vikali sana na Mzee Kingunge Ngombale Mwiru. Gazeti la Tanzania Daima na Muandishi wake walikuwa wapi ? Mbona hatukuona waandike KANISA LA CHOCHEA UDINI ? Kama hiyo haitoshi, hivi Gazeti la Tanzania Daima na Muandishi wake mbona hawakumkemea wala kuandika kuhusu Askofu Kakobe alipokua anampigia debe Mgombea wa Urais kupitia Chadema 2010 tendo ambalo lilikuwa linaonyeshwa wazi wazi kupitia Star Tv.

Kama hiyo haitoshi katika uchaguzi mdogo wa madiwani uliofanyika jijini Arusha na Chadema kushinda wafuasi na viongozi wake kutuma ujumbe mfupi wa simu (SMS) kuwa YESU AMESHINDA hilo nalo hukuliona?

Kama hiyo pia haitoshi ? Mwaka huu Mery Nagu amekwenda kusali Kanisani na kuwataka Wakristo wajitokeze kwa wingi kutoa maoni yao kuhusu katiba mpya na kuwataka waumini hao wapinge mambo yote yanayotakiwa na kikundi kidogo cha baadhi ya watu kwa maslahi ya Kanisa, je huu haukuwa UDINI ? Lowasa kila kukicha yupo Makanisani na Misikiti na anatoa Fedha anatoa je hilo sio tatizo ?

Kwa mkusanyiko wa hoja zote hizi , CUF –Chama cha Wanainchi kinashindwa kuelewa kwanini Serikali haioni hatari inayofanywa na Gazeti la Tanzania Daima na Muandishi kwa tendo hili la Uchochezi wa Kidini ? Ikiwa Serikali iliweza kuzifungia Radio Imani na Radio Maria zote zikiwa zinarusha matangazo yake kwa Malengo ya Kuendeleza Dini zao, inashindwaje kulitazama Gazeti hili la Tanzania Daima ? Hivi Serikali inasubiri nini ? mpaka hao Waislam wanaotumiwa kuwa wadini waje juu na kuleta vurugu ? Ni busara kwa Serikali kulitazama jambo hili kabla halijalet madhara.

CUF-Chama cha Wananchi kinaishauri Serikali kulitazama kwa makini jambo hili, kabla halijaleta madhara, uandishi wa aina hii ndio uliosababisha Mauaji ya Kimbali. Uandishi wa Uchochezi unaolenga kuligawa Taifa kwa misingi ya Ukabila au Udini ni uandishi hatari sana kwa Taifa letu.

Bahati mbaya Tanzania Daima hawajui au wamesahau kwamba kwa chuki ya Kidini wanayojitahitahidi kuipandikiza ndani ya Taifa letu kwa nguvu ya Tasnia ya Habari, haitawaacha SALAMA wao kama Gazeti wala Muandishi wa Habari hiyo ya Uchochezi na wanapaswa kutambua kwamba kwa kufanya hivyo tu, basi wanainunua hatari ya Taifa letu kwa gharama kubwa.

Malengo ya Kisiasa yasije kulisambaratisha Taifa letu eti kwa sababu tu Chadema ichukue Nchi. Mnaweza kufikia Lengo la kuchukua Nchi kwa Mtazamo na Mkakati huo wa Kidini, kama ambavyo mnaendlea kufanya, lakini mjue kwamba mtachukua Nchi isokuwa salama. Maana mtakuwa mmeigawa Nchi kwa Matabaka ya Udini.

Kama kweli wewe ni mwandishi mahiri na mpenda amani katika nchi, tafadhali soma kitabu cha KANISA KATOLIKI NA SIASA YA TANZANIA BARA KUANZIA MWAKA 1953 HADI 1985 kilichoandikwa na Dr. John C. Sivalon na uje na uchambuzi wa dini uliomo katika kitabu hicho.

CUF- Chama cha Wananchi kinalitaka Gazeti la Tanzania Daima , kuanzia Mmiliki wake, Mhariri wake na Muandishi wa Habari hizi, ambae mara huandika kwa mtindo wa Makala , mara huzipa uzito mkubwa kadri anavyoona inafaa kwa utashi wa Kisiasa au Udini wake, kujitazama upya juu ya hili wanalolitengeneza kama litaiweka Nchi yetu katika eneo salama.

Mwisho CUF-Chama cha Wananchi kinaitaka Serikali kuchukua hatua juu ya Uchochozi huu.

Imetolewa na
Abdul Kambaya, Naibu Mkurugenzi wa Habari, Haki za Bainaadam na Mahusiano ya Umma
0719 566 567

WAREMBO WANAONA DILI KUPIGA PICHA ZA UCHI.''MISS UTALII TENA MTOTO WA SHEKH APIGA PICHA ZA UTUPU.

WakatI maelfu ha waumini wa dini la Kiislam duniani wakiwa ndani ya mfungo mtukufu huku wengi wao wakitumia kipindi hiki kupunguza maovu yao kwa mola kwa kufanya ibada,Hali imekuwa tofauti kwa aliyekuwa mshiriki wa shindano la kumtafuta Miss Utalii Taifa Faithiya Madoud amepiga picha chafu za kujidhalilisha pamoja na kumdhalilisha mwanamke wa kitanzania.

Picha hizo chafu kwa mara ya kwanza zilinaswa na Xdeejayz toka kwa chanzo chetu cha habari ambapo inadaiwa msichana huyo ambae ameanza kuonja ladha ya ustaa kufuatia kufanya vyema kwenye filamu za Mrembo wa Facebook na Nimpende Nani ambapo filamu zote hizo amecheza kama staa.

Habari za uhakika toka kwa chanzo chetu klichofikisha cd nzima ya picha hizo mezani kwa mtandao huu hatari kwa kunasa matukio magumu kilisema kuwa msichana huyo ambae mapema mwaka huu alishiriki shindano hilo la Miss Utalii Taifa yaliyofanyika Mkoani Tanga. Lakini kwa bahati mbaya hakufanikiwa kushika nafasi za chini lakini alichaguliwa kuwa balozi wa Hotel zote za Kitalii nchini Tanzania pamoja na Kule Zanzibar

Hata hivyo habari zaidi ziliendelea kusema kuwa bint huyo kabla ya kuingia kwenye umiss alikuwa ni msanii maigizo na ametamba sana kwenye filamu hizo kiasi cha kujizolea umaarufu mkubwa nchini.

Aicha chanzo hicho kilisema picha hizo ambazo nyingine ni mbaya sana ambapo blog hii imeshindwa kuzitundika zote kwa kuzingatia maadili kwa wasomaji wetu lakini ilidaiwa kuwa picha hizo alikuwa anapigwa na mwanamke mwenzake na ilionekana walikuwa Hotel na haikufahamika walifika kufata nini kwenye nyumba hiyo ya wageni.

Baada ya kupata picha hizo xdeejayz ilivuta waya moja kwa moja hadi kwa staa huyo mtarajiwa na kwa bahati nzuri simu yake ilipokelewa na yeye mwenyewe na haya ni mahojiano kati ya mwandishi wa Xdeejayz na mrembo huyo " Xdeejayz habari yako dada bila shaka naongea na Fathiya? " Ndiyo habari yako nani mwenzangu?"
Xdeejayz" 
Hapa ni ofisi za DTV kupitia blog ya Xdeejayz" Fathiya" Ndiyo nikusaidieni nini DTV?" 
"Xdeejayz ahsante sana Fathiya ofisi yetu imenasa picha zako za utupu hivyo tulitaka ufike ofisini kwetu ili kuzitambua kama inawezekana au thubitisha kama uliwahi kupiga picha na namna hiyo"
"Fathiya umesema wewe nani?
"Xdeejayz ofisi za DTV kupitia blog ya xdeejayz"
"Fathiya sasa kwani nani kawaletea hizo picha? mimi hizo picha nilipiga kwa matumizi yangu binafsi sasa nyie inawahusu nini lakini mbona waandishi wa Tanzania mnapenda kufatilia maisha ya watu? Sitaki kabisa mtoe picha zangu kwenye Tv yenu au gazeti la sivyo nitakufa na mtu sipendi kabisa ****** zenu" Alimalizia na tusi Fathiya kisha akaata simu.

Hata hivyo juhusi za kumtafuta Rais wa Miss Utalii Tanzania Gedion Chipungahelo hazikufanikiwa baadaya namba yake ya simu kushindwa kupokelewa.
XDEEJAYZ ina laani vikari tabia za mabint wenye tabia chafu kama hizi za kujipiga picha za kujidhalilisha bila sababu za msingi.



 


  Fathiya hapa ameamua kuvua kabisa ili kubaki na chupi peke yake.



                                                                      chanzo : xdeejayz blog