Saturday, August 31, 2013

ANGALIA PICHA ZA KAHABA APEWA KICHAPO BAADA YA KUNASWA AKIJIUZA JIRANI NA MSIKITI


Kahaba  mmoja   alijikuta akiambulia kichapo kikali toka kwa vijana wa kiislamu baada ya kunaswa akijiuza karibu na msikiti wao..


Wakati mwanamke huyo akicharazwa bakora, nguo ya ndani ilimvuka huku akipiga kelele kuwa hatarudia kufanya hivyo na kama akirudia basi akatwe kichwa.


Kutokana na kukerwa na vitendo hivyo, vijana hao wanaofanya ibada katika msikiti huo, waliamua  kuwatafuta vijana wa ulinzi shirikishi na kuwapa kazi hiyo ya kuwakamata na kuwacharaza bakora kisha kuwapeleka katika kituo hicho cha polisi.


“Tumeamua kuwakamata na kuwacharaza bakora, hawana ustaarabu wala busara hawa, wanakojoa na kutupa kondomu  hovyo, “ alisikika mmoja wa vijana hao.
Mmoja wa vijana hao aliyekuwa akisimamia kwa karibu zoezi hilo, aliwaambia waandishi wetu kuwa wameamua kufanya hivyo na litakuwa zoezi endelevu kutokana na wanawake hao kutokuwa wasikivu kwani kila wanapoambiwa juu ya kukaa mbali na nyumba hiyo ya ibada hawasikii.

Alisema kuwa siku moja wanawake hao walimtoa udhu muumini mmoja ambaye alikuwa akienda kuswali alfajiri baada ya kumshika na kusababisha akose kuhudhuria swala siku hiyo.




Hata hivyo, wakati mahojiano yanaendelea, mmoja wa askari waliokuwa zamu aliamuru mwanamke huyo aingizwe lokapu kusubiri kesho yake aunganishwe na wenzake kisha wapelekwe mahakamani.

Habari zilizotufikia  ni kwamba baada ya kufikishwa mahakamani na kukutwa na kosa la uzururaji, wakahukumiwa kifungo cha miezi sita jela au faini ya shilingi elfu hamsini ambapo walilipa kiasi hicho na bado wanaendelea na biashara hiyo maeneo hayo.



GPL 

PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa jana

PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana
  • PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana 1
  • PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana 2
  • PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana 3
  • PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana 4
  • PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana 5
  • PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana 6
  • PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana 7
  • PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana 8
  • PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana 9
  • PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana 10
  • PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana 11
  • PICHA: Uzinduzi wa filamu ya foolish Age ya mwanadada Elizabeth Michael-LULU ulivyokuwa  jana 12
Hatimaye tukio la uzinduzi wa filamu ya ya mwanadada Elizabeth Michael lulu umefanyika jana katika ukumbi wa mlimani City kwa kishindo kikubwa kwani ulijaza watu wengi kupita kawaida na kuacha historia katika soko la filamu Tanzania.
Tazama baadhi ya picha za tukio hilo lilivyokuwa

RAIS KIKWETE AMUOMBA RAIS WA UGANDA AONGEE NA KAGAME ILI KUMALIZA UGOMVI ULIOPO


RAIS Jakaya Kikwete, amewasiliana na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, ili azungumze na Rais wa Rwanda, Paul Kagame kwa nia ya kumaliza mvutano wa maneno kati yao kwa busara.
 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema hayo jana bungeni, alipokuwa akijibu swali la Kiongozi wa Upinzani bungeni, Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe (Chadema).
 
“Tunataka suala hili limalizike kwa njia ya busara, ili watu waendelee kuchapa kazi, ninaamini busara zitatumika kumaliza tatizo hilo,” alisema.

Akiuliza swali katika kipindi cha maswali ya Papo kwa Hapo kwa Waziri Mkuu jana, Mbowe alitaka kujua kauli ya Serikali na mikakati iliyopo kupata suluhu katika mvutano wa maneno uliojitokeza kati ya Rais Kikwete na Rais Kagame.
 
Pia Mbowe alitaka Serikali kuunda jopo la ushawishi wa kimataifa, kutokana na Rwanda kuonekana kushawishi nchi za Uganda na Kenya, jambo ambalo linaashiria kuitenga Tanzania katika shughuli mbalimbali za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
 
Kwa mujibu wa Mbowe, kitendo cha marais wa Kenya, Uganda na Rwanda kukutana katika mikakati ya kuanza kutumia bandari ya Mombasa ambayo ingekuwa ya nchi za Afrika Mashariki, ni dalili kuwa Tanzania imeanza kutengwa.
 
Mbowe alisema pamoja na kuanza kutengwa kwa Tanzania katika shughuli za Afrika Mashariki pia kumekuwa na mgogoro uliozuka hivi karibuni wa Bunge la Afrika Mashariki, kutaka vikao vya Bunge hilo vifanyike kwa kupokezana katika nchi wanachama, tofauti na ilivyokuwa awali, ambapo vikao hivyo vilifanyika Arusha.
 
Hata hivyo, Pinda katika jibu lake, alisisitiza kuwa hakuna sababu ya Serikali kuunda jopo la kutafuta ushawishi wa suluhu na Rwanda kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), kwa kuwa hakuna sababu za kufanya hivyo.
 
Hakuna uhasama Akifafanua, Pinda alisema Serikali haina sababu ya kujenga uhasama na Rwanda, kwa kuwa nafasi ya Tanzania na mchango wake katika nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu na Afrika unajulikana.

Alisisitiza, kuwa ushauri aliotoa Rais Kikwete wa kutaka Rwanda kukaa meza moja na waasi, ulikuwa wa busara na haukuwa na tatizo lolote.

Kutokana na msingi huo, alifafanua kwamba ndiyo maana Tanzania haiangalii mvutano huo wa maneno kama tatizo, ingawa Serikali haitapuuza suala hilo linaloonesha kuwepo kwa dalili ya kutoelewana.
 
“Ukilitazama suala hili huwezi kuamini kama kweli kauli ya Rais Kikwete ingeleta haya, nadhani wenzetu wanalitazama kwa namna tofauti na sisi tunavyolitazama,” alisema.
 
Pinda alirejea kiini cha mtafaruku huo, kuwa ni ushauri wa Rais Kikwete kwa nchi ya Rwanda kukaa meza moja na waasi, ili kuacha mapigano kwa maslahi ya wananchi wa Rwanda.
 
Alisema kauli hiyo iliyotolewa na Rais Kikwete katika mkutano wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika Ethiopia, ilikuwa na nia njema kwa maslahi ya Rwanda, lakini imechukuliwa tofauti nje ya mkutano huo.
 

Propaganda za biashara
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tizeba, alisema kauli zinazotolewa kuwa mizigo ya Rwanda haitapitishwa kwenye bandari ya Dar es Salaam, ni propaganda za kibiashara kutoka nchi washindani.
 
Hata hivyo, Dk Tizeba hakuwa tayari kubainisha ni nchi ipi inahusika zaidi kutoa propaganda hizo ingawa aligusia kwamba ni nchi zenye bandari.
 
Alisema baada ya kukutana na wafanyabiashara wa Rwanda na viongozi wa Serikali ya nchi hiyo, wamebaini kuwa hakuna upande uliozuia mizigo kupita Tanzania.
 
“Huku wanasema kuna maelekezo kwamba wafanyabiashara wa Rwanda wasipitishe mizigo Tanzania, lakini kwa Rwanda wao wanasema Tanzania imezuia mizigo ya Rwanda kupita Tanzania … tumebaini kuwa kauli hizi hazikuwa na ukweli,” alisema.
 
Alisema wafanyabiashara wa Rwanda wamesema kama Tanzania wanataka Rwanda ipitishe mizigo mingi, ifanye marekebisho kadhaa, ikiwemo kukabiliana na matatizo kama lililowahi kutokea la kupotea kwa kontena mbili za dhahabu na mbolea, kuangalia tozo za kusafirisha magari yasiyosajiliwa Tanzania na kupunguza wingi wa mizani ambao wanadai unachelewesha usafirishaji.
 
Pia Tizeba alisema walilalamikia udokozi wa vitu vidogo kwenye magari bandarini, jambo ambalo limefanyiwa kazi na hali hiyo haipo tena, kwani baadhi ya magari vifaa vyao vilikuwa vikiibwa maeneo mengine kabla ya kufika Dar es Salaam.

“Kuna mambo mengi yanafanyiwa kazi ikiwamo kuwa na treni mbili za mizigo hadi Isaka, ambazo zitasafirisha mizigo ya Rwanda, Kongo na Burundi, na pia kuweka ofisa wa bandari Kigali, ambaye atakuwa akishughulikia matatizo na kuanzisha mizani ambayo itapima gari likiwa linatembea na kuwa na mizani maeneo matatu,” alisema.
 
Kuhusu hatua ya Rais Kagame kuzindua mpango wa nchi yake kutumia bandari ya Mombasa, Tizeba alisema nchi inaweza kuwa na njia nyingi za kupitishia mizigo, na kubainisha kuwa bado Tanzania ndilo eneo pekee zuri kwa kusafirisha mizigo kwa nchi zisizo na bandari.

HABARILEO AGOSTI 30, 2013

WABUNGE WATAKA MBIO ZA MWENGE WA UHURU ZIFUTWE



MBIO za Mwenge wa Uhuru nusura ziahirishe shughuli za Bunge baada ya baadhi ya wabunge kutaka zifutwe na hoja hiyo ijadiliwe bungeni.
 
Hata hivyo, suala hilo liligeuka shubiri kwa Waziri wa Nchi, Ofisa ya Rais (Utawala Bora), George Mkuchika, kuzomewa na kurushiwa maneno ya kejeli alipojaribu kuzitetea mbio hizo.
 
Chanzo cha mzozo huo kilitokana na maswali ya mbunge wa Musoma Mjini, Vicent Nyerere (CHADEMA), aliyeihoji serikali kama kuna uwezekano wa kutoukimbiza Mwenge katika maeneo ya watu wasiouhitaji.
 
Nyerere alisema watu wa wilaya ya Musoma, mkoani Mara, hawautaki Mwenge huo kwa sababu unachochea uhasama, chuki na upotevu wa rasilimali.
 
“Wakati wa mbio za Mwenge Musoma Mjini walilazimisha kuchukua magari ya halmashauri likiwemo la wagonjwa... huduma za afya zilisimama na hivyo kuleta chuki badala ya mwanga,” alidai.
 
Nyerere pia alitaka kujua nini faida za mbio hizo, bajeti yake ni kiasi gani kwa mwaka na matumizi yake kama yanafanyiwa ukaguzi.
 
Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Amos Makalla alisema serikali haina taarifa kama Musoma yalitokea mambo hayo wakati wa mbio hizo.
 
Alisema kuwa Mwenge hautaachwa kukimbizwa katika maeneo fulani bali utaendelea nchi nzima na wanaotaka kuchangia waendelee kufanya hivyo bila kusita.
 
Makalla alisema mbio hizo zilianzishwa kwa falsafa ya kuhamasisha ukombozi wa taifa la Tanganyika na bara zima la Afrika kama alivyosema Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere.
 
“Mbio za Mwenge wa Uhuru zimeendelea kuwahamasisha wananchi nchini kubuni, kuchangia na kutekeleza miradi ya maendeleo.
 
“Mwaka 2012/2013 jumla ya miradi 273 yenye thamani ya sh bilioni 15.8 ilizinduliwa na mingine kuwekewa jiwe la msingi nchini kote,” alisema.

Aliongeza kuwa kupitia mbio hizo, wananchi walichangisha sh bilioni 11.5 kwa hiari kwa ajili ya kukamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo katika wilaya zao. 


Makalla alisema serikali imetenga sh milioni 450 kwa mwaka wa fedha 2013/2014 kwa ajili ya shughuli za Mwenge wa Uhuru.
 
Majibu hayo yaliwanyanyua wabunge wote wa upinzani lakini Naibu Spika Job Ndugai alimpa nafasi mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari (CHADEMA) aliyehoji Mwenge huo unamulika wapi.
 
Alidai kuwa licha ya kuendelea kukimbizwa kila mwaka rushwa, dawa za kulevya, ongezeko la maambukizo ya ukimwi, ubadhirifu vimeendela kuongezeka.
 
Baada ya majibu ya Makalla kutotosheleza, Ndugai alimpa nafasi mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ally Keissy (CCM), aliyesema mbio hizo hazina faida kwa wananchi na zinatumia fedha nyingi.
 
Alisema kila zinapopita mbio hizo, shughuli za kiserikali, kijamii husimama kwa muda usiopungua siku tatu.

“Jamani tuwe wakweli Mwenge huu hauna faida, kila unapopita watendaji wote wa serikali au halmashauri hukimbia ofisi zao, sasa wananchi wanahangaika,” alisema.
 
Baada ya mbunge huyo kutoa kauli ile, Naibu Spika alisema “Nimekupa nafasi ya kuuliza swali nikidhani utampatia ahueni kumbe ndiyo umeharibu kabisa.”

Akijibu maswali hayo, Makalla alikiri kusimama kwa shughuli hizo unapokuwepo Mwenge lakini faida zake ni kubwa kuliko hasara.
 
Ufafanuzi wa Makalla ulifuatiwa na majibu ya nyongeza kutoka kwa Mkuchika akisema Mwenge huo uliwashwa na kuwekwa Mlima Kilimanjaro ili uwasaidie wananchi wa Tanganyika kupata nuru palipokuwa na giza, kuheshimiwa na kukombolewa.
 
Alisema anamshangaa Nyerere (Vicent) kuukataa Mwenge wakati babu yake ndiye aliyeuanzisha kwa lengo la kuwakomboa Watanzania; kwamba baadhi ya wabunge hawana uelewa juu ya umuhimu wa mbizo hizo ndiyo maana wanataka ufutwe.
 
Ufafanuzi huo uliwafanya wabunge waanze kumzomea huku wengine wakisikika kuwa ‘ukimwi’ kila unapokesha.
 
Mkuchika alijibu mapigo akisema: “Watu wanazomea wakati mimi natoa elimu; najua hiyo ndio tabia yao kuzomea, hivyo hawanipi shida.”
 
Mzozo huo ulizidi kuwa mkubwa kwani baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu walijitokeza wabunge watatu kuomba muongozo huku mbunge mmoja akitoa hoja ya kuahirishwa kwa shughuli za Bunge.

Moses Machali mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR), alisimama na kutoa hoja kwa Naibu Spika kwa kuomba kuahirishwa kwa shughuli za Bunge ili kuruhusu kujadiliwa kwa jambo hilo la Mbio za Mwenge.

Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), alisema suala la Mwenge muktadha wake mzima sio mbaya lakini kumekuwa na malalamiko na manung’uniko muda mrefu.

Alitaka ifanywe tathmini ya kina kujua faida na hasara zake ili kwenye upungufu kufanyiwe maboresho.
 
Mbunge wa Simanjiro Ole Sendeka aliomba muongozo akidai Mwenge huo ambao ni alama na tunu ya taifa kuleta tumaini pale ambapo hapana matumaini kwa wale wanaojua historia.

Alisema kwa kuwa kuna uelewa mdogo kwa Watanzania juu ya jambo hilo huku wengine wakijipenyeza na kuingia ni bora ofisi ya Bunge ikatoa elimu.
 
Naibu Spika alitoa nafasi kwa Mkuchika kutoa maelezo kwa yale ambayo yamemgusa na kuongeza kuwa kuhusiana na miongozo mingine ataitolea taarifa baadaye.
 
Mkuchika alisema hakuwa na nia mbaya na badala yake alikuwa ananukuu kauli ya Mwalimu Nyerere aliyoisema kabla Tanganyika na Zanzibar hazijaungana.

-Tanzania daima

IGP SAID MWEMA AWABADILI MAKAMANDA MTWARA NA VIWANJA VYA NDEGE

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema.
 
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema amefanya mabadiliko kwa baadhi ya makamanda wa Mikoa na Vikosi.
Mabadiliko hayo ni pamoja na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara  Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Linus Sinzumwa ambaye amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi Idara ya Upelelezi  na nafasi yake inachukuliwa na Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Zelothe Stephen  kutoka Makao Makuu ya Polisi.
Aidha, aliyekuwa Kamanda wa Polisi  Viwanda vya ndege Kamishina Msaidizi (ACP) Deusdedit  Kato amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi  na nafasi hiyo inachukuliwa na Kamishina  Msaidizi wa Polisi (ACP) Selemani Hamisi kutoka Makao Makuu Idara ya Upelelezi.
Wengine ni Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Hamad Hamad anayeenda kuwa Mkuu wa Upelelezi Viwanja vya ndege ambapo hapo awali nafasi hiyo ilikuwa inashikiliwa na David Mwafwimbo aliyehamishiwa mkoani Lindi kuwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Lindi (OCD).
Uhamisho huo ni wa kawaida kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya Jeshi la Polisi.
Imetolewa na:
Advera Senso-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

Friday, August 30, 2013

KAMA UNAPUNGUZA UNENE, USILE VYAKULA HIVI

Unene uliokithiri ni tatizo linalowasumbua watu wengi duniani hivi sasa. Ukiacha unene unaotokana na kurithi vinasaba vya unene katika familia, asilmia kubwa ya unene uliokithiri unatokana na staili ya maisha anayoishi mtu na mwenendo wa ulaji wake.
Kuna njia mbalimbali za kupunguza unene, lakini wakati wa kufanya njia hizo, ni vizuri kujua aina ya vyakula ambavyo huchangia kuongezeka kwa uzito ambavyo mtu anatakiwa kuviepuka. Itakuwa ni kupoteza muda na kujitesa iwapo utakuwa na bidii ya kupunguza uzito kwa kufanya mazoezi huku ukila vyakula vinavyochangia kuongeza uzito.
Vifuatavyo ni baadhi ya vyakula maarufu ambavyo mtu anapaswa kuviepuka kuvila kabisa kwani huongeza uzito wa mwili:

SODA
Usinywe soda ya aina yoyote ikiwemo soda zinazodaiwa  kuwa hazina sukari (diet soda). Badala yake kila mara usikiapo kiu ya maji au hamu ya kunywa soda, pendelea kunywa maji safi na salama kwa afya yako. Maji husaidia kuondoa mafuta na sumu mwilini.
POMBE
Usinywe pombe hata kwa kiasi kidogo iwapo upo kwenye zoezi la kupunguza uzito wa mwili. Kimsingi pombe nayo ina kiwango cha sukari ambacho huchangia ongezeko la unene wa mwili kirahisi.

‘SNACKS’
Jiepushe na ulaji wa vitafunwa ‘snacks’ vilivyotengenezwa kwa kuchanganywa na mafuta, sukari au chumvi. Mfano wa vitafunwa hivyo ni pamoja na chips, popkoni zenye sukari, biskuti, keki, askrimu, chokoleti, n.k.
Kwa kawaida vitafunwa hivi huwa havishibishi bali hutia hamu ya kula, hivyo utajikuta umekula kiasi kingi cha sukari au chumvi ambacho kinaenda kuongeza uzito mwilini bila kujijua.
Vitafunwa hivi huwa na tabia moja ya kumfanya anayependa kuvila aendelee kupenda kuvila kila siku bila kukosa, hivyo kumfanya awe ‘mlevi’ (addicted) wa vyakula hivyo. Kwa staili hii ya ulaji, ukifanya mazoezi ya kupunguza uzito huku unaendelea na ulaji huu, huwezi kupungua hata kidogo, zaidi utashangaa kuona unanenepa zaidi badala ya kupungua.

VYAKULA VILIVYOKOBOLEWA
Epuke ulaji wa vyakula vilivyopikwa kutokana na unga uliokobolewa, iwe unga wa mahindi, ngano, n.k., kwani vyakula vya namna hii vilivyoondolewa virutubisho vyake muhimu huchangia kulifanya zoezi la kupunguza uzito kuwa gumu, kwa sababu navyo vinachangia unene. Lakini ukila vile ambavyo havijakobolewa (whole grain), matokeo yake huwa mazuri, kwani husaidia kupunguza unene.
Listi ya vyakula unavyotakiwa kuviepuka kabisa wakati wa kufanya zoezi la kupunguza unene ni ndefu, lakini kwa ufupi ni pamoja na vyakula vyote vya kukaanga kwa mafuta, vyakula vya kwenye makopo, mkate mweupe, chips za viazi vitamu vilivyopikwa kwa mafuta na vingine vingi.
Badala yake pendelea kula matunda ya aina mbalimbali na mboga za majani kwa wingi na vyakula vya kubanika au kuoka badala kukaanga kwa mafuta na kula vyakula asilia. Suala la kunywa maji kwa wingi kila mara na kila siku linarahisisha kwa asilimia nyingi zoezi la kupunguza uzito.

TAZAMA PICHA 50 ZA UZINDUZI WA NYIMBO MPYA YA DIAMOND NA JINSI ALIVYOTOA ZAWADI YA GARI KWA MSANII MSTAAFU "MZEE GURUMO"

Diamond Platnumz jana alifanya uzinduzi wa video ya wimbo wake mpya, Number 1 kwenye ukumbi wa Serena Hotel jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huo ulihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo ndugu zake, marafiki, wasanii wenzake na wadau mbalimbali wa muziki nchini.
Chege Chigunda akifuatilia kwa makini
Chege Chigunda akifuatilia kwa makini
Kwenye uzinduzi huo pia, Diamond alimpa zawadi ya gari msanii mkongwe aliyetangaza kustaafu muziki, Muhidin Gurumo kama heshima kwake.
Diamond akienda kumkabizi Mzee Muidin Ngurumo Gari
Diamond akienda kumkabidhi Mzee Muhidin Gurumo gari
Diamond akimuonyesha Mzee Ngurumo Gari ambayo amemzawadia
Diamond akimuonyesha Mzee Gurumo gari aliyomzawadia

Diamond akiongea na wadau walio fika
Diamond akiongea na wadau waliofika
Dully Sykes akiwa na Diamond wakiongea machache
Dully Sykes akiwa na Diamond wakiongea machache

Hao ndugu na Marafiki katika picha ya Pamoja
Ndugu na Marafiki katika picha ya pamoja
Hapa Diamond akimkabidhi Mzee Ngurumo Funguo ya Gari
Hapa Diamond akimkabidhi Mzee Gurumo funguo ya gari

Hapa Diamond akiongea machache na wasanii wenzake waliyo fika kumpa sapoti
Diamond akiongea machache na wasanii wenzake waliofika kumpa sapoti
Hili ndo Gari alilo pewa zawadi Mzee Ngurumo na Diamond
Hili ndo gari alilopewa Mzee Gurumo na Diamond
Hivyo ndivyo watu walivyo jitokeza kuja kuona New Video ya My No 1
Hivyo ndivyo watu walivyojitokeza kuja kuona video ya Number 1

Kama kawa burudani ilikuwepo kidigo
Kama kawa burudani ilikuwepo kidogo
Mzee Ngurumo akijaribu kidogo kupiga lesi baada ya kukabidhiwa Gari
Mzee Gurumo akijaribu kidogo kupiga lesi baada ya kukabidhiwa gari

Mzee Ngurumo akiongea machache na kumshukuru Diamond kwa kumpatia hiyo zawadi ya gari
Mzee Gurumo akiongea machache na kumshukuru Diamond kwa kumpatia zawadi ya gari
Nay wa Mitego akiwa pamoja na Madam Ritta
Nay wa Mitego akiwa pamoja na Madam Rita

Qeen Darleen na Bi Sandra
Queen Darleen na Bi Sandra
Rey Kigosi akifuatilia kwa makini sana
Ray Kigosi akifuatilia kwa makini sana

Wadau mbali mbali walio pata mualiko wakifuatilia
Wadau mbalimbali waliopata mualiko wakifuatilia
Wadau wa burudani wakifuatilia
Wadau wa burudani wakifuatilia

Wadau wakisubiri kwa hamu kuona kuona Video ya My no 1
Wadau wakisubiri kwa hamu kuona kuona video ya Number 1
watu wakifuatilia
Watu wakifuatilia

Asha Baraka,Qeen Darleen pamoja na Mama Diamond Bi Sandra
Asha Baraka,Queen Darleen pamoja na Mama Diamond
IMG_5498
IMG_5500
IMG_5510
IMG_5516
IMG_5517
IMG_5520
IMG_5522
IMG_5524
IMG_5525
IMG_5526
IMG_5527
IMG_5533
IMG_5534
IMG_5535
IMG_5537
IMG_5540
IMG_5541
IMG_5548
IMG_5554
IMG_5557
IMG_5558
IMG_5561
IMG_5564
IMG_5575
IMG_5579
IMG_5582
IMG_5586
IMG_5588
  IMG_5506