Thursday, February 21, 2013

ARSENAL 3-1 NA BAYERN, SASA YASUBIRI MIUJIZA MECHI YA MARUDIANO

FIRED UP ... Bayern Munich fans

ARSENAL wanaelekea ukingoni mwa michuano ya klabu bingwa Ulaya baada ya kipigo cha 3-1 kwenye uwanja wao wa nyumbani dhidi ya Bayer Munich ya Ujerumani.
Bayern waliwasambaratisha vijana wachovu wa Wenger kupitia mabao ya Toni Kroos, Thomas Muller na Mario Mandzukic.
FIRED UP ... Bayern Munich fans

Shangwe za mashabiki wa Bayern
Hata pale Podolski alipoipunguzia Arsenal bao dakika ya 55 na kuwa 2-1 bado ilionekana Arsenal wana mlima mrefu wa kupanda ili kushinda mechi ya marudiano ugenini.
LADY LUK ... Podolski scores after corner fluke
Podolski akiifungia Arsenal bao pekee
Vijana wa Wenger walibakiwa na tumaini pekee katika ligi ya mabingwa baada ya kutolewa na Blackburn kwenye kombe la FA Jumamosi iliyopita.
Walianza kupumbazwa dakika ya nane pale Kroos alipoujaza mpira wavuni kupitia krosi ya Thomas Muller.
KROOS CONTROL ... hero Toni turns in triumph
Kroos (kushoto) baada ya kufunga bao la kwanza
Dakika ya 21 mambo yakawa mabaya zaidi baada ya mpira wa kona wa Daniel Van Buyten kutemwa na kipa Szczesny na kumkuta Muller aliyeujaza wavuni na kuandika bao la pili.

MULLER TIME ... Thomas Muller makes it 2-0
Muller akiipatia Bayern bao la pili
Bayern Munich ikapigilia msumari wa mwisho kwenye jeneza la Arsenal dakika ya 77 baada ya Mandzukic kumalizia mpira wa krosi ya Arjen Robben aliyetokea benchi.
Katika mchezo mwingine, Porto iliifunga Malaga 1-0

No comments: