Thursday, February 21, 2013

KIMWANA WA TWANGA IPO PALE PALE, MAIMATHA ATUPWA NJE



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgZuD4rVoHNxfaxQKmTcu5Cl7zynhkGb4h1ERhXQu9dSOjB4RiL4gyJgIw3gWAiqLqRJLtz4tNf-LPVVdWSJVuhlI7qWTQhHNxFxmnO9GxG-9rhS6qkOmBOjk4FgAU0kGVTWCKgvgAGZig/s1600/Mai.jpgUONGOZI wa ASET unaomiliki bendi ya Twanga Pepeta, umesema mchuano wa Kimwana wa Twanga upo pale pale na unatarajiwa kufanyika baadae mwaka huu.
Mmoja wa viongozi wa Aset, Hassan Rehani ameiambia Saluti5 kuwa tofauti na uvumi uliozagaa kuwa mchuano huo umeyeyuka, ni kwamba Kimwana wa Twanga itaendelea kuwepo kila mwaka.
Rehani amesema badiliko pekee ni kwamba aliyekuwa mratibu wa Kimwana wa Twanga, Maimatha wa Jesse (pichani chini) hatakuwepo tena katika mchuano huo kwa vile hakidhi tena vigezo vinavyohitajika.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgZuD4rVoHNxfaxQKmTcu5Cl7zynhkGb4h1ERhXQu9dSOjB4RiL4gyJgIw3gWAiqLqRJLtz4tNf-LPVVdWSJVuhlI7qWTQhHNxFxmnO9GxG-9rhS6qkOmBOjk4FgAU0kGVTWCKgvgAGZig/s1600/Mai.jpg
Hivi karibuni Maimatha alitangaza kuanzisha kinyang’anyiro kingine kitakachojulikana kama Kigoli kwa kushirikiana na Extra Bongo na Hassan Rehani ameitaja hali hiyo kama moja ya vitu vinavyomuondolea Maimatha vigezo vya kuratibu Kimwana wa Twanga.
Kwa mujibu wa Hassan mchuano huo ambao hushirikisha mabinti wenye vipaji vya kunengua mitindo mbali mbali ya Twanga Pepeta, utafanyika baada ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.Via saluti5

No comments: