Baada ya shutuma za rushwa ya ngono kuzidi kwa waandaaji wa shindano
la Miss Tanzania, uongozi unaosimamia shindano hilo umesema kama kuna
mrembo yeyote ambae amewahi kuombwa rushwa hiyo ya ngono ajitokeze.
Mkurugenzi Hashim Lundenga amesema “kuna kushutumiwa kwamba tunachukua rushwa ya ngono kutoka kwa Wasichana kitu ambacho sio kweli, hakuna msichana aliesema ameingia kambini au ameshinda kwa sababu ametoa rushwa ya ngono, katiba yetu inakataza kabisa yeyote kujihusisha na hilo”
.
Moja
ya kesi hizo ni pamoja na ya Mchungaji aliemuondoa mwanae baada ya
kupewa ubalozi wa kinywaji chenye kilevi, mrembo mwingine alikua Nadya
aliekua masomoni Chuo kikuu familia yake ilikataa kabisa mtoto wao
kushiriki.
.
Kwa kumalizia, Lundenga amekiri kwamba wanao utaratibu, sheria na kanuni kwenye katiba yao ambayo imepitishwa na Serikali ikiwa na maagizo mablimbali ikiwemo marufuku ya kiongozi yeyote kuomba rushwa ya ngono.
Pamoja
na kuzushiwa hizo kashfa, amesema idadi ya Warembo wanaotaka kushiriki
haijapungua bali imeongezeka kwa sababu Wasichana ndio wanazidi
kujitokeza.
No comments:
Post a Comment