Tuesday, January 15, 2013

WEMA SEPETU AJIKUTA AKIWAKUMBATIA WAZEE AKIKWEPA KUGUSWA NA "PANZI"

KATIKA hali isiyo ya kawaida ya kutozoea maisha ya kijijini, msanii asiyeishiwa matukio, Wema Sepetu, hivi karibuni alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuwakumbutia wazee wa kijijini akikwepa panzi  pindi walipokuwa katika ziara ya uzinduzi wa mpango wa Kilimo Kwanza kwa vijana eneo la Kwandelo, Kondoa.


Wakati wakiwa katika harakati za kuhamasisha kilimo kwanza , panzi alianza kuruka ruka eneo hilo ambalo ni sehemu ya shamba hali iliyomchanganya msanii huyo na kuanza kukimbia hovyo huku akijifunika usoni na mkoba wake akikimbilia sehemu waliyokuwa wamesimama wazee.


Hata hivyo baada ya kurejea Dar mwandishi wetua  alizungumza na mrembo huyo ambaye  alisema kuwa hakuwai kumuona mdudu huyo hivyo hali hiyo ilimpa wasiwasi mkubwa kwa kuhisi anaweza kudhuliwa afya yake

No comments: