Saturday, May 11, 2013

WANAFUNZI WA CHUO WAPATA KIBANO BAADA YAKUKUTWA NJE YA GETI LA CHUO SAA NANE USIKU KWENYE GETI LA KIGO CHEKI PICHA HAPA

WAREMBO watatu wanaodaiwa kuwa ni madenti wa chuo kikuu kimoja jijini Dar, waliojitambulisha kwa jina mojamoja, Rachel, Neema na Suzan, wamekumbana na balaa zito baada ya kupokea kibano cha kutosha, Ijumaa lina mkanda kamili.

Soo: Warembo hao watatu wakificha sura zao kwa aibu baada ya kubambwa na kushushiwa kichapo getini kwa kigogo.

Tukio hilo lililonaswa laivu na gazeti hili lilitokea maeneo ya Kijitonyama, jijini Dar, usiku wa saa 8:00, mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo madenti hao walipokea kibano ‘hevi’ kutoka kwa Polisi Jamii.

Kipondo: Madenti hao baada ya kusurubiwa na Polisi Jamii.

KERO
Warembo hao walifikwa na kasheshe hilo baada ya kugeuka kero kwenye geti la kigogo mmoja (jina linahifadhiwa kwa sababu maalum) kwa kuwa walionywa mara kadhaa kuacha kupanga foleni katika eneo hilo na kujihusisha na vitendo vya ngono.
“Unajua walikuwa kero sana. Yaani asubuhi kukicha utakuta mipira ya kiume imetapakaa kila sehemu. Mbaya zaidi utakuta watoto wakicheza mchana wanaokota hiyo mipira ya kiume na kupuliza kama puto,” alisema shuhuda mmoja aliyeamshwa na makelele ya warembo hao wakati wakila kibano.



Vilio: Warembo hao wakilia baada ya kichapo.

Aliendelea: “Unajua wakikaa hapa ni hatari tupu kwani wanaume wanaokuja kuwafuata wanaweza wakatudhuru kwa sababu hatuwajui.”

MALALAMIKO
Katika tukio hilo, walinzi hao wakiwa kwenye doria, walipokea malalamiko kwa mara 1000, kutoka kwa kigogo huyo akiomba msaada wa kuwaondoa warembo hao getini kwake wanaodaiwa kujiuza eneo hilo.
LENGO KUMNASA KIGOGO
Habari nyingine zilieleza kuwa wadada hao wamekuwa wakiweka mitego yao nje ya nyumba hiyo ikidaiwa kwamba lengo ni kumnasa kigogo huyo ili kumuuzia biashara yao kwa kuwa ni ‘mkataji’ mzuri wa mkwanja.
Mbali na hilo, pia ilidaiwa kuwa wanaume wapenda ngono rejareja na hatarishi huwafuata eneo hilo kupata huduma yao.
Ilidaiwa kuwa walinzi hao walielezwa kuwa katika kukuza biashara hiyo haramu, warembo hao wamekuwa wakiwabugudhi wakazi wa eneo hilo hadi kufikia hatua ya kuwagongea madirishani na kusimamisha magari hovyo.
WAONESHA NYETI
Huku wakijua wamepata wateja, kundi la kinadada hao wakiwa na vinguo vya kimitego na wengine kujifunua na kubaki nusu utupu ili kuwaonesha wanausalama hao nyeti zao wakijua ni wateja ndipo wakakutwa na kasheshe hilo.

KIBANO
Wanausalama hao, bila kuchelewa waliwazingira warembo hao na kuwanasa kisha kuwapa kibano lakini katika purukushani hiyo wengine walifanikiwa kupata upenyo na kuchoropoka.
WAFUNGA MTAA
Katika kibano hicho, makelele ya warembo hao yalisababisha watu kuamka na kufunga mtaa.
Kutokana na timbwili hilo la akina dada hao kuwa zito, iliwabidi polisi hao jamii watumie nguvu ya ziada kuwatuliza kabla ya kuwapeleka mbele ya sheria.
FUNDISHO
Baada ya warembo hao ‘kutaitiwa’ walipakizwa kwenye Bajaj na kupelekwa kituo cha polisi ili wafikishwe mahakamani.
Kwa kashikashi waliyopata ni dhahiri kuwa kilichowapa madenti hao ni fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.

No comments: