Friday, November 1, 2013

PICHA,RAHA YA UTOTO,MTOTO AKALIA KITI CHA PAPA NA KUGOMA KUONDOKA

Mtoto wa kiume aliyepata utambulisho wa nguo aliyokuwa amevaa ‘the boy in yellow’ alijikuta anachukua ‘attention’ ya waumini wote waliohudhuria siku ya familia St Peter’s Square huko Vatican baada ya kuvamia jukwaani na kukaa na papa Francis kwa muda wa dakika kadhaa.
Kiongozi mkuu wa kanisa Katoliki Papa Francis alikuwa akizungumza mbele ya umati mkubwa wa familia mbalimbali zilizohudhuria sherehe za siku ya familia. Baada ya mtoto huyo kupanda jukwaani alienda mbele ya papa na kumtazama na kuzunguka hapa na pale japo hakufanya fujo ya aina yoyote.
 
Makadinali walijaribu kutumia njia za kumshawishi kutoka kama kumpatia pipi, lakini mtoto huyo aligoma kuondoka. Papa alimgusa kichwani na kutabasam akamwacha na kuendelea na alichokuwa akikifanya.
Kuna wakati papa akiwa amesimama anazungumza mtoto huyo alimkumbatia miguu lakini papa alimwacha.
Baadaye Vatican walishare moja ya picha za tukio hilo katika akaunti yao ya Instagram ikimwonesha mtoto huyo akiwa amekalia kiti cha papa na kuandika ‘A special guest with #popefrancis.
Source: Mail Online

No comments: