Tuesday, April 30, 2013

MAELEZO YA JUMLA KUHUSU MKOA KAGERA


 
Mkoa wa Kagera unapatikana kaskazini magharibi mwa nchi ya  Tanzania. Makao makuu ya mkoa yapo katika mji wa Bukoba umbali wa kilometa 1500 kutoka Dar es Salaam, mkoa huu unapakana na nchi ya Uganda kwa kaskazini, Rwanda na Burundi kwa upande wa magharibi mkoa wa Kigoma, Mwanza kwa upande wa kusini na ziwa Victoria kwa upande wa mashariki. Vile vile mkoa wa Kagera uko kusini mwa ikweta kati ya 1 “00” na 2”45” latitudi. Kwa Iongitudo uko katika nyuzi 30”25” na 32”40” Mashariki mwa ‘greenwich'.
Mkoa wa Kagera ulijulikana kama “Ziwa Magharibi” jina hili lilidumu katika kipindi cha ukoloni na baada ya uhuru mpaka mwaka 1979 baada ya vita kati ya Tanzania na Uganda.
Mkoa ulipata jina hili kutokana na mto Kagera ambao hutiririsha maji yake kutoka Rwanda kupitia kaskazini na kumwaga maji yake katika ziwa Victoria.
Mkoa wa Kagera una jumla ya eneo la kilomita za mraba 39,168 kati ya hizo kilometa za mraba 28,513 ni eneo la nchi kavu za kilomita 10,655 ni eneo la maji. Ukiacha mbali wilaya za Biharamulo na Chato ambazo ni tambarare sehemu kubwa ya mkoa ni yenye milima na vilima vilivyogawanywa na mabonde yenye matingatinga. Upande wa magharibi wa mkoa mito mingi inamwaga maji yale katika mto Kagera ambao nao humwaga maji yake katika ziwa Victoria.

Hali ya hewa
Hali ya hewa ya mkoa wa Kagera kwa ujumla ni ya joto la wastani wa 26.02 sentigredi. Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800-1,100 kwa mwaka kati ya mwezi Septemba na Januari na kati ya mwezi Machi na Mei. Mvua hizi ndizo zinazowezesha kuwepo kwauoto wa asili wa kuvutia katika maeneo mengi ya mkoa. Kwa miaka ya kawaida mkoa hupata mvua za uhakika za vuli na masika ambazo ni muhium kwa shughuli za kilimo na ufugaji.

UTAWALA
 
Wakati tunapata UHURU, mkoa wa Kagera ulikuwa na jumla ya wilaya nne (4), wilaya hizo ni Ngara ambayo ilianzishwa mwaka 1947, Biharamulo, Bukoba, na Karagwe mwaka 1958 ambayo ilizinduliwa rasmi na gavana wa kiingereza Sir Richard Turnbul. Aidha, mwaka 1975 wilaya mpya ya Muleba ilianzishwa kutoka kwenye wilaya ya Bukoba na mwaka 2007 wilaya ya Chato na Missenyi zilianzishwa na kuunda jumla ya wilaya 7 za mkoa wa Kagera.
Kwa sasa mkoa wa Kagera una jumla ya wilaya saba (7) na halmashauri 8. Wilaya hizo ni Bukoba, Muleba, Biharamulo, Ngara, Chato, Karagwe, Missenyi na Ngara. Halmashauri ni Bukoba Manispaa, halmashauri ya wilaya ya Bukoba, Muleba, Biharamulo, Ngara, Chato, Karagwe na Missenyi.
Kisiasa mkoa una jumla ya majimbo 10 ya uchaguzi (Muleba 2, Karagwe 2, Ngara 1, Biharamulo 1, Missenyi 1, Bukoba Manispaa 1, Bukoba Vijijini 1 na Chato jimbo 1).

IDADI YA WATU
 
Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 1967 mkoa ulikuwa na watu 658,712, mwaka 1978 watu 1,009,379, mwaka 1988 mkoa ulikuwa na watu 1,326,183 na mwaka 2002 watu 2,033,888. Ongezeko la idadi ya watu lilikuwa kwa wastani wa asilimia 2.7. Aidha, mwaka 2011 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002 mkoa unakadiriwa kuwa na idadi ya watu 2,746,058.

 
Halmashauri Ya Wilaya
Idadi ya Watu

1978
1988
2002
MAOTEO 2011
Missenyi
-
-
-
174,889
 
Bukoba (V)
296,462
343,950
395,130
467,129

Bukoba (M)
36,914
47,009
81,221
153,016

Muleba
217,493
274,447
386,328
492,404

Chato
-
-
-
383,162
 
Biharamulo
165,580
209,524
410,794
252,218

Karagwe
185,013
292,589
425,476
542,517

Ngara
107,917
158,658
334,939
422,044

JUMLA
1,000,379
1,326,183
2,033,888
2,746,058
 
Chanzo: Ofisi Kuu ya Takwimu Taifa (NBS) , 2011
 
HISTORIA YA MKOA WA KAGERA
Mkoa huu haukuitwa Kagera bali ulikuwa moja ya maeneo yaliounda jimbo lililoitwa Lake Province. Jimbo hili lilijumuisha Wilaya ya Bukoba, Musoma, Shinyanga na Tabora. Baadaye ulibadilishwa jina na kuitwa ‘West Lake Region' (Ziwa Magharibi) na kujumuisha Wilaya 4 za Ngara, Biharamuro, Karagwe na Bukoba.
Kabla na baada ya kuja kwa wakoloni mkoa wa Kagera ulikuwa na utawala wa Kimila (Chiefdoms) uliogawanyika katika himaya 8. Himaya hizo ni pamoja na Kyamutwara, Kihanja (Kanazi), Kiziba, Ihangiro, Bugabo, Karagwe, Biharamulo (Rusubi) na Maruku (Bukara).
Baadhi ya Watemi waliotawala himaya hizo ni pamoja na Emmanuel Rukamba (Kyamtwara), Rumanyika (Karagwe), Kasusura (Biharamulo), Lugomola (Bukara), Rutinwa (Kiziba), Kayoza (Bugabo), Kahigi (Kihanja) na Nyarubamba (Ihangiro). Kila mtemi alikuwa na walinzi wake walioitwa Warugaruga.
Wakazi wa asili ya Kagera ni wabantu na wengi wao wana asili ya Bunyoro. Wanaongea lugha sawa na ile ya Wanyoro, Wanyankole, Watoro na Wakiga. Busubi na Bugufi wana lugha na desturi sawa na Watusi, Wahutu na Waha. Lakini makabila hayo ni ya Wabantu wa Ziwa (Interlacustrine Bantu) na yanafanana mila na desturi. Makundi hayo yaligawanyika kati ya wachungaji (Bahima) ambao walitawala na wakulima (Bairu) ambao walitawaliwa na mara nyingi kudharauliwa. Bahima (Balangira) walikuwa na koo chache zipatazo 20 na walitawaliwa na Wahinda, Wabito na Wankango.
Bairu walikuwa na Koo kama 130 zenye mashina 24 ambayo kiasili walikuwa Bairu lakini kwa kuoa katika Bahima au kufanya kazi kwa Watemi walipandishwa hadhi na kuwa Bahima (Batware). Kila ukoo uliitwa jina la Baba mwanzilishi wake na kina ukoo ulikuwa na kitu walichokatazwa kula (Omuziro) na mnyama walioshirikishwa nae (Ekyerumono).
Mkoa ulibadilishwa jina na kuitwa Kagera mwaka 1979 baada ya vita ya Tanzania na Uganda. Chini ya uongozi wa Mkuu wa Mkoa aliyekuwepo wakati huo Capt. Peter Kafanabo jina la Kagera lilipendekezwa kwa sababu ya mto Kagera unaogusa sehemu kubwa ya Wilaya zote zinazounda Mkoa wa Kagera.
Uchumi wa wenyeji wa Kagera ulijikita katika mashamba ya migomba. Chakula chao kikuu ni ndizi katika aina zake mbalimbali. Katika mashamba yao hulima mazao mengine kufuatana na msimu. Mazao hayo ni pamoja na maharage, mihogo, mahindi na mboga. Baada ya kuja kwa wazungu waliongeza ulimaji wa kahawa kama zao la biashara lililowasaidia kujiongea kipato.

 





 
 

 

 
 
 
 
 

 
 
 
 
 
MAJIMBO YA UCHAGUZI
Mkoa unayo majimbo ya Uchaguzi 10 na wapo Wabunge 9 wa kuchaguliwa na Wabunge 3 wa viti maalum. Jumla ya Wabunge 11 wanatoka chama cha Mapinduzi (CCM) na Mbunge 1 anatoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo. Majina ya waheshimiwa wabunge na majimbo wanayowakilisha pamoja na wale wa viti maalumu ni kama ifuatavyo:-

 
Na
Jina La Mbunge
Jimbo
Chama
Wilaya
1.
Mhe. Hamis Sued Kagasheki
Bukoba Mjini
CCM
Bukoba
2.
Mhe. Jason Samson Rweikiza
Bukoba Vijijini
CCM
Bukoba
3.
Mhe. John Pombe Magufuli
Chato
CCM
Chato
4.
Mh. Dk Antony Mbasa  
B'mulo Magharibi
CHADEMA Biharamulo
5.
Mhe. Begumisa Gosbert Blandes
Karagwe
CCM
Karagwe
6.
Mhe. Eustace Katagira
Kyerwa
CCM
Karagwe
7.
Mhe. Anna Tibaijuka
Muleba Kusini
CCM
Muleba
8.
Mhe. Charles Mwijage
Muleba Kaskazini
CCM
Muleba
9.
Mhe.Asumpta Nshunju Mushama
Nkenge
CCM
Missenyi
10.
Mhe. Deogratius Ntukamazina
Ngara
CCM
Ngara
11.
Mhe. Bernadetha Mushashu
Viti Maalumu
CCM

12.
Mhe. Elizabeth Batenga
Viti Maalum
CCM

13.
Mhe. Conjester Rwamulaza
Viti Maalum
CHADEMA

 
Vyama vya siasa vinavyoendesha shuguli zake vizuri hapa mkoani ni pamoja na CCM, TLP, NCCR - Mageuzi, CUF, UMD, UDP, na CHADEMA. Hatuna matukio ya kukiukwa kwa sheria na utaratibu kwa vyama vya siasa.

HALI YA UCHUMI NA MAENDELEO YA MKOA
Uchumi wa mkoa unategemea zaidi kilimo ambapo zaidi ya asilimia 70 ya watu wanajishughulisha na kilimo cha mazao ya chakula na biashara. Shughuli za uvuvi, mifugo,viwanda na madini zinachangia pia katika uchumi wa mkoa.
Kwa kuzingatia malengo ya Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (MKUKUTA) , Dira ya Taifa ya mwaka 2025 na malengo ya Milenia, Mkoa wa Kagera unaendelea kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo na umepiga hatua katika sekta za uchumi, miundo mbinu na huduma za jamii. Hata hivyo pamoja na hatua hizi zilizopigwa, juhudi za wananchi mkoani za kujiletea maendeleo zinakumbana na matatizo na vikwazo mbalimbali ambavyo vimeendelea kupatiwa ufumbuzi kwenye mipango ya maendeleo ya Mkoa.

KANDA ZA IKOLOJIA (ECOLOGICAL ZONES) :
Mkoa wa Kagera umetenganishwa katika Kanda tano za kilimo kuzingatia mwinuko wa maeneo hayo kutoka usawa wa bahari na kiwango cha unyeshaji wa mvua.
 
Ukanda wa kwanza : Ukanda huu unajumuisha maeneo ya mashariki ya wilaya ya Bukoba na Muleba yanayoambaa kandokando ya ziwa victoria na uko katika mwinuko wa mita 1,300 mpaka 1,500 kutoka usawa wa bahari. Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800 - 1,750 kwa mwaka. Shughuli kuu za kiuchumi katika eneo hili ni kilimo cha ndizi, maharagwe, mahindi na kahawa. Eneo la ukanda huu ni asilimia 17 ya eneo la Mkoa.
 
 
 
Ukanda wa pili : Huu ni ukanda wa juu ulioko kwenye mwinuko wa mita 1,400 mpaka 1,800 kutoka usawa wa bahari. Ukanda huu unajumuisha maeneo ya juu ya wilaya ya Karagwe na Ngara na mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800-1,000 kwa mwaka. Mazao yanayolimwa kwenye ukanda huu ni ndizi, maharagwe, mahindi na kahawa. Eneo la ukanda huu ni asilimia 19 ya eneo la mkoa.
 
 
Ukanda wa Tatu : Ukanda huu uko katika mwinuko wa mita 1,000 kutoka usawa wa bahari na unajumuisha wilaya ya Ngara ,Biharamulo na Chato.Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 750-800 kwa mwaka. Shughuli kuu za kiuchumi ni uzalishaji wa mazao ya mahindi, mihogo, mpunga, mtama, karanga na pamba. Eneo la ukanda huu ni asilimia 27 ya eneo la mkoa.
Ukanda wa Nne : Ukanda huu upo kwenye mwinuko wa mita 1,000 kutoa usawa wa bahari na unajumuisha maeneo ya mashariki ya wilaya ya Karagwe,wilaya ya Misenyi na maeneo ya magharibi ya wilaya ya Bukoba. Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800-1,000 kwa mwaka. Shughuli kuu za kiuchumi ni kilimo cha mazao ya mahindi,maharagwe na ufugaji. Eneo la ukanda huu ni asilimia 10 ya eneo la mkoa.
 Ukanda wa Tano :Ukanda huu unajumuisha maeneo ya kaskazini ya wilaya ya Karagwe na Misenyi na uko kwenye mwinuko wa mita 1,000 kutoka usawa wa bahari .Ukanda huu unapata mvua za wastani wa milimita 750-800 kwa mwaka.Sehemu kubwa ya ukanda huu ni misitu ya hifadhi na mapori ya akiba. Eneo la ukanda huu ni asilimia 27 ya eneo la mkoa.

 


 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

No comments: