Sunday, September 29, 2013

MISAADA YA KIMAENDELEO JIMBONI KALENGA YAMNYIMA USINGIZI WAZIRI DR MGIMWA


Dr Wiliam Mgimwa
KUELEKEA uchaguzi  mkuu  mwaka 2015 mbunge  wa  jimbo la kalenga na waziri fedha na uchumi Dr Wiliam Mgimwa ameanza kuingia na hofu ya kupata  upinzani mkali katika jimbo lake  la  uchaguzi na  kuwataka wapiga  kura  kuwapuuze wadau wa maendeleo  wanaofika  kusaidia kutatua  kero za  wananchi.
 
Katika  kile kinachoonyesha  kuwa  waziri Dr Mgimwa ameanza kuingiwa na hofu ya  kushindwa katika  uchaguzi  mkuu mwaka 2015  hata kabla ya wana CCM  wanaotaka  kuwania ubunge kujitangaza hadharani ,Dr Mgimwa ameponda misaada  hiyo   na kuwataka  wananchi kuwapuuza wadau  wanaojitolea  kusaidia matatizo ya  wananchi jimboni kwake.

Wakizungumza na mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com ,John  Adam   na  Sarah Sanga  wakazi wa kata ya Nzihi walisema  kuwa  hawakutarajia   kusikia mbunge  wao  akionyesha kuwabeza  watoto  wao  wanaofika  katika vijiji  vyao  walivyozaliwa  kusaidia matatizo ya wananchi.

Alisema  Adam kuwa  ni  vema  wabunge na madiwani kuendelea  kuwa na mshikamano  wa  kweli kwa  wadau mbali mbali  wa maendeleo  wanaofika kusaidia shughuli za maendeleo  katika maeneo yao badala ya  kuendelea  kuingizwa misaada  hiyo katika sura ya  kisiasa .

Kwani  alisema  kuwa  hatua  ya  mbunge Dr Mgimwa  kuwataka  wananchi  wa  jimbo  hilo la Kalenga  kuwapuuza  watu mbali mbali  wanaofika  kusaidia  shughuli za kimaendeleo  katika  jimbo  hilo ni kauli isiyo na faida kwa  maendeleo ya  wana kalenga .

"  Hivi  kweli  siasa itugawe  wananchi na familia zetu ...leo mtoto  wetu anapokuja  kutusaidia  misaada  ya kimaendeleo  tukatae kwa  sasa  mbunge wetu  hapendi  watu hao kutusaidia sasa  nini maana ya maendeleo"

Huku Bi Sanga  akimtaka  mbunge Dr Mgimwa  kuachana na  hofu ya kisiasa na kuwa  wanaoweza  kufanya mabadiliko  ya mbunge ama chama kipi kitawale  jimbo la Kalenga ni  wananchi ambao  mwisho  wa  siku  wanapima kazi iliyofanywa na mbunge  ama  diwani  husika na kama  hakuna  jipya  hawataangalia mtu  wala chama wanatoa hukumu .

Mbunge  Mgimwa katika moja kati  ya mikutano yake  aliyoifanya katika jimbo la Kalenga  alipata  kutoa kauli iliyonukuliwa na gazeti la Majira  la Jumamosi tarehe 28/9/2013  kauli inayoonyesha  wazi  kuwa ameanza  kupata  hofu ya  kisiasa  jimboni  baada ya kutamka  wazi  kuwa  wapo  watu  wanazunguka kutoa misaada vikiwemo  vitanda  katika Hospital ya Ipamba .huku zikiwa ni siku  chache  kupita toka mkazi wa Nyamihuu Jackson Kiswaga  kukabidhi  msaada  huo wa vitanda  katika  Hospital  hiyo kama fadhila  yake kwa Hospital kutokana na kulazwa  hapo na kuhudumiwa  vema ,msaada ambao hata  hivyo mbunge  huyo anadaiwa  kuwa na taarifa  nao.

No comments: